Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,481
- 46,005
Ikiwa ni miaka miwili imepita tangu marufuku ya kutengeneza na kutumia mifuko ya plastiki kupitishwa nchini bado kuna vimifuko vya plastiki ambavyo hutumika zaidi kwenye mabucha ya nyama na biashara ya matunda.
Kama serikali ilikataza matumizi ya mifuko ya plastiki kwa sababu ya athari zake nyingi na za muda mrefu katika mazingira ni sababu gani imeendelea kuruhusu hii mifuko ya plastiki nyepesi kuendelea kutumika baadaye katika baadhi ya biashara? Umefika wakati sasa wa kuharamisha kabisa mifuko yoyote ya plastiki ambayo bado inaendelea kutumika.
Tuyalinde mazingira yetu kwa nguvu zote.Ni wajibu wetu kwa kizazi chetu na kijacho kuuacha ulimwengu ukiwa mzuri zaidi.
Kama serikali ilikataza matumizi ya mifuko ya plastiki kwa sababu ya athari zake nyingi na za muda mrefu katika mazingira ni sababu gani imeendelea kuruhusu hii mifuko ya plastiki nyepesi kuendelea kutumika baadaye katika baadhi ya biashara? Umefika wakati sasa wa kuharamisha kabisa mifuko yoyote ya plastiki ambayo bado inaendelea kutumika.
Tuyalinde mazingira yetu kwa nguvu zote.Ni wajibu wetu kwa kizazi chetu na kijacho kuuacha ulimwengu ukiwa mzuri zaidi.