KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 537
Ngome ya chadema imeingiwa na vilio na kusaga meno baada ya vijana wengi wenye usongo wa kuibwaga CCM kutoona majina yao kwenye orodha ya majina yaliyobadikwa kwenye jengo la Nkruma pale mlimani. "kwa kweli inasikitisha sana kutoonekana jina langu wakati mwaka 2005 nilipiga kura hapa hapa" Alilalama dada mmoja.
Mwingine aliuliza "iwapo hajaona jina lake achukue hatua zipi ili kuhakikisha kuwa haki yake ya kupiga kura inapatikana" wenine walimshauri aende ofisi za NEC au awapigie simu. Cha kushangaza majina yamebandikwa lakini hakuna maelekezo kwa yule ambae hatakuta jina lake afanye nini.
Kwa kweli dalili za uchakachuaji zimeanza kuonekana mapema kabisa.
Mwingine aliuliza "iwapo hajaona jina lake achukue hatua zipi ili kuhakikisha kuwa haki yake ya kupiga kura inapatikana" wenine walimshauri aende ofisi za NEC au awapigie simu. Cha kushangaza majina yamebandikwa lakini hakuna maelekezo kwa yule ambae hatakuta jina lake afanye nini.
Kwa kweli dalili za uchakachuaji zimeanza kuonekana mapema kabisa.