geophysics
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 904
- 166
Ni kweli Companero naona huyo namba 4 ni kaka yako etie....Comrade Companero...... kapotelea wapi?
yupo Atletico Madrid na kina Diego Forlan,Sergio Aguero Kun na ndio mabingwa watetezi wa europa cupJose antonio Reyes
Yu wapi Rene Higuita yule kipa wa Colombia?
Nkwingwa....Umenikumbusha mbali sana babu.....Huyu jamaa mzee wa 'Scorpion kick' alikuwa na mbwembwe na vituko golini dizaini ya Juma Pondamali 'Mensah'....Kwa mujibu wa wikipedia jamaa kastaafu soka mwezi January mwaka huu akiwa anadakia Deportivo Pereira ya kwao Colombia
René Higuita - Wikipedia, the free encyclopedia
Kuna wakati Colombia ilicheza mechi ya kirafiki (nadhani) na England pale Wembley stadium...jamaa aliokoa goli kwa sarakasi flani hivi....mpaka sasa sijawahi kuona tena kipa akiokoa goli kwa njia ile. Unaikumbuka hiyo Nkwingwa?
Hao wote wamestaafu soka,kuna mwingine anaitwa Yildray Basturk ni mfupi anaonekana kama mjapan yupo blackburn rovers,alicheza na kina Ballack,Lucio,Placente,Neuville na Berbatov pale Bayer Leverkusen 2002 inacheza final champions league baada ya kuwatoa Man Utd ,vs Real Madrid Zidane anafunga bao maridadi la ushindi.Wako wapi kina Hassan Sas, Ilhan Mansiz, wale jamaa wa uturuki waliofika semifinal world cup 2002?
Wachezaji wengi wanaokuwa moto kwenye age 17-23,huwezi kuwakuta ktk age 30 wakifanya mambo makubwa. Huwa wanakuwa wametumika vya kutosha kuweza kuhimili kashkash na wengine hupotea sababu ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu na wanapokuwa wamepona wanapata wakati mgumu kurudi kwenye kiwango chao,hivyo makocha wengine huwaacha bench au kuwatoa kwa mkopo kwenye timu ambazo wengi huwa hatuna mazoea ya kuzifuatilia kwa hiyo huwa wanapotea katika fikra zetu japo huko waliko kiwango huwa juu.Mosesk: Uko sahihi kwa kiasi fulani ila hapa suala ni wachezaji hao kuisha kabla ya wakati - Aimar alitakiwa awe anatesa pamoja na Messi kwenye timu ya taifa; yaani kuna siku walicheza pamoja timu ya taifa na Messi akafurahi sana kuungana na mtaalamu mwenzake waliyetesa pamoja kwenye timu ya taifa ya yosso; Ronaldinho wachambuzi wote wa soka wanakubali kuwa bado umri unamruhusu kutesa katika kiwango chake cha zamani ila amepoteza hamu yake ya kufanya mambo mazito kutoka na msongo wa matatizo ya nje ya uwanja - akitatua hilo basi atarudisha tu kasi yake; Okocha si wa kustaafu bila kuwa mchezaji bora wa dunia katika viwango vya Maradona na Messi; Signori alikuwa mkali kuliko hata Baggio ila Azzuri haimkumbuki; Asprilla alipaswa kuifikisha Colombia mbali; na Companero angezaliwa kwingine angetesa!
Kweli: ni kweli Van Basten alipotea kutokana na kuumia, alikuwa anapiga mabao Van Nilsteroy cha mtoto!
Nilibahatika kuona mechi moja,nadhani mwaka juzi,jamaa alikokota mpira mpaka katikati ya uwanja na kwa mshangao wa wengi, akatoa pasi kwa adui na halafu akageuka haraka kurudi golini kabla hajafika akakuta gozi linadundadunda ndani ya kimia!!!Yu wapi Rene Higuita yule kipa wa Colombia?
No! Kipaji cha mtu huyu hakikupotea sababu ya bangi. Alivunjika mguu ktk mechi ya FA Cup final na wakati huo akitakiwa kwenda ku join Lazio Rome ya Italy,so alikwenda Italy akiwa majeruhi na akakosa namba katika kikosi cha kwanza. Waingereza wakanzisha mkakati wa kumrudisha nyumbani,hivyo Headlines za magazeti ya Uingereza zikamchanganya mno na ndipo alipohamia Rangers ya Uskoch ambako alikuwa moto.Paul Gasgoine 'Gazza' - Mabangi nibangue yalifanya kipaji chake kipotee kabla ya wakati!
Diego Armando Maradona - Madawa ya kulevya yalifanya tukose uhondo wake WC 1994!
Huyo aliyemsahau alikuwepo 1994, alitolewa kwa red card ktk mechi na USA baada ya kumpiga kwa kiwiko Tab Ramos (hapa nadhani gutierez anakumbuka vizuri,nshazeeka sasa!!!)1998...
Tafarer, cafu, carlos, baiano aldair...
2002...
Marcos, cafu, carlos, roque Jr, edmilson, lucio...
kati ya hao yupo huyo uliyemsahau?
Dinho alimalizwa na penzi la mtoto wa Rijkaardt!! Jamaa akaanza kumweka ubaoni,akakasirika sana na kuanza kukacha mazoezi, kisaikolojia, benchi lilimmaliza.Nasisitiza: Huyo ni kivuli cha Dinho tunayemjua!
Narudia: Kwa umri wake Dinho hastahili kuisha!
Nakumbusha: Bado Dinho anapaswa kukimbiza!
Martin Dahlin naye alishafika tamati maana wakati anasumbua wc 98 alikuwa aged,ila Thomas Brolin....aliishia mapemaHapa tunazungumzia tu wachezaji waliopotea kabla ya wakati wao japo walikuwa na kiwango cha juu sana, yaani, ama walistaafu au walikwisha kabla ya muda wao - watu kama Dahlin wa Sweden na Viola wa Brazil!
Huyo aliyemsahau alikuwepo 1994, alitolewa kwa red card ktk mechi na USA baada ya kumpiga kwa kiwiko Tab Ramos (hapa nadhani gutierez anakumbuka vizuri,nshazeeka sasa!!!)
Dinho alimalizwa na penzi la mtoto wa Rijkaardt!! Jamaa akaanza kumweka ubaoni,akakasirika sana na kuanza kukacha mazoezi, kisaikolojia, benchi lilimmaliza.
Huyohuyo Gang Chomba, ni boy friend wa binti wa Frank Rijkaardt na walikuwa wakijirusha sana, binti baada ya kuombwa na baba yake amwache Dinho,akatishia kujiua,Dinho huyuhuyu ambaye Jana kawapiga goli Auxere dk ya 91 na kisha kuifanya Milan kufuzu au kuna Dinho mwingine wa Mbagala maji matitu