Vijana wa Tanzania watakapoacha kumilikiwa na Vyama vya Siasa ndio tutapata Katiba Mpya. Mnyika aliwahi kupigania Baraza la Vijana!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
82,754
139,558
Huwezi kupata Katiba Mpya bila ya Kuwa na movement (Vuguvugu) sahihi na hiyo hufanywa na Vijana wenye fikra Huru

Alichofanikiwa Nyerere na ambacho Wapinzani wamerithi pia ni kuzikamata fikra za Vijana tangu wakiwa Shuleni na Vyuoni

Ndio sababu kama Taifa hatuwezi kusogea kwa sababu Vijana hawako Huru kifikra ndio hawa CHAWA wanaozaliana kila iitwapo leo

Kuna wakati J J Mnyika alipigania uwepo wa Baraza la Vijana pale Bungeni lakini cha ajabu Jafo akajipenyeza na kujifanya 'kijana' akaipora ile hoja na ikafia mikononi mwake

Ukitaka kujua sumu ya vyama muangalie Polepole wa Tume ya Warioba kisha muangalie Polepole wa Sekretarieti ya CCM

Jumaa kareem!
 
Pale Jambazi anapokuwa ametubu injili yake huwa nzuri mnoo ikiambatana na shuhuda za ukweli ambazo zinasisimua🙌🙌🙌🙌
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom