Vijana wanaoshambulia madereva kwenye foleni

Darling

Member
Jul 30, 2007
69
1
Jamani kama hamna habari habari ndio hiii; kuweni makini.

Good afternoon

Lets share this with you

Napenda kuwatahadharisha kuwa muwe makini zaidi mkiwa barabarani hasa kwenye foleni. Kuna kundi la vijana zaidi ya 30 wanavamia magari wakiwa na mapanga, nondo na visu kwa lengo la kupora chochote ulichonacho na halikadhalika wanauwa ama kujeruhi.

Maeneo hatari ni maeneo ya Jangwani- Morogoro Road,Ocean Road Seaview,Salender Bridge, Bonde la Kigogo ukitokea Ilala kuja Magomeni, Daraja la Ubungo karibu na njia panda ya kwenda UDSM na barabara ya Mandela Road ukitokea Tazara kuja Ubungo.
 
Kuna kanuni inasema kuwa yeyote mwenye mali ni mwangalizi wa mali za jamii. Jamii ikiamua inaweza kuzichukua mali zake. Ni kama kitendo kinachoonekana hapa kwa hiki kikundi kinachojiita "Kiboko Msheli". Haya ni matokeo ya ubinafsi na sera mbovu za kujua kuwa unapokula wewe na kusaza wakati mwenzako analala na njaa basi hata wewe pia hautakuwa na furaha ya shibe hiyo.

The late Prof Chachage alikuwa anapigia kelele sana gap kati ya masikini na tajiri na kusema kuwa Tanzania hatuna amani, ila tuna utulivu tu. Kwani amani itapatikana mpaka pale watu watakapo kuwa na milango ya vioo badala ya magrili, watu watakapoona kuwa hakuna haja ya kuvunja kwa mtu kuchukua kitu ambacho hata mimi kama nikitaka ntakipata kihalali.

Haya ni matokeo ya kutowaandaa vijana kukabili maisha yao na kuendelea na utamaduni wa "on your own" kunakofanywa na watunga sera. Kwa kuwa wao wana walinzi kuanzia wanapotembea barabarani na mpaka majumbani mwao basi hawaoni haja ya kutatua tatizo hili la vijana kutokuwa na mwelekeo wa maisha na kuamua kuanzisha himaya zao barabarani kama nchi haina serikali vile ya kuvamia na kupora au hata kuua ikibidi ili mradi nao wapate kile ambacho si halali yao ila kwa kunyimwa nafasi halali ya kukipata.

Serikali na Jeshi la Polisi hawana budi kuimarisha ulinzi kwa walipa kodi wote including wenye magari ambao wamekuwa kwenye matatizo ya kukosa ulinzi japo wanalipa kile kinachostahili. Tusipolitafutia suluhu hili basi tusishangae siku moja hawa vijana watakapokuwa tayari kufa na kuvamia pale magogoni na twin towers kwa malengo ya kuchukua chao ambacho kinaliwa na wachache kwa njia ya maandamano au hata vurugu.

kiboko msheli yaibuka kwenye foleni za magari dar

Napenda kuwatahadharisha wadau wote kuwa muwe makini zaidi mkiwa barabarani hasa kwenye foleni jijini Dar kwani kuna kundi la vijana zaidi ya 30 maarufu kama 'KIBOKO MSHELI' wanaovamia magari wakiwa na mapanga,nondo na visu kwa lengo la kupora chochote ulichonacho na halikadhalika wanauwa ama kujeruhi.

Maeneo hatari ni maeneo ya Jangwani- Morogoro Road,Ocean Road, Seaview, Salender Bridge, Bonde la Kigogo ukitokea Ilala kuja Magomeni, Daraja la Ubungo karibu na njia panda ya kwenda UDSM na barabara ya Mandela Road ukitokea Tazara kuja Ubungo (NDIPO ALIPOVAMIWA RAFIKI YANGU)
His Case.

Akiwa kwenye folen majira ya saa mbili usiku, ghafla lilitokea kundi la vijana kama kumi na mapanga na kuanza kupiga vioo vya gari
wakitaka kuvunja, aidha waliongezeka ghafla na wakafunga barabara kama kwa dk 7 hivi wakiendelea kumshambulia (kwenye gari walikuwa watatu),kumbuka kwenye foleni huwezi kukimbia popote, Mungu aliwasaidia sana kwani milango ya gari ilikuwa imefungwa/locked, na vioo vilikuwa vimefungwa kasoro kimoja kilikuwa wazi nusu.

Baada ya mapambano na kelele za kuomba msaada,ndipo msamalia mwema aliyekuwa na silaha aliingilia kati na ndipo alipowatawanya.Kwa mujibu wa Taarifa mbalimbali, haya matukio yamekuwa yakiongezeka sana katika siku za usoni, kwa hilo nawatahadharisha msinunue vitu ovyokwenye traffic light, vioo msishushe ovyo na lock za milango ya magari mfunge, muwe makini.
Ujambazi huu unafanyika kila siku sehemu tofauti kuanzia saa 12 jioni kuendelea.

Namshukuru Mungu hakuna aliyeumizwa sana, japo walifanikiwa kupata baadhi ya vitu ikiwemo simu ya mwenye gari.Natambua unaweza kuona kama sinema,ila haya ndio yanayotokea katika jiji la Dar kwenye foleni za magari.
Mdau Dar
Kwa hisani ya blog ya Michuzi
 
Ninamkumbuka Mzee Ali Haji Hassan Mwinyi alisema, "pengo la wenye nacho na wasio nacho linapoongezeka, linasababisha pale yule aliyenacho anapotumia asiyenacho huona anaonewa".
 
kwa tunaotembea na manati ya mzungu,ukiona kundi limekuzunguka na mapanga na nondo,na ukiona wanaanza kuvunja vioo,usingoje kusikia parapanda. Lenga na kuachia kwa watatu au wanne,magari yenyewe ya mikopo haya,yanavyouma!
 
Back
Top Bottom