Mngurimi
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 819
- 789
Uzi wangu huu ni kwa wale vijana ambao tulipata nafasi ya kusoma hadi level kubwa kidogo. Hapa nazungumzia watu wenye certificate, diploma, bachelor, masters n.k. Kwa mtazamo wako na hali halisi ya maisha hapo ulipo unadhani ni kiongozi gani anaweza kukukufaa na kubadilisha maisha yako?
Mimi ni kijana mpambanaji tena nirudie kusema kuwa mimi ni "Mpambanaji". Maana ya upambanaji ni hali ya kujitoa kufanya kazi yoyote ile regardless ni ya taaluma yako au nje ya taaluma yako. Pamoja na kusoma kidogo hadi nikapata degree ni kwa sababu ya juhudi za wazazi wangu na kidogo juhudi za serikali.
Kwa sasa nipo mtaani bila ajira, nafanya kazi za uvuvi na kusaidia mafundi ujenzi. Serikali haikusema kuwa ukisomeshwa lazima uajiriwe. Watumishi wa serikali wanasema tujiajiri. Mama yangu kama mlezi wangu mkuu aliwahi kuuza ng'ombe wawili kwa thamani ya laki 3 ili nisome. Kibaya zaidi "Mama yangu aliyenipambania hajawahi kula matunda yangu tofauti na pesa kidogo ya boom niliyokuwa nikimtumia sometimes". Moyo wa ujasiri unahitajika katika kufanya maamuzi kwa polling box hiyo Oktoba 28.
Pamoja na juhudi zote nifanyazo katika maisha kitu nilichofanikiwa kumiliki ni uwanja/kiwanja cha kujenga ambacho nacho nilikipata kwa mbinde hadi leo sina hakimiliki yake japo ni kiwanja changu.
Kura yetu tunampa nani?
Mimi ni kijana mpambanaji tena nirudie kusema kuwa mimi ni "Mpambanaji". Maana ya upambanaji ni hali ya kujitoa kufanya kazi yoyote ile regardless ni ya taaluma yako au nje ya taaluma yako. Pamoja na kusoma kidogo hadi nikapata degree ni kwa sababu ya juhudi za wazazi wangu na kidogo juhudi za serikali.
Kwa sasa nipo mtaani bila ajira, nafanya kazi za uvuvi na kusaidia mafundi ujenzi. Serikali haikusema kuwa ukisomeshwa lazima uajiriwe. Watumishi wa serikali wanasema tujiajiri. Mama yangu kama mlezi wangu mkuu aliwahi kuuza ng'ombe wawili kwa thamani ya laki 3 ili nisome. Kibaya zaidi "Mama yangu aliyenipambania hajawahi kula matunda yangu tofauti na pesa kidogo ya boom niliyokuwa nikimtumia sometimes". Moyo wa ujasiri unahitajika katika kufanya maamuzi kwa polling box hiyo Oktoba 28.
Pamoja na juhudi zote nifanyazo katika maisha kitu nilichofanikiwa kumiliki ni uwanja/kiwanja cha kujenga ambacho nacho nilikipata kwa mbinde hadi leo sina hakimiliki yake japo ni kiwanja changu.
Kura yetu tunampa nani?