Vijana tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa Mzee Jakaya Kikwete na Edward Lowassa

I declare interest Mimi ni muumini wa Kikwete na Lowassa, Historia inaeleza kua hawa jamaa walikua marafiki wakubwa sana mpaka lilivokuja suala la Richmond inasemekana ndio lililowavuruga

Lakini pamoja na kugombana mmoja akiwa ni mwenyekiti wa CCM taifa mwingine akiwa mgombea urais wa chama pinzani lakini bado waliheshimiana hawajawahi kutukanana jukwaani ninachokumbuka Mimi kuhusu Lowassa kila akipanda jukwaani alikua anasema rafiki yangu kaharibu nchi wakati Jk alikua akisema mwenye Richmond chadema wanae hakuwahi kumwita Lowassa fisadi.

Natamani tupate mwandishi mmoja afanye interview na hawa jamaa aangalie Historia yao wapi wametoka mangapi wamefanya pamoja je nini kiliwagombanisha na status yao kwa Sasa ipoje, nadhani itakua documentary nzuri mno.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app

Angalia kwa upana zaidi.

Katika huo “ustaarabu” wao katika harakati zao za kisiasa, hawa wawili ni miongoni mwa vinara walioasisi na kuneemesha ufisadi mkuu wa kimfumo ndani ya serikali na CCM yake.

Enzi zao ndipo mikono ya Ikulu ilikuwa ikionekana wazi katika dili kubwa kubwa nchini. CCM iligeuzwa chombo cha wafanyabishara hasa watu kati (middle men/agents of the state) kufanya yao bila bugdha na fursa kadhaa za uongozi wa kisiasa serikalini zikawa kwa ajili ya wawezeshaji, washikaji na michepuko.

Richmond ilikuwa dili yao wote, ila Msoga, aliyekuwa smart zaidi kisiasa, akaona fursa kumuangushia jumba bovu mwenzake akose sifa za kugombea uRais awamu inayofuata. Kama roho mbaya vile.

Hicho kitabu kikiandikwa, itapendeza zaidi kikipewa title ya: “The Classic Partners in Crime”.
 
I declare interest Mimi ni muumini wa Kikwete na Lowassa, Historia inaeleza kua hawa jamaa walikua marafiki wakubwa sana mpaka lilivokuja suala la Richmond inasemekana ndio lililowavuruga

Lakini pamoja na kugombana mmoja akiwa ni mwenyekiti wa CCM taifa mwingine akiwa mgombea urais wa chama pinzani lakini bado waliheshimiana hawajawahi kutukanana jukwaani ninachokumbuka Mimi kuhusu Lowassa kila akipanda jukwaani alikua anasema rafiki yangu kaharibu nchi wakati Jk alikua akisema mwenye Richmond chadema wanae hakuwahi kumwita Lowassa fisadi.

Natamani tupate mwandishi mmoja afanye interview na hawa jamaa aangalie Historia yao wapi wametoka mangapi wamefanya pamoja je nini kiliwagombanisha na status yao kwa Sasa ipoje, nadhani itakua documentary nzuri mno.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Haya yote ni majangili
 
Mkuu Chaliifrancisco , mimi Pasco Mayalla, hata mara moja, sijawahigi kutaka uteuzi wowote, ila humu jf, tuna members wengi wenye viwango tofauti tofauti vya uelewa, wengine ni ma GT, wengine ni watu wa kawaida, wengine ni vilaza, na wengine ni wajinga kabisa, yaani empty shells, hivyo wale ma GT, kiukweli wananielewa vizuri na wana uwezo wa kusoma in between the lines, wakinisoma, wananielewa na huwezi kumsikia GT yoyote akisema Pasco anatafuta uteuzi. Wengi wa wanaodhani natafuta uteuzi ni vilaza tuu na wajinga wajinga.

Mimi ni mjasiriamali, ambaye kwenye kodi yangu pekee, at optimum, inawalipa mishahara ma DC 5, ma RC 3 na Wakurugenzi 2. Ila ni kweli Blaza alipoingia, aliponiita njaa, kusema ukweli kauli nyingine zina nguvu, mambo yangu yaliniendea kombo, ofisi nikahama, nikapunguza wafanyakazi, na kweli njaa ikanitembelea, na Corona ilipoingia, ndio ikanimaliza kila kitu, na hadi sasa mambo yangu bado hayajatengamaa, ila sitafuti uteuzi, sijawahi kutafuta uteuzi na wala sitakuja kutafuta uteuzi, mimi ni masikini jeuri, kama alivyo Kozi mwana mandanda, kulala njaa kupenda.
P
Masikini jeuri? Mwenyewe unathibitisha kuwa hapa Tanzania, huwezi kuwa masikini jeuri.

Wenye dola yao wakiamua hata hako kafremu kako unakopigia vimishe vyako wanaweza kukapiga nyundo kavunjikie mbali hadi ukawapigie magoti.

Btw nini hasa ilikuwa MOTIVE yako kupambania ubunge wa Kawe dhidi ya gwiji Halima akiwemo mshindani “mnajimu” Gwajima?
 
Back
Top Bottom