Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), limesema halitakubali kuona viongozi wa kitaifa wanadhalilishwa na kudhihakiwa na kikundi cha mamluki waliopandikizwa kuharibu mikutano ya katibu mkuu wa chama hicho, Dk. willibrod Slaa.
Limesema italinda kwa nguvu zote mikutano hiyo na kukabiliana na mamluki wanaopandikizwa ili kushawishi polisi kupiga marufuku mikutano ya chadema kwa kuwa ina sura ya vurugu.
Mwenyekiti wa Bavicha taifa, John Heche, alitoa msimamo huo jana, ulioungwa mkono na viongozi wengine na wajumbe wa kamati kuu, katika kongamano la kutafakari miaka 52 ya uhuru na mustakabali wa taifa kimaendeleo.
Huku akishangiliwa na vijana wasomi wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 1000 Heche alisema vijana watailinda Chadema na viongozi wao na kamwe hawatakubali kutishwa kwani yanayojitokeza sasa hayana taswira njema kwa chama bali yanafanywa na waliobainika kuwa wasaliti na kutimuliwa.
Source:Nipashe Jumanne
Limesema italinda kwa nguvu zote mikutano hiyo na kukabiliana na mamluki wanaopandikizwa ili kushawishi polisi kupiga marufuku mikutano ya chadema kwa kuwa ina sura ya vurugu.
Mwenyekiti wa Bavicha taifa, John Heche, alitoa msimamo huo jana, ulioungwa mkono na viongozi wengine na wajumbe wa kamati kuu, katika kongamano la kutafakari miaka 52 ya uhuru na mustakabali wa taifa kimaendeleo.
Huku akishangiliwa na vijana wasomi wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 1000 Heche alisema vijana watailinda Chadema na viongozi wao na kamwe hawatakubali kutishwa kwani yanayojitokeza sasa hayana taswira njema kwa chama bali yanafanywa na waliobainika kuwa wasaliti na kutimuliwa.
Source:Nipashe Jumanne