ThaGreatman
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 708
- 1,465
Jana nimeamka asubuhi nikatafakari kwa kina sana juu ya maisha haya. Kubwa zaidi ni namna aliyewahi kuwa mpnz wangu aliponishambulia sana kuwa nimempa pesa kidogo,(aliniomba 150,000/= lakini mimi nilimpatia 100,000/=) kwa sababu nilikuwa najua kabisa kuwa ana pesa yake nyingine nyingi tu,kwa hiyo nikafanya jaribio la makusudi kuona reaction yake ingekuwaje baada ya kumpa kiasi pungufu na alichokiomba!
Lahaulaaa,lawama nilizopokea sasa....,"haujali shida zangu, najua unanikomoa, sawa,ila kumbuka mimi ni mke wako mtarajiwa,kama leo hii unashindwa kunisaidia 150k,sijui huko baadaye itakuwaje"
Nilipomaliza kusoma meseji nilivuta pumzi nikazifuta zote,nikajisemea moyoni,kuwa huyu hanifai kabisa....(na ndiyo ukawa mwisho wa mimi na yeye,japo mpaka sasa sijamwambia chochote)
Kilichofanya nije hapa ni baada ya kuamua kumtumia mama yangu mzazi kiasi cha sh.ELFU HAMSINI TU YA MATUMIZI,maombi niliyopokea hakika niliumia sana moyoni,sanaaa,kwamba mpenzi wangu nilimtumia sh.LAKI MOJA akaishia kunilaumu na kunisema sana,lakini mama yangu nimemtumia sh.50k shukrani alizotoa ni nzito sana! Hii imeniongezea hasira juu ya wanawake wasioridhika na kingi tunachowapatia,ilhali wazazi wetu wanapata kidogo na bado wanashukuru kweli kweli!
Haya ni maombi ya mama baada ya kutumiwa kiasi kidoogo sana cha pesa
Vijana wenzagu,tuwakumbukeni wazazi wetu wana baraka nyingi sana kwetu
Lahaulaaa,lawama nilizopokea sasa....,"haujali shida zangu, najua unanikomoa, sawa,ila kumbuka mimi ni mke wako mtarajiwa,kama leo hii unashindwa kunisaidia 150k,sijui huko baadaye itakuwaje"
Nilipomaliza kusoma meseji nilivuta pumzi nikazifuta zote,nikajisemea moyoni,kuwa huyu hanifai kabisa....(na ndiyo ukawa mwisho wa mimi na yeye,japo mpaka sasa sijamwambia chochote)
Kilichofanya nije hapa ni baada ya kuamua kumtumia mama yangu mzazi kiasi cha sh.ELFU HAMSINI TU YA MATUMIZI,maombi niliyopokea hakika niliumia sana moyoni,sanaaa,kwamba mpenzi wangu nilimtumia sh.LAKI MOJA akaishia kunilaumu na kunisema sana,lakini mama yangu nimemtumia sh.50k shukrani alizotoa ni nzito sana! Hii imeniongezea hasira juu ya wanawake wasioridhika na kingi tunachowapatia,ilhali wazazi wetu wanapata kidogo na bado wanashukuru kweli kweli!
Haya ni maombi ya mama baada ya kutumiwa kiasi kidoogo sana cha pesa
Vijana wenzagu,tuwakumbukeni wazazi wetu wana baraka nyingi sana kwetu