smarte_r
JF-Expert Member
- Nov 8, 2013
- 4,538
- 11,868
Nimeandika uzi huu baada ya kuvutiwa na mjadala unaondelea kwenye uzi wa APPROXIMATELY: ARUSHA, nakupenda sana, najivunia kuzaliwa Arusha...
Licha ya jiji la Dar kuwa na hali ya hewa ya joto kwa kipindi kirefu cha mwaka, hali ambayo sio rafiki kwa baadhi yetu, Mungu ana kusudi lake kulifanya jiji hili liwe the capital city of Tanzania.
Utake usitake, Dar ni jiji namba moja la kibiashara nchini na Afrika Mashariki likicheza ligi moja na Nairobi, Kampala na Kigali.
Ni jiji ambalo kila mtu kutoka kila kabila lake, anapatikana na kufanya shughuli zake za kiuchumi kwa amani bila kusimangwa au kubugudhiwa na wenyeji ambao ni wazaramo, wandengereko na wakwere.
Niseme tu ukweli, watu wa Pwani licha ya mapungufu yao machache, ni wastaarabu, waungwana na wakarimu sana. wenyeji wa mji huu wamewakaribisha na kuwakarimu wageni wengi waliohamia Dar na kupageuza kuwa makazi yao ya kudumu.
Dar ni jiji la fursa, jiji la kutengeneza network na connection za kutoboa kimaisha kupitia wadau mbalimbali utakao kutananao kwenye mishe zako. Huwa naifananisha Dar na taifa la Marekani kupitia ile concept yao ya chasing the American Dream.
Kama wewe ni kijana uliyeweka malengo ya kufanikiwa kupitia talent mbalimbali hususani uigizaji au mziki, utake usitake lazima utoke mkoani kwenu uje dar ujiweke karibu na big fish wa industry husika.
Mfano mdogo ni wasanii wa Arusha kama Dogo Janja, Joh Makini na wenzake wa kundi la weusi. Hawa wote wamefika hapo walipofika baada ya kuhamia Dar halafu wakashikwa mkono na watoto wa mjini wa jiji hili(sina haja ya kuwataja, jamii inajua).
Laiti kama Arusha ndio ingekuwa the main capital city ya Tanzania kama lilivyo jiji la Dar, basi vijana wa mikoa mingine ambao wangehamia Arusha, wangeishi kwa manyanyaso sana kutoka kwa vijana wazawa wa Arusha. pengine wangefukuzwa warudi makwao na labda tungekuwa tunashuhudia xenophobic incidents kama zile za South Africa.
Nalisema hili kwasababu ya arrogant, rude behaviour and uncivilised culture ya vijana wa Arusha. Hapo kwenye uncivilised culture wote ni mashahidi wa ile tabia yao kuvuta bangi kiholela na kijisifiia kana kwamba ni ufahari.
Pia ile dress code yao ya kuvaa mashati oversize na mabuti makubwa. Nakumbuka huu uvaaji walikuwa wanavaa vijana wa Dar katikati na mwishoni mwa90s. For now this dress code style is out of date.
Mtindo huu wa uvaaji ulichochewa na wasanii wakubwa wa mziki wa rap huko Marekani. Ni miaka ambayo Dr Dre na Snoop Dogg walikuwa wanatamba na ngoma yao ya nuthin' but a "G" thang, the late 2pac akitamba na me against the world.
Jambo lingine ni tabia ya chuki na kujiona superior dhidi ya vijana wenzao wa mikoa mingine specifically wa Dar.
Mimi ni mhanga wa hili, huwa natembelea Arusha mara nyingi tu. Kuna siku niliingia duka moja la kuuza viatu, wale vijana walinipokea vizuri tu. Ila baada ya kusikia kiswahili changu na kugundua natokea Dar, customer care yao ikabadilia ghafla. Wakajifanya kama hawanisikii nilipokuwa nawaongelesha. Mbaya zaidi wakapandisha bei ya viatu ili wanikomoe. Nikaondoka zangu.
Sio hilo tu, hata unapotembelea maeneo ya starehe ndani ya Arusha, kama meza yako ipo jirani na meza ya vijana wenyeji halafu wagundue wewe ni wa Dar, kuna chuki flani unaiona machoni mwao, wanapoteza uchangamfu.
Ni kweli hali ya hewa ya Arusha ni nzuri na mji unapata wageni wengi wa kimataifa wanaokuja kufanya utalii, bado Dar itabaki kuwa juu na bado vijana wa Dar watabaki kuwa na exposure kubwa dhidi yenu.
Karibu kwenye mjadala. Changia kwa lugha ya staha.
Licha ya jiji la Dar kuwa na hali ya hewa ya joto kwa kipindi kirefu cha mwaka, hali ambayo sio rafiki kwa baadhi yetu, Mungu ana kusudi lake kulifanya jiji hili liwe the capital city of Tanzania.
Utake usitake, Dar ni jiji namba moja la kibiashara nchini na Afrika Mashariki likicheza ligi moja na Nairobi, Kampala na Kigali.
Ni jiji ambalo kila mtu kutoka kila kabila lake, anapatikana na kufanya shughuli zake za kiuchumi kwa amani bila kusimangwa au kubugudhiwa na wenyeji ambao ni wazaramo, wandengereko na wakwere.
Niseme tu ukweli, watu wa Pwani licha ya mapungufu yao machache, ni wastaarabu, waungwana na wakarimu sana. wenyeji wa mji huu wamewakaribisha na kuwakarimu wageni wengi waliohamia Dar na kupageuza kuwa makazi yao ya kudumu.
Dar ni jiji la fursa, jiji la kutengeneza network na connection za kutoboa kimaisha kupitia wadau mbalimbali utakao kutananao kwenye mishe zako. Huwa naifananisha Dar na taifa la Marekani kupitia ile concept yao ya chasing the American Dream.
Kama wewe ni kijana uliyeweka malengo ya kufanikiwa kupitia talent mbalimbali hususani uigizaji au mziki, utake usitake lazima utoke mkoani kwenu uje dar ujiweke karibu na big fish wa industry husika.
Mfano mdogo ni wasanii wa Arusha kama Dogo Janja, Joh Makini na wenzake wa kundi la weusi. Hawa wote wamefika hapo walipofika baada ya kuhamia Dar halafu wakashikwa mkono na watoto wa mjini wa jiji hili(sina haja ya kuwataja, jamii inajua).
Laiti kama Arusha ndio ingekuwa the main capital city ya Tanzania kama lilivyo jiji la Dar, basi vijana wa mikoa mingine ambao wangehamia Arusha, wangeishi kwa manyanyaso sana kutoka kwa vijana wazawa wa Arusha. pengine wangefukuzwa warudi makwao na labda tungekuwa tunashuhudia xenophobic incidents kama zile za South Africa.
Nalisema hili kwasababu ya arrogant, rude behaviour and uncivilised culture ya vijana wa Arusha. Hapo kwenye uncivilised culture wote ni mashahidi wa ile tabia yao kuvuta bangi kiholela na kijisifiia kana kwamba ni ufahari.
Pia ile dress code yao ya kuvaa mashati oversize na mabuti makubwa. Nakumbuka huu uvaaji walikuwa wanavaa vijana wa Dar katikati na mwishoni mwa90s. For now this dress code style is out of date.
Mtindo huu wa uvaaji ulichochewa na wasanii wakubwa wa mziki wa rap huko Marekani. Ni miaka ambayo Dr Dre na Snoop Dogg walikuwa wanatamba na ngoma yao ya nuthin' but a "G" thang, the late 2pac akitamba na me against the world.
Jambo lingine ni tabia ya chuki na kujiona superior dhidi ya vijana wenzao wa mikoa mingine specifically wa Dar.
Mimi ni mhanga wa hili, huwa natembelea Arusha mara nyingi tu. Kuna siku niliingia duka moja la kuuza viatu, wale vijana walinipokea vizuri tu. Ila baada ya kusikia kiswahili changu na kugundua natokea Dar, customer care yao ikabadilia ghafla. Wakajifanya kama hawanisikii nilipokuwa nawaongelesha. Mbaya zaidi wakapandisha bei ya viatu ili wanikomoe. Nikaondoka zangu.
Sio hilo tu, hata unapotembelea maeneo ya starehe ndani ya Arusha, kama meza yako ipo jirani na meza ya vijana wenyeji halafu wagundue wewe ni wa Dar, kuna chuki flani unaiona machoni mwao, wanapoteza uchangamfu.
Ni kweli hali ya hewa ya Arusha ni nzuri na mji unapata wageni wengi wa kimataifa wanaokuja kufanya utalii, bado Dar itabaki kuwa juu na bado vijana wa Dar watabaki kuwa na exposure kubwa dhidi yenu.
Karibu kwenye mjadala. Changia kwa lugha ya staha.