MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Napenda niwashauri tu vijana wenzangu wa chama cha mapinduzi CCM, chama chenu kimepewa dhamana kubwa sana na wananchi. Onesheni utofauti wenu na vyama viingine msikalie kimya mambo makubwa ya kitaifa kwa kuusoma upepo, hizi ni akili za watu wa kuswagwa utafikiri hawajitambui.Msilifanye kila jambo kua ni lakutaftia umaarufu wa kisiasa,wenzenu wa upinzani wanakesha hawalali kutafuta vyanzo vya taarifa mbali mbali na kuzitengenezea hojalakini ninyi mnalala udingizi mnasubiri kupinga hizo hoja kwa kutukana na kukejeli. Hili litawagharimu sana wakati ni mwalimu mzuri sana.
Sio uzalendo hata kidogo pale linapotokea jambo ambalo linalitikisa taifa letu mnakalia kimya mnasubiri kusoma upepo ndio mseme, haya ni mawazo ya ajabu kabisa na hamtalisaidia taifa. Ni bora mu ushinde na njaa kwa kusema ukweli maana kweli hiyo hiyo itakushibisha kesho. Vijana wa CCM mmekosa uzalendo jaribuni kufikiria kua taifa lijao ni lenu ikiwa mtasimama imara.Mwl Nyerere mpaka anakabidhi kijiti cha kuisimamia TANU hakua na tabia hii, haua mtu wa kuogopa ogopa kama ninyi.Hakua mtu wa kupelekwa na upepo na ndio maana kwenye CCM hii ya leo hakuna kijana wa kufanana nae.
Nataka niamini kwamba hata teuzi nyingi zinazofanywa na Mh Rais ni kwa maprofesa wa PhDs na vijana kutoka upinzani sio kwamba hawaoni vijana wa CCM, kuna siku mh Rais aliwahi kusema amepelekewa majina kutoka UVCCM kwa ajili ya teuzi mbali mbali lakini hakuona kabisa wenye sifa.Mkae na kujiuliza ni sifa zipi Mh Rais anataka? Ameshawasoma mlivyo, sura zenu hazijakaa kulisaidia taifa.Anaaminu niyi sura zenu hazioneshi kumpa msaada wa kulijenga taiga.
Leo hii hata ukifukuzwa ndani ya chama hako kwa kusimama katika ukweli taifa litakutambua tuu, nyota yako haitokaa kuzimika ispokua ni rahisia sana kuzimwa na tabia kama hizi.
Amkeni teteeni mambo yenye maslahi ya umma, msiwe vigeu vigeu kama PETRO ambaye aliusoma upepo akaona ni bora adanganye kwa kumkana YESU kukwepa mijeledi ya wayahudi.
Ushauri wangu ni huo kwenu, mpokee au msipokee chamsingi ujumbe umewafikia, acheni kua na udhaifu kubwa kiasi hiki maana hauna tija kwa taifa wala chama chenu.
Sio uzalendo hata kidogo pale linapotokea jambo ambalo linalitikisa taifa letu mnakalia kimya mnasubiri kusoma upepo ndio mseme, haya ni mawazo ya ajabu kabisa na hamtalisaidia taifa. Ni bora mu ushinde na njaa kwa kusema ukweli maana kweli hiyo hiyo itakushibisha kesho. Vijana wa CCM mmekosa uzalendo jaribuni kufikiria kua taifa lijao ni lenu ikiwa mtasimama imara.Mwl Nyerere mpaka anakabidhi kijiti cha kuisimamia TANU hakua na tabia hii, haua mtu wa kuogopa ogopa kama ninyi.Hakua mtu wa kupelekwa na upepo na ndio maana kwenye CCM hii ya leo hakuna kijana wa kufanana nae.
Nataka niamini kwamba hata teuzi nyingi zinazofanywa na Mh Rais ni kwa maprofesa wa PhDs na vijana kutoka upinzani sio kwamba hawaoni vijana wa CCM, kuna siku mh Rais aliwahi kusema amepelekewa majina kutoka UVCCM kwa ajili ya teuzi mbali mbali lakini hakuona kabisa wenye sifa.Mkae na kujiuliza ni sifa zipi Mh Rais anataka? Ameshawasoma mlivyo, sura zenu hazijakaa kulisaidia taifa.Anaaminu niyi sura zenu hazioneshi kumpa msaada wa kulijenga taiga.
Leo hii hata ukifukuzwa ndani ya chama hako kwa kusimama katika ukweli taifa litakutambua tuu, nyota yako haitokaa kuzimika ispokua ni rahisia sana kuzimwa na tabia kama hizi.
Amkeni teteeni mambo yenye maslahi ya umma, msiwe vigeu vigeu kama PETRO ambaye aliusoma upepo akaona ni bora adanganye kwa kumkana YESU kukwepa mijeledi ya wayahudi.
Ushauri wangu ni huo kwenu, mpokee au msipokee chamsingi ujumbe umewafikia, acheni kua na udhaifu kubwa kiasi hiki maana hauna tija kwa taifa wala chama chenu.