CarloJesus
JF-Expert Member
- Nov 5, 2019
- 431
- 833
Naandika kwa masikitiko, imejengeka namna hii, kuwa ili tuwafurahishe watu ama watu/mtu afurahi ni lazima uwepo ulevi fulani.
Viko vilevi vingi, wengine shisha, wengine kungu, wengine madawa, wengine bangi/jani nk. Bahati mbaya hili limekuwa kama fashion, ambao hawakuwa walevi wengi wameingia kwa mkumbo.
Haya yameingia katika akili ya mtu kutoka ama, katika familia, jamii inayotuzunguka hata vitu kama picha na movies ambayo pombe inasifiwa sana bila nguvu hiyo hiyo kutumika kuonyesha madhara yake, humu pia kuna uzi wa walevi.
Ieleweke kuwa siongei ukamilifu wa maadili ya kidini au miiko fulani, hayo siwezi kuyagusia kwa sababu kila mtu kafungwa kwa imani yake, na bahati mbaya imani si rahisi kuhoji.
Naongea haya baada ya kuona rafiki yangu ambaye tayari alikuwa na future nzuri, alikuwa na ajira yake, lakini kwa ajili ya mkumbo mambo yote yameharibika.
Amefika hatua mbaya, alitemwa kazini kwa sababu ya pombe, udhuru ulizidi ikafika hatua akawa anaenda ama anaamka nazo kazini.
Navyoongea yuko kijijini anakunywa gongo hana mbele wala nyuma, amekuwa kama chizi, zaidi alichobaki nacho ni Kiingereza tu.
Mimi nakunywa pombe, lakini si tegemezi wa pombe katika furaha yangu.
Vijana wadogo mnaopata ajira na kuanza maisha ya uhuru mbali na wazazi, pombe/ulevi si starehe pekee ya kukupa furaha.
Viko vilevi vingi, wengine shisha, wengine kungu, wengine madawa, wengine bangi/jani nk. Bahati mbaya hili limekuwa kama fashion, ambao hawakuwa walevi wengi wameingia kwa mkumbo.
Haya yameingia katika akili ya mtu kutoka ama, katika familia, jamii inayotuzunguka hata vitu kama picha na movies ambayo pombe inasifiwa sana bila nguvu hiyo hiyo kutumika kuonyesha madhara yake, humu pia kuna uzi wa walevi.
Ieleweke kuwa siongei ukamilifu wa maadili ya kidini au miiko fulani, hayo siwezi kuyagusia kwa sababu kila mtu kafungwa kwa imani yake, na bahati mbaya imani si rahisi kuhoji.
Naongea haya baada ya kuona rafiki yangu ambaye tayari alikuwa na future nzuri, alikuwa na ajira yake, lakini kwa ajili ya mkumbo mambo yote yameharibika.
Amefika hatua mbaya, alitemwa kazini kwa sababu ya pombe, udhuru ulizidi ikafika hatua akawa anaenda ama anaamka nazo kazini.
Navyoongea yuko kijijini anakunywa gongo hana mbele wala nyuma, amekuwa kama chizi, zaidi alichobaki nacho ni Kiingereza tu.
Mimi nakunywa pombe, lakini si tegemezi wa pombe katika furaha yangu.
Vijana wadogo mnaopata ajira na kuanza maisha ya uhuru mbali na wazazi, pombe/ulevi si starehe pekee ya kukupa furaha.