Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,658
- 22,254
Ni aibu watanzania kudai nchi za ulaya ziondowe vikwazo kwa Zimbabwe wakati sisi wenyewe tunaviwekea vikwazo vyama vya upinzani nchini kama walivyokuwa wakifanya makaburu Afrika Kusini, Jana tulishuhudia wanaccm wakiipokea ndege yao! Ambayo imenunuliwa kwa pesa za watanzania wote, hii ni sawa na kilichofanyika kwenye Shamba la Wanyama kama alivyotafsiri Mwalimu Nyerere.
Walishangilia kumtoa mkulima mnyonyaji bila kujua kuwa kati yao watakao wapa madaraka ya kuwaongoza watakuja kuwa wabaya zaidi ya yule waliyemuondoa! Waliojibinafsishia ndege iliyonunuliwa kwa pesa zetu walkusanyika na kuanza kuwarushia madongo waliochanga pesa japo hawawataki kwenye kula keki! Hivi Mungu wa watanzania ni mmoja au kuna miungu wengine wa wapinzani?
Na pesa zinazokusanywa na TRA huchambuliwa na kuziondoa za wapinzani kisha hutupwa? Inakuwaje unampenda baniani lakini haukipendi kiatu chake? Kwa hili labda wahenga walikosea. Mnapokula keki ya wote huku mmejifungia hamuoni aibu mnapoona macho ya mliowawekea vikwazo wakiwachungulia madirishani?
Vikwazo kwa Zimbabwe na kwa wapinzani Tanzania viondolewe.
Walishangilia kumtoa mkulima mnyonyaji bila kujua kuwa kati yao watakao wapa madaraka ya kuwaongoza watakuja kuwa wabaya zaidi ya yule waliyemuondoa! Waliojibinafsishia ndege iliyonunuliwa kwa pesa zetu walkusanyika na kuanza kuwarushia madongo waliochanga pesa japo hawawataki kwenye kula keki! Hivi Mungu wa watanzania ni mmoja au kuna miungu wengine wa wapinzani?
Na pesa zinazokusanywa na TRA huchambuliwa na kuziondoa za wapinzani kisha hutupwa? Inakuwaje unampenda baniani lakini haukipendi kiatu chake? Kwa hili labda wahenga walikosea. Mnapokula keki ya wote huku mmejifungia hamuoni aibu mnapoona macho ya mliowawekea vikwazo wakiwachungulia madirishani?
Vikwazo kwa Zimbabwe na kwa wapinzani Tanzania viondolewe.