Rah_sputin
Member
- Nov 3, 2009
- 83
- 10
Ninaye shemeji ambaye anatutia aibu sana sisi kwenye ukoo wetu.
Yeye hujifanya mtu wa heshima nyingi,ana cheo kikubwa, mali na kila kitu.ana mke na watoto na kila ambacho mtu angetamani akipate. Tatizo lake ni moja - kutaka kila sketi aionayo.tukianza na nyumbani kwake...
Hakuna mfanyakazi wa kike anaacha kumtaka kimapenzi. Kazini kwake kamaliza wanawake wote. Kibaya sasa anaanza kunyemelea ndugu zake wa damu!
Amekuwa akimlea binti mmoja yatima ambaye ni mwana wa shangazie - yaani binamu take. Amemsomesha hadi akamaliza. Sasa anamdai ujira wa mapenzi. Je huyu binti afanyeje? Amemkatalia lakini jamaa kakomaa tu. Binti kahama hadi nyumbani. Binti ni mcha mungu sana na hataki katakata kujiingiza kwenye uchafu huu wa binamu ambaye kwanza kamlea kama baba maana analingana na watoto wa huyu shemeji.
Mshaurini huyu yatima.
Yeye hujifanya mtu wa heshima nyingi,ana cheo kikubwa, mali na kila kitu.ana mke na watoto na kila ambacho mtu angetamani akipate. Tatizo lake ni moja - kutaka kila sketi aionayo.tukianza na nyumbani kwake...
Hakuna mfanyakazi wa kike anaacha kumtaka kimapenzi. Kazini kwake kamaliza wanawake wote. Kibaya sasa anaanza kunyemelea ndugu zake wa damu!
Amekuwa akimlea binti mmoja yatima ambaye ni mwana wa shangazie - yaani binamu take. Amemsomesha hadi akamaliza. Sasa anamdai ujira wa mapenzi. Je huyu binti afanyeje? Amemkatalia lakini jamaa kakomaa tu. Binti kahama hadi nyumbani. Binti ni mcha mungu sana na hataki katakata kujiingiza kwenye uchafu huu wa binamu ambaye kwanza kamlea kama baba maana analingana na watoto wa huyu shemeji.
Mshaurini huyu yatima.