Vikwazo vipya vya USA kwa Huawei vinazuia hata kampuni choka mbaya kama Mediatek kufanya biashara na Huawei

The Evil Genius

JF-Expert Member
Mar 21, 2014
5,451
17,155
Marekani imetangaza vikwazo vipya kwa kampuni ya Huawei zaidi ya vile ilivyotangaza mwezi MAy mwaka huu ambavyo vilizuia makampuni makubwa ya kutengeneza chipsets kama Samsung na TSMC kuiuzia Huawei.

Jana Jumatatu Marekani imetangaza vikwazo vipya kwa Huawei ambavyo vinazuia kampuni hata za chipsets za viwango hafifu kama Mediatek kuiuzia chipsets Huawei bila kibali cha Marekani.

Marekani imesema vikwazo hivi vinaenda mbali zaidi ya vile vya mwezi May ili kuhakikisha Huawei hapati vifaa vya kutengenezea simu zake wala mitambo yake ya mawasiliano ya 5G.

Huawei imetangaza kua simu ya Mate 40 ndio itakua simu ya mwisho yenye processor za hali ya juu kwa sababu haitapata tena material kwa sababu ya vikwazo vya Marekani.

Huawei ilikua inategemea kuendelea na simu za daraja la kati na la chini, entry level and med range phones ambazo ingepata vifaa kutoka Mediatek ili kutengeneza chipsets lakini Marekani amepiga pini hadi huko.

Mediatek ndio processor ambazo zinatumika kwenye simu za infinix, tecno na baadhi ya low end na mid range phones za makampuni mengine kama A10s ya Samsung.

New sanctions deal 'lethal blow' to Huawei. China decries US bullying
 
Jana Jumatatu Marekani imetangaza vikwazo vipya kwa Huawei ambavyo vinazuia kampuni hata za chipsets za viwango hafifu kama Mediatek kuiuzia chipsets Huawei bila kibali cha Marekan
nieleweshe, why kibali toka USA? Kwani chips ni mali ya USA? nieleweshe please
 
Huyu marekani anaumwa degedege hapo anatafuta wa kufa nae naona kapata halafu kila siku yanahubiri demokrasia Sasa hiyo ndo demokrasia..? Uhuru wa makampuni ndo huo?

Huyu aseme ukweli China imemshika pabaya tena huyu korona huyu..😅
 
nieleweshe, why kibali toka USA? Kwani chips ni mali ya USA? nieleweshe please
Unajua hapa Duniani hakuna kitu kipya, sayansi unayoiona leo tunayoona imeendelea sana imejengwa kwenye msingi wa wanasayansi wa zamani. Mfano leo hata utengeneze ndege ama meli inayokimbia namna gani lazima utatumia kanuni zile zile za Archimedes ama za Newton za laws of motion.

Hivyo basi sehemu kubwa ya teknolojia hiyo imekua patented Marekani, teknolojia kubwa ya vifaa vingi imekua patented Marekani, ndio maana hutaweza kutengeneza kitu chako kikawa na 0% ya American technology, sio rahisi.

Ndio maana ili utengeneze vitu vyako vingi utahitaji kutumia teknolojia ya Mmarekani, upende usipende hivyo akikuwekea vikwazo utapata wapi hiyo teknolojia? Ndio maana Huawei hana namna hapa.

Marekani anasema angekuwepo miaka 8 iliyopita China isingekua hapa ilipo.

Kwa sasa ametangaza kufungia Tik Tok, We chat na ametishia kuidhibiti Alibaba kufanya shughuli zake MMarekakani.
 
Back
Top Bottom