Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Unapoona maraisi wa tano tu kutoka Afrika wamekuja kushiriki katika hafla ya kumpongeza JK na ushindi wa mezani basi ujue mabadiliko Afrika bado yana safari ndefu................
Maraisi hao ni Mwai Kibaki wa Kenya, Mugabe wa Zimbabwe, Rupiah Banda wa Zambia, Kabila wa Kongo na Zuma wa Afrika ya Kusini...............
Kibaki, Mugabe, Kabila na Banda hawahitaji utambulisho hata chembe kwenye ulingo wa kuchakachua kura..........
Zuma atakumbukwa kwa jinsi alivyompindua bosi wake Bw. Thabo Mbeki isivyo halali na kinyume cha sheria....................Matarajio ya wasauzi kuwa Zuma angeleta mabadiliko ya kiuchumi sasa yamefifia kabisa na wanafikiria namna ya kumtupia virago vyake............
Kutokana na viongozi Afrika kuingia madarakani bila ya ridhaa ya wapigakura ndiyo maana huchukia utawala bora na hufanya jitihada za khali na mali kuuchelewesha kwa sababu utawala bora ni tishio lao kuendelea madarakani....................
Hii yatushibisha kwa nini AU ipo tayari kubeza maelekezo ya mahakama za kimataifa ili kuwalinda akina Al-Bashir wa Sudan na kukwepa kuwakamata ili wajibu tuhuma za mauaji kule Darfur................Bila ya misingi ya kiutu ya utawala bora Afrika itaendelea tu kuwa shamba la bibi na kutafunwa na wajanja wachache...............Kibaki alikwisha mwalika Al-Bashir Kenya na kudharau maelekezo ya mahakama ya kimataifa kuwa akamatwe.........Huu ni mfano mzuri wa viongozi wa Afrika wasivyopenda kuwajibishwa ila ni magwiji wa kuwaajibisha mahasimu wao kisiasa............ kama kule Rwanda kugombea uraisi dhidi ya Kagame ni kosa la jinai na waweza kuhukumia kifungo cha maisha.................Kweli Afrika bado tunayo safari ndefu ya kujikomboa.................
Maraisi hao ni Mwai Kibaki wa Kenya, Mugabe wa Zimbabwe, Rupiah Banda wa Zambia, Kabila wa Kongo na Zuma wa Afrika ya Kusini...............
Kibaki, Mugabe, Kabila na Banda hawahitaji utambulisho hata chembe kwenye ulingo wa kuchakachua kura..........
Zuma atakumbukwa kwa jinsi alivyompindua bosi wake Bw. Thabo Mbeki isivyo halali na kinyume cha sheria....................Matarajio ya wasauzi kuwa Zuma angeleta mabadiliko ya kiuchumi sasa yamefifia kabisa na wanafikiria namna ya kumtupia virago vyake............
Kutokana na viongozi Afrika kuingia madarakani bila ya ridhaa ya wapigakura ndiyo maana huchukia utawala bora na hufanya jitihada za khali na mali kuuchelewesha kwa sababu utawala bora ni tishio lao kuendelea madarakani....................
Hii yatushibisha kwa nini AU ipo tayari kubeza maelekezo ya mahakama za kimataifa ili kuwalinda akina Al-Bashir wa Sudan na kukwepa kuwakamata ili wajibu tuhuma za mauaji kule Darfur................Bila ya misingi ya kiutu ya utawala bora Afrika itaendelea tu kuwa shamba la bibi na kutafunwa na wajanja wachache...............Kibaki alikwisha mwalika Al-Bashir Kenya na kudharau maelekezo ya mahakama ya kimataifa kuwa akamatwe.........Huu ni mfano mzuri wa viongozi wa Afrika wasivyopenda kuwajibishwa ila ni magwiji wa kuwaajibisha mahasimu wao kisiasa............ kama kule Rwanda kugombea uraisi dhidi ya Kagame ni kosa la jinai na waweza kuhukumia kifungo cha maisha.................Kweli Afrika bado tunayo safari ndefu ya kujikomboa.................