Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Mpoki Bukuku, Pemba na Salim Said
CHAMA cha wananchi (CUF) kimedai vitambulisho vya ukaazi vinatolewa kwa vijana wa bara ili waweze kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwakani.
Akizungumza Mjini Wete, mbunge wa viti maalum wa chama hicho, Riziki Omar Juma, alidai kwa sasa baadhi ya vijana wameshapatiwa vitambulisho kwajili yakujiandikisha kupiga kura mwakani na wengine wanatarajiwa kuingia Zanzibar wakati wa mbio za mwenge.
"Sasa umefika wakati wa kuwashughulikia watu hawa kwani wapemba wakiwa na chao wanatoa kwa hiari si kwa nguvu," alisema na kuongeza kuwa vijana wajihadhari wakati wa mbio za mwenge kwani vijana wengi wataletwa na kusambazwa sehemu mbalimbali.
Akizungumzia suala hilo Katibu Mkuu wa CUF, alisema kuwa wabara wengi wamekuwa wakipewa vitambulishio hivyo na Wapemba wakiachwa bila ya kitu kinachowasababisha kupoteza haki ya kupiga kura.
Alitoa mfano wa baadhi ya mikoa ambako kuna mvuto kwa chama cha CUF ambako maelfu ya wananchi wamezuiwa kupata fomu za vitambulisho hivyo kwa madai kuwa hawana sifa, lakini maeneo mengine ya CCM kila mtu anapatiwa.
Wakati huo huo wazee wanaotetea kujitenga kwa kisiwa cha Pemba, wameitaka Jumuiya ya Umoja wa Mataifa (UN) kuingilia kati zoezi la uboreshaji wa daftari la wapigakura kisiwani humo, ili kuepusha maafa makubwa ambayo yanaweza kusababishwa na zoezi hilo.
Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa wazee hao Hamad Ali Mussa alisema, tayari wameiandikia UN barua (nakala tunayo) wakiitaka kuingilia kati zoezi hilo na kwamba waliifikisha ofisi za UN jijini hapa siku ya Julai 30 mwaka huu.
Alisema, UN kupitia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) iliahidi kubeba jukumu la kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar mwakani utakuwa huru na wa haki na haitavumilia Taasisi yoyote itakayoonekana kwamba inataka kuhatarisha amani kwa kuchafua uchaguzi huo.
"Usajili wa wapigakura ni hatua muhimu ya mchakato wa uchaguzi mkuu, tayari kuna ushahidi wa kutosha kwamba mchakato huu umeshavurugwa na unaendelea kuvurugwa vibaya," alisema na Mussa na kusisitiza:
"Kwa hivyo tunaiomba mamlaka ya UN kuingilia kati zoezi hilo katika hatua hii ya awali ambapo ni muda mzuri bado, ikitokea juhudi za UN kusimamia uchaguzi visiwani Zanzibar kushindwa, tunaiomba kutumia nguvu zake kuizuia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kufanya uchaguzi mkuu mwakani hadi hapo madai yao yatakapotekelezwa".
Alisema, unyama wote unaofanywa na SMZ katika usajili wa wapigakura unafadhiliwa na UN kupitia UNDP na kwamba mabaya yoyote yaliyotokea, yanayotokea na yatakayoendelea kutokea lawama zake zitabebwa na Umoja huo.
"UN ikae ikijua kwamba damu ya kwanza kumwagika kwa ajili ya kutetea demokrasia ya vyama vingi nchini ni ya Kisiwa cha Pemba, hivyo kama inapuuzia hilo basi ituachie sisi tuliwe na samaki na hao wachache watakaobakia itakuja kuwabwagia 'vibiskuti' na mahema," alisema kwa uchungu Mussa.
Kwa upande wake Katibu wa wazee hao Ali Makame alisema kwa sasa hawako tayari kuvumilia kuona haki yoyote ya watu wa kisiwa hicho ikidhulumiwa na utawala wa SMZ.
Alisema, kinachofanywa Pemba hivi sasa katika zoezi la kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura ni unyama na uvunjaji wa katiba ambao matokeo yake ni kutoweka kwa utulivu na amani ya kisiwa hicho.
SOURCE: MWANANCHI.
CHAMA cha wananchi (CUF) kimedai vitambulisho vya ukaazi vinatolewa kwa vijana wa bara ili waweze kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwakani.
Akizungumza Mjini Wete, mbunge wa viti maalum wa chama hicho, Riziki Omar Juma, alidai kwa sasa baadhi ya vijana wameshapatiwa vitambulisho kwajili yakujiandikisha kupiga kura mwakani na wengine wanatarajiwa kuingia Zanzibar wakati wa mbio za mwenge.
"Sasa umefika wakati wa kuwashughulikia watu hawa kwani wapemba wakiwa na chao wanatoa kwa hiari si kwa nguvu," alisema na kuongeza kuwa vijana wajihadhari wakati wa mbio za mwenge kwani vijana wengi wataletwa na kusambazwa sehemu mbalimbali.
Akizungumzia suala hilo Katibu Mkuu wa CUF, alisema kuwa wabara wengi wamekuwa wakipewa vitambulishio hivyo na Wapemba wakiachwa bila ya kitu kinachowasababisha kupoteza haki ya kupiga kura.
Alitoa mfano wa baadhi ya mikoa ambako kuna mvuto kwa chama cha CUF ambako maelfu ya wananchi wamezuiwa kupata fomu za vitambulisho hivyo kwa madai kuwa hawana sifa, lakini maeneo mengine ya CCM kila mtu anapatiwa.
Wakati huo huo wazee wanaotetea kujitenga kwa kisiwa cha Pemba, wameitaka Jumuiya ya Umoja wa Mataifa (UN) kuingilia kati zoezi la uboreshaji wa daftari la wapigakura kisiwani humo, ili kuepusha maafa makubwa ambayo yanaweza kusababishwa na zoezi hilo.
Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa wazee hao Hamad Ali Mussa alisema, tayari wameiandikia UN barua (nakala tunayo) wakiitaka kuingilia kati zoezi hilo na kwamba waliifikisha ofisi za UN jijini hapa siku ya Julai 30 mwaka huu.
Alisema, UN kupitia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) iliahidi kubeba jukumu la kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar mwakani utakuwa huru na wa haki na haitavumilia Taasisi yoyote itakayoonekana kwamba inataka kuhatarisha amani kwa kuchafua uchaguzi huo.
"Usajili wa wapigakura ni hatua muhimu ya mchakato wa uchaguzi mkuu, tayari kuna ushahidi wa kutosha kwamba mchakato huu umeshavurugwa na unaendelea kuvurugwa vibaya," alisema na Mussa na kusisitiza:
"Kwa hivyo tunaiomba mamlaka ya UN kuingilia kati zoezi hilo katika hatua hii ya awali ambapo ni muda mzuri bado, ikitokea juhudi za UN kusimamia uchaguzi visiwani Zanzibar kushindwa, tunaiomba kutumia nguvu zake kuizuia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kufanya uchaguzi mkuu mwakani hadi hapo madai yao yatakapotekelezwa".
Alisema, unyama wote unaofanywa na SMZ katika usajili wa wapigakura unafadhiliwa na UN kupitia UNDP na kwamba mabaya yoyote yaliyotokea, yanayotokea na yatakayoendelea kutokea lawama zake zitabebwa na Umoja huo.
"UN ikae ikijua kwamba damu ya kwanza kumwagika kwa ajili ya kutetea demokrasia ya vyama vingi nchini ni ya Kisiwa cha Pemba, hivyo kama inapuuzia hilo basi ituachie sisi tuliwe na samaki na hao wachache watakaobakia itakuja kuwabwagia 'vibiskuti' na mahema," alisema kwa uchungu Mussa.
Kwa upande wake Katibu wa wazee hao Ali Makame alisema kwa sasa hawako tayari kuvumilia kuona haki yoyote ya watu wa kisiwa hicho ikidhulumiwa na utawala wa SMZ.
Alisema, kinachofanywa Pemba hivi sasa katika zoezi la kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura ni unyama na uvunjaji wa katiba ambao matokeo yake ni kutoweka kwa utulivu na amani ya kisiwa hicho.
SOURCE: MWANANCHI.
Last edited by a moderator: