Ningependa kutoa msimamo wangu juu ya matukio yanayotoke huko Arusha kama kijana Mtanzania, mpenda nchi yangu na watu wake, pia kama kijana kiongozi ndani ya UVCCM.
Siridhishwi na hali inayoendelea huko Mkoani Arusha na jinsi suala hilo linavyoshughulikiwa.
Siridhishwi na namna ya dola inavyowabagua vijana wa arusha kutokana na kutofautiana kiitikadi na chama tawala, na hivyo kuwa ni tiketi ya kuwafanyia unyanyasaji, udhalilishaji na uonevu wa kila hali. Vijana ndio wanaoshiriki kudai kile wanachokidai, hawsikilizwi, badala yake wanakumbana na kikwazo cha vitisho, mabomu, risasi za moto, kufunguliwa mashitaka pamoja na kudhalilishwa mbele ya raia.
Vijana wa CCM tunabeza haya, tunafurahia, tumesimama pembeni tukiwa tunaangali kinachoendelea. Ila tukumbuke, nje ya itikadi zetu za vyama, vijana wote ni wamoja, vijana wote ndio tutakalolijenga taifa hili sasa na hapo baadaye.
Katika kujenga taifa haihitaji nguvu ya itikadi moja, bali ni nguvu ya pamoja. Kama katika hili vijana wa ccm tutakuwa tunajitenga nalo basi tujue tunajitengenezea au tunatengenezewa mwanzo mbaya wa kutokuja shirikiana hapo baadaye kuijenga nchi yetu kwa umoja uliokuwepo hapo zamani.
Ningependa kutoa nasaha kwa serikali yangu ya CCM, watambue kwamba Arusha ni zaidi ya siasa, Arusha ni sehemu muhimu sana kwa uchumi wetu, sekta ya utalii ni ya pili katika kuchangia pato la taifa. Hakuna utalii bila kujumuisha mji wa arusha. Arusha ndio serengeti. Arusha ndio manyara, arusha ndio mlima kilimanjaro na arusha ndio Tanzanite. Pia Arusha ni kituo kikubwa kwa diplomasia ya kimataifa na mahusiano ya masuala mbalimbali ya kijumuiya na mashirikiano ya kikanda.
Si sahihi kuacha tunu yote hiyo ipotee kwa maslahi madogo ya kisiasa na matakwa ya kundi ama hisia za kiitikadi. Chadema imefanya makosa, CCM imefanya makosa.
Lakini CCM imefanya makosa makubwa zaidi kwakuwa wao baada ya kushika dola mgogoro uliozaliwa kwenye siasa wakauhamishia kwenye dola na chadema kubaki na wanasiasa, hivyo dola kupitia jeshi la polisi wanapambana na ugomvi ambao haukutakiwa ufike kwao. Na sasa tunaona madhara yake.
Wanasiasa waliohusika na yanayotokea Arusha warudi nyuma, waache ubabe kwa kuwa wao wana dola, wana nguvu ya majeshi na kauli za kuamrisha chochote.
Ikumbukwe wakati tunapigania uhuru hatukumwaga damu. Ila sasa tunagombania madaraka tunamwaga damu, tunauwana wenyewe kwa wenyewe, hii sio maana ya uhuru tulioutaka.
Vijana wa CCM tukiacha unyanyasaji huu kwa vijana na viongozi wa upinzani basi dhambi hii haitaishia hapo, itajirudia. Itafika wakati vijana ambao wamo ndani ya CCM lakini wanapingana kimtazamo na kiongozi fulani ambaye ana ushawishi kuwaambia polisi washughulikie kundi fulani kwenye ccm itakuwa hivyo.
Daima mwisho wa yote, manyanyaso, mateso na dhulma haki ndiyo mshindi na daima ukweli ndio utamuweka mtu huru. Kama viongozi wa serikali yangu ya CCM wakaona hakuna busara inayohitajika kusikiliza malalamiko wanayodai wapinzani basi dhana ya kuchagua viongozi kwa kuzingatia busara zao utakuwa haukufuatwa, kwani busara tungependa kuiona kwenye masuala kama haya.
Vijana tunatakiwa tukatae matumizi ya nguvu dhidi ya wananchi bila kujali itikadi zetu, kwani hili ni jukumu letu kama katiba ya ccm inavyosema. Lakini pia tunajukumu la kusimamia na kutilia mkazo juu ya kutendeka kwa haki za msingi za kikatiba ili tanzania iwe sehemu huru kwa maisha ya kila mmoja!
"Tujisahihishe"
M. Nyundo.
Mjumbe, Baraza kuu UVCCM (M)
Siridhishwi na hali inayoendelea huko Mkoani Arusha na jinsi suala hilo linavyoshughulikiwa.
Siridhishwi na namna ya dola inavyowabagua vijana wa arusha kutokana na kutofautiana kiitikadi na chama tawala, na hivyo kuwa ni tiketi ya kuwafanyia unyanyasaji, udhalilishaji na uonevu wa kila hali. Vijana ndio wanaoshiriki kudai kile wanachokidai, hawsikilizwi, badala yake wanakumbana na kikwazo cha vitisho, mabomu, risasi za moto, kufunguliwa mashitaka pamoja na kudhalilishwa mbele ya raia.
Vijana wa CCM tunabeza haya, tunafurahia, tumesimama pembeni tukiwa tunaangali kinachoendelea. Ila tukumbuke, nje ya itikadi zetu za vyama, vijana wote ni wamoja, vijana wote ndio tutakalolijenga taifa hili sasa na hapo baadaye.
Katika kujenga taifa haihitaji nguvu ya itikadi moja, bali ni nguvu ya pamoja. Kama katika hili vijana wa ccm tutakuwa tunajitenga nalo basi tujue tunajitengenezea au tunatengenezewa mwanzo mbaya wa kutokuja shirikiana hapo baadaye kuijenga nchi yetu kwa umoja uliokuwepo hapo zamani.
Ningependa kutoa nasaha kwa serikali yangu ya CCM, watambue kwamba Arusha ni zaidi ya siasa, Arusha ni sehemu muhimu sana kwa uchumi wetu, sekta ya utalii ni ya pili katika kuchangia pato la taifa. Hakuna utalii bila kujumuisha mji wa arusha. Arusha ndio serengeti. Arusha ndio manyara, arusha ndio mlima kilimanjaro na arusha ndio Tanzanite. Pia Arusha ni kituo kikubwa kwa diplomasia ya kimataifa na mahusiano ya masuala mbalimbali ya kijumuiya na mashirikiano ya kikanda.
Si sahihi kuacha tunu yote hiyo ipotee kwa maslahi madogo ya kisiasa na matakwa ya kundi ama hisia za kiitikadi. Chadema imefanya makosa, CCM imefanya makosa.
Lakini CCM imefanya makosa makubwa zaidi kwakuwa wao baada ya kushika dola mgogoro uliozaliwa kwenye siasa wakauhamishia kwenye dola na chadema kubaki na wanasiasa, hivyo dola kupitia jeshi la polisi wanapambana na ugomvi ambao haukutakiwa ufike kwao. Na sasa tunaona madhara yake.
Wanasiasa waliohusika na yanayotokea Arusha warudi nyuma, waache ubabe kwa kuwa wao wana dola, wana nguvu ya majeshi na kauli za kuamrisha chochote.
Ikumbukwe wakati tunapigania uhuru hatukumwaga damu. Ila sasa tunagombania madaraka tunamwaga damu, tunauwana wenyewe kwa wenyewe, hii sio maana ya uhuru tulioutaka.
Vijana wa CCM tukiacha unyanyasaji huu kwa vijana na viongozi wa upinzani basi dhambi hii haitaishia hapo, itajirudia. Itafika wakati vijana ambao wamo ndani ya CCM lakini wanapingana kimtazamo na kiongozi fulani ambaye ana ushawishi kuwaambia polisi washughulikie kundi fulani kwenye ccm itakuwa hivyo.
Daima mwisho wa yote, manyanyaso, mateso na dhulma haki ndiyo mshindi na daima ukweli ndio utamuweka mtu huru. Kama viongozi wa serikali yangu ya CCM wakaona hakuna busara inayohitajika kusikiliza malalamiko wanayodai wapinzani basi dhana ya kuchagua viongozi kwa kuzingatia busara zao utakuwa haukufuatwa, kwani busara tungependa kuiona kwenye masuala kama haya.
Vijana tunatakiwa tukatae matumizi ya nguvu dhidi ya wananchi bila kujali itikadi zetu, kwani hili ni jukumu letu kama katiba ya ccm inavyosema. Lakini pia tunajukumu la kusimamia na kutilia mkazo juu ya kutendeka kwa haki za msingi za kikatiba ili tanzania iwe sehemu huru kwa maisha ya kila mmoja!
"Tujisahihishe"
M. Nyundo.
Mjumbe, Baraza kuu UVCCM (M)