Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
Kwa muda mrefu tumeilalamikia katiba yetu kwamba inabana demokrasia. Hata hivyo ni mara chache mno tumeweza kutaja vipengele ambavyo ni tatizo. Leo nimeamua kwa kuanzia kutajia ibara angalu mbili ambazo mimi ninaona ni sumu kwa demokrasia ya vyama vingi na vinafaa kubadilishwa.
1)Ibara ya 1 iayozungumzia misingi ya katiba. Nafikiri hakuna haja ya kutaja ujamaa kama sehemu ya misingi. mambo ya itikadi wangeachiwa vyama vya siasa kama nyenzo yao ya kuomba ridhaa. Mambo ya itikadi hayawezi kuwa mambo ya kitaifa na hivyo hakuna haja kuyatamka kwenye katiba.
2) Katika ibara ya 39 (1) kinachozungumzia sifa za kuchaguliwa kuwa Rais, nafikiri kuna haja ya kupunguza umri wa kukubalika kuwa Rais kutoka miaka 40 ya sasa hadi angalau 35. Inawezekana mwaka 1977 ilieleweka kuweka huo umri, lakini sasa umefika wakati tukakibadilisha hiki kipengele
3) Ibara ya 40(6) pamoja na mambo mengine inakataza mtu yeyote kwenda mahakamani kuhoji matokeo ya kura za urais mara Tume ya Uchaguzi ikishakutangaza matokeo husika. Hiki nafikiri ni kipengele kibovu na hatari mno kwa demokrasia na kinatoa mwanya watu kuiba kura za urais bila woga wala kificho. Ibara hii inahitaji mabadiliko ya haraka. Actually ni sisi peke yetu katika Jumuiya ya Madola wenye kipengele hiki.
Kwa leo naishia hapa. Nakaribisha maoni zadi.
1)Ibara ya 1 iayozungumzia misingi ya katiba. Nafikiri hakuna haja ya kutaja ujamaa kama sehemu ya misingi. mambo ya itikadi wangeachiwa vyama vya siasa kama nyenzo yao ya kuomba ridhaa. Mambo ya itikadi hayawezi kuwa mambo ya kitaifa na hivyo hakuna haja kuyatamka kwenye katiba.
2) Katika ibara ya 39 (1) kinachozungumzia sifa za kuchaguliwa kuwa Rais, nafikiri kuna haja ya kupunguza umri wa kukubalika kuwa Rais kutoka miaka 40 ya sasa hadi angalau 35. Inawezekana mwaka 1977 ilieleweka kuweka huo umri, lakini sasa umefika wakati tukakibadilisha hiki kipengele
3) Ibara ya 40(6) pamoja na mambo mengine inakataza mtu yeyote kwenda mahakamani kuhoji matokeo ya kura za urais mara Tume ya Uchaguzi ikishakutangaza matokeo husika. Hiki nafikiri ni kipengele kibovu na hatari mno kwa demokrasia na kinatoa mwanya watu kuiba kura za urais bila woga wala kificho. Ibara hii inahitaji mabadiliko ya haraka. Actually ni sisi peke yetu katika Jumuiya ya Madola wenye kipengele hiki.
Kwa leo naishia hapa. Nakaribisha maoni zadi.