Vijana wajifunze staha kwa taifa na uongozi wake.

sekulu

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
988
157
Vijana wajifunze staha kwa taifa na uongozi wake sio kukurupuka bila hoja mwaka 2014 nilimshusha Joshua Nasary jukwaani aliposema Kikwete asiende Arusha ni nchi ya CHADEMA. Tuna rasilimali chache kuwatetea mahakamani FANYENI KAZI MKIHOJI MHOJI KWA EVIDENCE NA HOJA KUNTU ifike mahali tusiwe watu wa mahakamani kwa makosa ya kuropoka jukwaani na mitandaoni ni MUDA WA KAZI

SOURCE
 
Naona kama hoja yako haijakaa sawa, sema vijana wajifunze woga, maana woga sasa ni mali hasa kwa hawa vijana waliozoea kusema ukweli kama ulivyo na wanaoambiwa hawako tayari kuuvumilia ukweli huo.
 
Vijana wajifunze staha kwa taifa na uongozi wake sio kukurupuka bila hoja mwaka 2014 nilimshusha Joshua Nasary jukwaani aliposema Kikwete asiende Arusha ni nchi ya CHADEMA. Tuna rasilimali chache kuwatetea mahakamani FANYENI KAZI MKIHOJI MHOJI KWA EVIDENCE NA HOJA KUNTU ifike mahali tusiwe watu wa mahakamani kwa makosa ya kuropoka jukwaani na mitandaoni ni MUDA WA KAZI

SOURCE
Serikali iheshimu wananchi wake! Vijana sii vichaa wafanye wafanyao! Serikali ni ya Wananchi na sii ya Familia chache zinazoishi enzi za Ujima katika Karne hii ya 21. Uongozi si vinyongo,hasira,visasi,kukomoana,na kujiona wewe ndo Alfa na Omega! Ni vema sasa watawala Waka concentrate kwenye mambo ya msingi badala ya kushughulika na Watu Wanaoonesha HISIA zao!
 
Message sent and delivered to Nyumbuz
Mimi naona watu wanalitumia vibaya hili jina nyumbu, kila nikipitia katika comments hapa wakati mwingine sioni utofauti, hivyo kifupi tunao Nyumbu wa kijani na Nyumbu upinzani. Nyumbu upinzani ni wale ambao wanajua kabisa kuwa wanachezewa akili na wanaowaita makamanda na bado wanawashangilia, na Nyumbu wa kijani ni hatari zaidi ya nyumbu upinzani maana hawa wanajitolea kuwa vipofu kujifanya hawaoni nini kinatokea mitaani na bado wanasifu. Watanzania ambao siyo nyumbu ni wale ambao wanakosoa pale panapotakiwa kukosolewa bila kujali wanamkosoa CDM,CCM, Upinzani ama serikali. Hawa ni raia wapenda nchi yao. Lakini nyumbu wa kivyama Tanzania wanawaibisha hata nyumbu orignal maana nyumbu wa Serengeti walao wanatumia akili zao kujua msimu umefika wa kuhamia maasai mara lakini nyumbu wa hapa JF wanajisahau mpaka kitu kilichotokea jana hawakikumbuki kama mwanasiasa jana alikua CDM akihamia CCM wanamshangilia vivyo hivyo kama jana alikua CCM akihamia CDM anapewa jina jipya kamanda.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom