MANKA MUSA
JF-Expert Member
- Jul 9, 2014
- 922
- 1,093
Kijana mmeba box nikipata nafasi ya kupumzika huwa napitia sana mitandaoni si unajua huku hauli bila kazi, kilichonishangaza ni update za Vijana waliopo Tanzania wakishangilia ubabe wa Putin na story kuhusu uharibifu wa Putini. Nikajiuliza Vijana hawa wanafahamu balaa lililopo mbele Yao hawa?
sasa hivi majuzi hapa Dubai nimeshuhudia bei kali ya mafuta na foleni ndefu ya magari wakigombania kujaza mafuta kabla ya tarehe moja Julai nikajiuliza hapo nyumbani Bongo hali itakuwaje…? Kisha nikawakumbuka wale Vijana wanaomshangilia Putin kwenye mitandao.
Wakati Nikiwa na Peruzi nikakutana na Habari ya anguko la Uchumi wa nchi ya Sri Lanka shule zimefungwa kwa muda wa wiki ya tatu mfululizo, kutokana na uhaba wa mafuta ya kuendeshea magari ya kusafirisha walimu na wanafunzi.
Waziri wa Elimu amewataka walimu na wanafunzi ambao wameathirika na tatizo hilo kutumia mafunzo kwa njia ya mtandao hadi pale tatizo hilo litakapokuwa limepatiwa ufumbuzi.
Waziri wa Nishati wa Sri Lanka, Kanchana Wijesekera amesema, shehena ya kwanza ya mafuta ya tani elfu 40 inatarajiwa kuwasili nchini humo tarehe 22 mwezi huu.
Serikali ya Sri Lanka inahitaji dola milioni 587 kwa ajili ya kununulia mafuta ambapo nchi hiyo inadaiwa dola milioni 800 na wasambazaji wa mafuta kutokana na deni la kuagiza nishati hiyo nchini humo. Vijana wa Sri Lanka hawawezi kumsifia Putin kwa madhara ya vita hivi wameona matokeo yake.
Sisi hapa nyumbani tunaweza kubeza hizi bilioni 100 za Ruzuku ya mafuta kwa kuwa tumejaliwa midomo ya kuongea tungetembea kujionea Marekani wananchi wake wanavyotaabika, majuzi pale Uingereza kwa Malikia watu wakiaandamana juu ya hali ngumu ya maisha.
Hapa JF kuna Uzi zinazomsifia Putin na kuponda Ruzuku ya bilioni 100 inayotolewa na serikali kunusuru kupanda kwa bei ya mafuta nchi.
sasa hivi majuzi hapa Dubai nimeshuhudia bei kali ya mafuta na foleni ndefu ya magari wakigombania kujaza mafuta kabla ya tarehe moja Julai nikajiuliza hapo nyumbani Bongo hali itakuwaje…? Kisha nikawakumbuka wale Vijana wanaomshangilia Putin kwenye mitandao.
Wakati Nikiwa na Peruzi nikakutana na Habari ya anguko la Uchumi wa nchi ya Sri Lanka shule zimefungwa kwa muda wa wiki ya tatu mfululizo, kutokana na uhaba wa mafuta ya kuendeshea magari ya kusafirisha walimu na wanafunzi.
Waziri wa Elimu amewataka walimu na wanafunzi ambao wameathirika na tatizo hilo kutumia mafunzo kwa njia ya mtandao hadi pale tatizo hilo litakapokuwa limepatiwa ufumbuzi.
Waziri wa Nishati wa Sri Lanka, Kanchana Wijesekera amesema, shehena ya kwanza ya mafuta ya tani elfu 40 inatarajiwa kuwasili nchini humo tarehe 22 mwezi huu.
Serikali ya Sri Lanka inahitaji dola milioni 587 kwa ajili ya kununulia mafuta ambapo nchi hiyo inadaiwa dola milioni 800 na wasambazaji wa mafuta kutokana na deni la kuagiza nishati hiyo nchini humo. Vijana wa Sri Lanka hawawezi kumsifia Putin kwa madhara ya vita hivi wameona matokeo yake.
Sisi hapa nyumbani tunaweza kubeza hizi bilioni 100 za Ruzuku ya mafuta kwa kuwa tumejaliwa midomo ya kuongea tungetembea kujionea Marekani wananchi wake wanavyotaabika, majuzi pale Uingereza kwa Malikia watu wakiaandamana juu ya hali ngumu ya maisha.
Hapa JF kuna Uzi zinazomsifia Putin na kuponda Ruzuku ya bilioni 100 inayotolewa na serikali kunusuru kupanda kwa bei ya mafuta nchi.