Vilio kwa Tanesco vinazidi kuwa vingi kwakuwa tunakaa kimya, sasa umefika muda wa kuwafichua

Mimi pia ni mhanga wa TANESCO nilifungiwa mita tatu baada ya mudawakaniambia mita moja haiwezi kununua umeme, kwa bahati nzuri namba za mita nilizofungiwa nilikuwa nazo kuangalia ile iliyoko sio ile yangu, kuuliza mpangaji akasema kuna siku TANESCO walikuja kuangalia shoti baada ya hapo miezi miwili baadae mita hainunui umeme. Nikaenda pale Gongo la mboto wananiambia ninunue mita mpya , ikabidi niende makao makuu kutafuta suluhisho, kule ikachukua takriban wiki kupata ufumbuzi na nikafungiwa mita nyingine. Kummbuka mizunguko yote hiyo ilichukua miezi miwili na nusu, kufuatilia zaidi nikaambiwa wakiona kuna mita ina deni kubwa, wanang'oa na kuchukua wanakubadilishia mita ya nyumba nyingine. Kuweni makini mnaporipoti shoti kwani ile mita yangu ilifungwa nyumba ya mtaa wa jirani na akawa ananunua umeme kwa jina langu. Kisa cha pili kwenye nyumba nyingine kule Ubungo ni kuwa nililipia Survey (kumbe hailipiwi) na bado wakaniambia nitume pesa ya taxi ili muweka mita aje, nikagoma kufuatilia wakageuza mada, nyumba haikidhi kufungiwa mita, ila report ya surveyor wao iliidhinisha kufungiwa mita. TANESCO wote wanastahili kupelekwa mikoani, hata mabosi wao hawana msaada kabisa na wanawaogopa wa chini yao.
Hii sio sahihi kama ni kweli tupatie namba yako ya mita, namba ya simu na eneo tufatilie kwa kuwa bila taarifa kamili uma hauwezi kujua ukweli wa upande wa pili
 
Mimi pia ni mhanga wa TANESCO nilifungiwa mita tatu baada ya mudawakaniambia mita moja haiwezi kununua umeme, kwa bahati nzuri namba za mita nilizofungiwa nilikuwa nazo kuangalia ile iliyoko sio ile yangu, kuuliza mpangaji akasema kuna siku TANESCO walikuja kuangalia shoti baada ya hapo miezi miwili baadae mita hainunui umeme. Nikaenda pale Gongo la mboto wananiambia ninunue mita mpya , ikabidi niende makao makuu kutafuta suluhisho, kule ikachukua takriban wiki kupata ufumbuzi na nikafungiwa mita nyingine. Kummbuka mizunguko yote hiyo ilichukua miezi miwili na nusu, kufuatilia zaidi nikaambiwa wakiona kuna mita ina deni kubwa, wanang'oa na kuchukua wanakubadilishia mita ya nyumba nyingine. Kuweni makini mnaporipoti shoti kwani ile mita yangu ilifungwa nyumba ya mtaa wa jirani na akawa ananunua umeme kwa jina langu. Kisa cha pili kwenye nyumba nyingine kule Ubungo ni kuwa nililipia Survey (kumbe hailipiwi) na bado wakaniambia nitume pesa ya taxi ili muweka mita aje, nikagoma kufuatilia wakageuza mada, nyumba haikidhi kufungiwa mita, ila report ya surveyor wao iliidhinisha kufungiwa mita. TANESCO wote wanastahili kupelekwa mikoani, hata mabosi wao hawana msaada kabisa na wanawaogopa wa chini yao.
Yaani uko sahihi kabisa..ndio mambo yao hayo...
 
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
Huu upumbavu wa kutuomba namba za simu hausaidii hata kidogo.

Yani Wafanyakazi wenu wanasababisha tatizo tukiwasiliana na Nyie mnaomba namba !


Kwanini Msiandae madawati ya kusikiliza Usumbufu wa Wateja wenu kila wilaya. Na ikionekana ni uzembe wa makusudi wa wafanyakazi wenu Kwanini msiwafukuze
 
Huu upumbavu wa kutuomba namba za simu hausaidii hata kidogo.

Yani Wafanyakazi wenu wanasababisha tatizo tukiwasiliana na Nyie mnaomba namba !


Kwanini Msiandae madawati ya kusikiliza Usumbufu wa Wateja wenu kila wilaya. Na ikionekana ni uzembe wa makusudi wa wafanyakazi wenu Kwanini msiwafukuze
Unapolalamika unawajibika kutoa taarifa kamili ili tukuhudumie.Tunasikitika sana kwa kuwa wengi mnalalamika tukiwapigia simu hakuwahi hata kutoa taarifa.Njoo PM tukuhudumia sisi Huduma kwa wateja tumejipanga kukufata ulipo na kukuhusumia.

Toa taarifa kamili, pata huduma sahihi
 
Watu wenye madeni ya zamani magufuli aliwasamehe na kusema yafutwe waanze upya ameondoka mumeyarudisha tena madeni.
Unapolalamika unawajibika kutoa taarifa kamili ili tukuhudumie.Tunasikitika sana kwa kuwa wengi mnalalamika tukiwapigia simu hakuwahi hata kutoa taarifa.Njoo PM tukuhudumia sisi Huduma kwa wateja tumejipanga kukufata ulipo na kukuhusumia.

Toa taarifa kamili, pata huduma sahihi
 
Watu wenye madeni ya zamani magufuli aliwasamehe na kusema yafutwe waanze upya ameondoka mumeyarudisha tena madeni.
Huu ni upotoshaji wa wazi hakuna kitu kama hicho ulichodai tafadhali kuwa na uungwana kwa kusema ukweli
 
Nimeona kuna dada kaenda ofisini zenu pale zakihem ameambiwa kuwa hawezi kununua umeme wa elfu 20 kisa kuna madeni ya zamani madeni mabayo yalishafutwa akaambiwa aende ofisi za kurasini (mbagala)
Huu ni upotoshaji wa wazi hakuna kitu kama hicho ulichodai tafadhali kuwa na uungwana kwa kusema ukweli
 
Nimeona kuna dada kaenda ofisini zenu pale zakihem ameambiwa kuwa hawezi kununua umeme wa elfu 20 kisa kuna madeni ya zamani madeni mabayo yalishafutwa akaambiwa aende ofisi za kurasini (mbagala)
Tafadhali onyesha namba ya mita tukujibu kwa taafifa kamili, hakuna mteja anayewekewe deni kwenye mita lisilo na sababu
 
Tunashukuru kwa taarifa, kwa aina ya swala lako unashauriwa kufika ofisini au kutoa taarifa kamili zitakazotusaidia kukupatia ufafanuzi kama jina, eneo, wilaya, namba ya mita , namba ya simu na tatizo.

Aidha huu utaratibu upo tunapokuta mita ambayo haikufata utaratibu wa kutoka TANESCO kwenda kwa mteja mteja anawajibika kutupatia taarifa zitazosaidia uchunguzi wa uhalali wake.
Tunashukuru kwa taarifa, kwa aina ya swala lako unashauriwa kufika ofisini au kutoa taarifa kamili zitakazotusaidia kukupatia ufafanuzi kama jina, eneo, wilaya, namba ya mita , namba ya simu na tatizo.

Aidha huu utaratibu upo tunapokuta mita ambayo haikufata utaratibu wa kutoka TANESCO kwenda kwa mteja mteja anawajibika kutupatia taarifa zitazosaidia uchunguzi wa uhalali wake.
Vishoka wenu anatuuzia mita mtakuja mnatuwekea madeni ya mil 15

Michezo yenu ni ya kuumiza wananchi
 
Vishoka wenu anatuuzia mita mtakuja mnatuwekea madeni ya mil 15

Michezo yenu ni ya kuumiza wananchi
Kwanini ununue mita? Mita haizwi mteja anapaswa kulipia kwa kufata taratibu na sisi tutamfungia mita.Tafadhali toa ushirikiano nasisi tutaweka taarifa kamili hapa ili kuonyesha ukweli wa malalamiko haya.
 
" ukipata nafasi ya kumuona waziri wa nishati utamuambia nini??
Mimi: Nitampiga kofi kama njia ya kuamsha ubongo wake
Makamba hafai kabisa kuwa waziri. Wizara hii inahitaji mtu wa aina ya Lukuvi, Aweso na yule wa madini. Mama watu wameanza kumchukia sababu ya watu kama Makamba. He is not aggressive and committed enough.
 
Kufika ofisini ni wazo jema lakini wengi tunaishi mbali na ofisi zenu.
Nawashauri muweke ofisi ndogo kila kata.

Hata hivyo ingefaa kila kijiji muwe na wakala au mwakilishi wenu hata kama hamkumuajiri.

Utaratibu wa sasa ni mgumu.
Mko mbali na wateja wenu.
Wakaribieni.

Igeni mifano ya benki.
 
Nina mita mbili kwenye nyumba mbili tofauti.
Yaani kila nyumba ina mita yake.
Ni zaidi ya mwaka mmoja na nusu tangu nimeziweka.

Sijawahi kuzidi uniti 40 kwa mwezi kwa kila mita.

Nahitaji ziingie kwenye tarrif 4.

Nilikwenda ofisi ya Tanesco ya wilaya [ zaidi ya km.30 kutoka hapa].
Niliambiwa nilipe sh.25,000/= kwa kila mita.
Yaani sh.50,000/= kwa mita mbili.

Sikulipa kwa kuwa sina uwezo huo.

Je huu ndio utaratibu?
 
Back
Top Bottom