Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,398
Russia inashambuliwa kiuchumi kila kona kwa nguvu zote na matajiri wakubwa wajulikanao kama "Oligarchs" wanazuiwa mali zao katika mabenki mbalimbali duniani.
Hiyo ni kufuatia nchi mbalimbali duniani zikiongozwa na Marekani na Uingereza kuamua kuiweka vikwazo vya kiuchumi Russia baada ya nchi huyo moja ya mataifa makubwa duniani kuivamia nchi jirani ya Ukraine Alhamisi ilopita.
Pia baadhi ya mali kama meli au "Yacht" zinakamatwa zingine zikiwa zimepaki kwa ajili ya matengenezo na meli za mizigo kukamatwa na serikali ya Ufaransa katika kutekeleza masharti ya vikwazo hivyo.
Russia inadai yataka kuhakikisha Ukraine haina zilaha kali za maangamizi, haina nguvu yoyote ya kijeshi na pia haina watu wenye misimamo ya kinazi na kifashisti.
Lakini huku vikwazo hivyo vikizidi kuimarishwa kuna somo ambalo viongozi wengi duniani ambao wamezoea kuiba mali katika nchi zao na kuzificha katika nchi za Ulaya khasa Ulaya Magharibi, kwa sasa wamekuwa na tumbo joto.
Hali hiyo ni kutokana na nchi za Ulaya magharibi kuamua kuangalia fedha zinazomilikiwa na watu mbalimbali ambao wana mahusiano na uongozi wa Kremlin.
Lakini zoezi hilo la kutaka kuzuia fedha kwenye mabenki au mali (kama nyumba) haliwezi kutekelezwa leo wala kesho, bali laweza kuchukua miezi kadhaa na hata mwaka au zaidi kutokana na mapingamizi ya kisheria kutoka kwa wenye mali hizo.
Tayari wanasheria nguli wa masuala ya fedha na usalama wa mali kwa matajiri wamekuwa wakisubiria kuzuia hatua zozote zisizo na haki kisheria kuzuia mali hizo kwa kusisitiza uwepo wa sababu za kisheria kwa serikali kufanya hivyo.
Switzerland ikiwa ni moja ya nchi hizo zilizotangaza kuzuia mali (freezing assets) imewalenga baadhi ya hao mabilionea wa Russia, marafiki zao na familia zao.
Kwa mujibu wa SNB yaani benki kuu ya Uswiss,mwaka 2020 mabilionea hao wa Russia walikuwa wana kiasi cha faranga za Uswiss bilioni 10.4 au dola bilioni 11.24 katika mabenki ya Switzerland.
Viongozi wengi duniani ambao hujilimbikizia mali na kisha kuwekeza katika nchi za ughaibuni kwa sasa (inasemwa kuwa) wanapanga mipango mipya juu ya kukabiliana na matatizo kama haya.
Hiyo ni kwasababu haujulikani sheria zinazorekebishwa sasa zitaelekeza hatua za kuzuia fedha hizo kwa watu wote au wale matajiri wa Russia pekee au akina nani.
Sani Abacha aliekuwa raisi wa Nigeria alipofariki aliacha kiasi cha dola milioni 267 katika kisiwa cha Jersey, dola milioni 480 katika mabenki ya Marekani na fedha zote hizo hazikurudi Nigeria bali kugawiwa katika ya serikali za nchi hizo za mamlaka za nchi hizo yaani Marekani, Jersey na Nigeria ambayo inajulikana fedha hizo zingeishia wapi.
Mwaka 2000 Switzerland baada ya kujivuta sana kutoa kiasi halisi cha fedha ambazo Abacha aliziweka katika mabenki ya nchi hiyo walikuja kusema kulikuwa na kiasi cha dola milioni 300 tu! na ambazo pia zilihamishwa kwenda katika mabenki nchini Uingereza ambayo nayo ilichukua muda mrefu (miezi 4) kujibu barua ya maulizo kutoka kwenye serikali ya Nigeria.
Lakini baadae mwaka 2015 Uswiss walikuja kurudisha rasmi fedha kiasi cha dola milioni 380 kwa serikali ya Nigeria baada ya kuzikomboa fedha hizo kutoka katika benki moja nchini Luxembourg, baada ya kuzikusanya tangu mwaka 2006. Hiyo ilikuwa baada ya Serikali ya Nigeria kukubaliana na familia ya Abacha na kufuta mashitaka dhidi ya mtoto wake aitwae Abba Abacha.
Fedha hizo (dola milioni 380) ni mbali ya kiasi cha dola milioni 700 ambazo Switzerland ilizirudisha kwa serikali ya Nigeria, fedha ambazo Sani Abacha aliekuwa kiongozi wa kijeshi alizificha katika mabenki mbalimbali jijini Geneva.
Switzerland ilibadili sheria ya usiri wa kanuni za kibenki au "Banking Secrecy Rules" ambapo kunapokuwepo uchunguzi wa uhalifu wa kibenki au wizi wa kalamu, mabenki hupaswa kutoa taarifa za washukiwa walo na akaunti katika mabenki hayo, ilimradi mwanasheria raia wa Uswiss ndie aombe taarifa hizo kwa kuweka ombi maalum la kisheria.
Serikali za Marekani na Uingereza nazo zimekuwa na wakati mgumu wa kuchambua sheria za mabenki ili kuzuia vitendo vya utakatishaji fedha na kuweka vikwazo kwa baadhi ya matajiri wakubwa wenye mahusiano na serikali ya Russia au raisi Putin kwa kuzuia fedha zao.
Lakini nchi nyingi zinaishangaa Uingereza kwa kusuasua katika kutekeleza vikwazo kwa kuwawekea vikwazo matajiri wakubwa waishio nchini humo.
Hadi sasa ni ni matajiri wakubwa sita tu ndo walokumbwa na dhahama hizo za vikwazo akiwemo bwana Alisher Usmanov ambae meli yake ya kupumzikia iitwayo Dilbar yenye thamani ya dola milioni 600 imekamatwa na serikali ya Ufaransa ikishirikina na serikali ya Ujerumani.
Lakini hapohapo chama cha wahafidhina kimekuwa na wakti mgumu kujitetea kuhusiana na mchango wa pauni milioni 2 ambazo zimetolewa na mwanamama raia wa Russia aitwae Lubov Chernukin tangu mwaka 2012.
Isitoshe bilionea Roman Abramovich amepewa mwanya wa kuiuza timu ya mpira ya Chelsea ili kuokoa fedha zake pauni milioni 2 ambazo anaidai Chelsea na tiyari amepata wateja ambao wameweka mezani pauni bilioni 3 kutaka kuinunua timu hiyo.
Hivyo, suala hili la vikwazo vya kiuchumi wanowekewa baadhi ya watu binafsi na makampuni yao kadha wa kadha yaonyesha kuwa ni dalili ya mambo mengine kuibuliwa kuhusiana na sheria mbalimbali za uwekaji fedha katika mabenki, uhamishaji (bank transfer) na udhibiti wa utakatishaji fedha.
London ni moja ya miji ambayo inatuhumiwa kuwa ni kitovu cha utakatishaji fedha zinodaiwa kuibwa kutoka Russia na nchini zingine mbalimbali duniani ambapo fedha hizo hutumika katika manunuzi ya majumba (mansions) na vipande vya ardhi, pamoja na uendeshaji wa biashara zingine mbalimbali kubwa na ndogo.
Serikali za nchi za magharibi kwa kuweka vikwazo kwa washirika wa raisi Putin na kuangalia upya sheria mbalimbali zinohusiana na masuala ya fedha kunaweza pia kutumika kama mwanya wa kuhakikisha fedha zinoingizwa barani Ulaya na Marekani zinaangaliwa kwa jicho la tatu.
Hali hiyo bila shaka itapelekea watu wengi wenye akaunti mbalimbali katika sehemu mbalimbali duniani kuanza kuingizwa na wasiwasi na kupanga namna ya kurekebisha mabenki hayo.
Hiyo ni kufuatia nchi mbalimbali duniani zikiongozwa na Marekani na Uingereza kuamua kuiweka vikwazo vya kiuchumi Russia baada ya nchi huyo moja ya mataifa makubwa duniani kuivamia nchi jirani ya Ukraine Alhamisi ilopita.
Pia baadhi ya mali kama meli au "Yacht" zinakamatwa zingine zikiwa zimepaki kwa ajili ya matengenezo na meli za mizigo kukamatwa na serikali ya Ufaransa katika kutekeleza masharti ya vikwazo hivyo.
Russia inadai yataka kuhakikisha Ukraine haina zilaha kali za maangamizi, haina nguvu yoyote ya kijeshi na pia haina watu wenye misimamo ya kinazi na kifashisti.
Lakini huku vikwazo hivyo vikizidi kuimarishwa kuna somo ambalo viongozi wengi duniani ambao wamezoea kuiba mali katika nchi zao na kuzificha katika nchi za Ulaya khasa Ulaya Magharibi, kwa sasa wamekuwa na tumbo joto.
Hali hiyo ni kutokana na nchi za Ulaya magharibi kuamua kuangalia fedha zinazomilikiwa na watu mbalimbali ambao wana mahusiano na uongozi wa Kremlin.
Lakini zoezi hilo la kutaka kuzuia fedha kwenye mabenki au mali (kama nyumba) haliwezi kutekelezwa leo wala kesho, bali laweza kuchukua miezi kadhaa na hata mwaka au zaidi kutokana na mapingamizi ya kisheria kutoka kwa wenye mali hizo.
Tayari wanasheria nguli wa masuala ya fedha na usalama wa mali kwa matajiri wamekuwa wakisubiria kuzuia hatua zozote zisizo na haki kisheria kuzuia mali hizo kwa kusisitiza uwepo wa sababu za kisheria kwa serikali kufanya hivyo.
Switzerland ikiwa ni moja ya nchi hizo zilizotangaza kuzuia mali (freezing assets) imewalenga baadhi ya hao mabilionea wa Russia, marafiki zao na familia zao.
Kwa mujibu wa SNB yaani benki kuu ya Uswiss,mwaka 2020 mabilionea hao wa Russia walikuwa wana kiasi cha faranga za Uswiss bilioni 10.4 au dola bilioni 11.24 katika mabenki ya Switzerland.
Viongozi wengi duniani ambao hujilimbikizia mali na kisha kuwekeza katika nchi za ughaibuni kwa sasa (inasemwa kuwa) wanapanga mipango mipya juu ya kukabiliana na matatizo kama haya.
Hiyo ni kwasababu haujulikani sheria zinazorekebishwa sasa zitaelekeza hatua za kuzuia fedha hizo kwa watu wote au wale matajiri wa Russia pekee au akina nani.
Sani Abacha aliekuwa raisi wa Nigeria alipofariki aliacha kiasi cha dola milioni 267 katika kisiwa cha Jersey, dola milioni 480 katika mabenki ya Marekani na fedha zote hizo hazikurudi Nigeria bali kugawiwa katika ya serikali za nchi hizo za mamlaka za nchi hizo yaani Marekani, Jersey na Nigeria ambayo inajulikana fedha hizo zingeishia wapi.
Mwaka 2000 Switzerland baada ya kujivuta sana kutoa kiasi halisi cha fedha ambazo Abacha aliziweka katika mabenki ya nchi hiyo walikuja kusema kulikuwa na kiasi cha dola milioni 300 tu! na ambazo pia zilihamishwa kwenda katika mabenki nchini Uingereza ambayo nayo ilichukua muda mrefu (miezi 4) kujibu barua ya maulizo kutoka kwenye serikali ya Nigeria.
Lakini baadae mwaka 2015 Uswiss walikuja kurudisha rasmi fedha kiasi cha dola milioni 380 kwa serikali ya Nigeria baada ya kuzikomboa fedha hizo kutoka katika benki moja nchini Luxembourg, baada ya kuzikusanya tangu mwaka 2006. Hiyo ilikuwa baada ya Serikali ya Nigeria kukubaliana na familia ya Abacha na kufuta mashitaka dhidi ya mtoto wake aitwae Abba Abacha.
Fedha hizo (dola milioni 380) ni mbali ya kiasi cha dola milioni 700 ambazo Switzerland ilizirudisha kwa serikali ya Nigeria, fedha ambazo Sani Abacha aliekuwa kiongozi wa kijeshi alizificha katika mabenki mbalimbali jijini Geneva.
Switzerland ilibadili sheria ya usiri wa kanuni za kibenki au "Banking Secrecy Rules" ambapo kunapokuwepo uchunguzi wa uhalifu wa kibenki au wizi wa kalamu, mabenki hupaswa kutoa taarifa za washukiwa walo na akaunti katika mabenki hayo, ilimradi mwanasheria raia wa Uswiss ndie aombe taarifa hizo kwa kuweka ombi maalum la kisheria.
Serikali za Marekani na Uingereza nazo zimekuwa na wakati mgumu wa kuchambua sheria za mabenki ili kuzuia vitendo vya utakatishaji fedha na kuweka vikwazo kwa baadhi ya matajiri wakubwa wenye mahusiano na serikali ya Russia au raisi Putin kwa kuzuia fedha zao.
Lakini nchi nyingi zinaishangaa Uingereza kwa kusuasua katika kutekeleza vikwazo kwa kuwawekea vikwazo matajiri wakubwa waishio nchini humo.
Hadi sasa ni ni matajiri wakubwa sita tu ndo walokumbwa na dhahama hizo za vikwazo akiwemo bwana Alisher Usmanov ambae meli yake ya kupumzikia iitwayo Dilbar yenye thamani ya dola milioni 600 imekamatwa na serikali ya Ufaransa ikishirikina na serikali ya Ujerumani.
Lakini hapohapo chama cha wahafidhina kimekuwa na wakti mgumu kujitetea kuhusiana na mchango wa pauni milioni 2 ambazo zimetolewa na mwanamama raia wa Russia aitwae Lubov Chernukin tangu mwaka 2012.
Isitoshe bilionea Roman Abramovich amepewa mwanya wa kuiuza timu ya mpira ya Chelsea ili kuokoa fedha zake pauni milioni 2 ambazo anaidai Chelsea na tiyari amepata wateja ambao wameweka mezani pauni bilioni 3 kutaka kuinunua timu hiyo.
Hivyo, suala hili la vikwazo vya kiuchumi wanowekewa baadhi ya watu binafsi na makampuni yao kadha wa kadha yaonyesha kuwa ni dalili ya mambo mengine kuibuliwa kuhusiana na sheria mbalimbali za uwekaji fedha katika mabenki, uhamishaji (bank transfer) na udhibiti wa utakatishaji fedha.
London ni moja ya miji ambayo inatuhumiwa kuwa ni kitovu cha utakatishaji fedha zinodaiwa kuibwa kutoka Russia na nchini zingine mbalimbali duniani ambapo fedha hizo hutumika katika manunuzi ya majumba (mansions) na vipande vya ardhi, pamoja na uendeshaji wa biashara zingine mbalimbali kubwa na ndogo.
Serikali za nchi za magharibi kwa kuweka vikwazo kwa washirika wa raisi Putin na kuangalia upya sheria mbalimbali zinohusiana na masuala ya fedha kunaweza pia kutumika kama mwanya wa kuhakikisha fedha zinoingizwa barani Ulaya na Marekani zinaangaliwa kwa jicho la tatu.
Hali hiyo bila shaka itapelekea watu wengi wenye akaunti mbalimbali katika sehemu mbalimbali duniani kuanza kuingizwa na wasiwasi na kupanga namna ya kurekebisha mabenki hayo.