Vijana tuingie kwenye siasa, hapa Tanzania ni rahisi sana kuongoza wananchi.

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Sep 22, 2016
4,580
7,938
Habari wadau!

Nimetafakari kwa muda kidogo nimegundua njia rahisi ya kufanikiwa katika maisha hapa nchini, ambayo ni kujitosa kwenye siasa.
Hii ni kutokana na asili ya wananchi (waajiri wa wanasiasa ambao ni wananchi wa Tanzania) kuwa wafuata mkumbo, wasiojielewa na wepesi kusahau makonzi waliyopigwa siku za nyuma.
Hivi kitendo cha Watanzania kuishangilia na kuitumainia bajeti iliyosomwa majuzi ni dhahiri kwamba Watanzania wameshasahau kwamba bajeti ya 2016/17 imefail kwa asilimia nyingi, pia wameshindwa kubaini njia zilizoainishwa na waziri wa fedha majuzi kwamba zitatumika kukusanya mapato hazina utofauti na zilizotumika mwaka wa jana ambazo hazikuzaa matunda.
Ajabu zaidi ni kwamba mpaka wasomi nchi hii wageuka kuwa mzigo; haiingii akilini msomi kusifu hatua ya kuondoa ushuru wa kusafirisha mazao yasiyozidi tani moja kwenda halmashauri nyingine, kimsingi hakuna mkulima au mfanyabiashara atakayekubali kuingia hasara ya kukodi gari au kutumia gari yake kusafirisha mbali mzigo usiozidi tani moja(kg. 1000). Tani moja ni kama gunia kumi hivi, nani aunguze gharama za kusafirisha gunia 8 au 9 za mahindi kutoa Morogoro mpaka Dar ili kutafuta soko zuri Dar es salaam huku utofauti wa bei ni elfu 15 kwa kila gunia?
Yaani ngoja tu niishie hapa.
 
Tatizo nchi ina wajinga wengi sana.. Kweli bana, kama mtu anaweza jitosa siasani aende tuu akajitafutie pesa fasta
Nchi imejaa matutusa mengi.
Kuna pimbi majuzi nilimuhoji , akasema anafurahia utumbuaji majipu wa Magufuli. Nikamuuliza ananufaika nini na utumbuaji huu akasema hata asipopata kitu anafurahi tu ili heshima iwepo. Nikamwangalia nikamtoa akili, mkurugenzi anayetumbuliwa hatakuja aishi maisha ya kula mihogo na kulala kama yeye labda apate ukichaa.
 
Siasa inalipa huoni Daud anavyong'ang'ania u-RC hataki kutoka hadi anaenda kulia kanisani.
 
Samahani kama nitakuwa tofauti...

Hili suala la vijana wengi kukimbilia SIASA nchi itajengwa na nani kwa maana vijana ndio tunawategemea kama NGUVU KAZI ya taifa kwenye shughuli mbalimbali za kimaendeleo na miradi ya kijamii...
 
Taifa hujengwa kwa namna nyingi ndugu. Hata ukiwa mbunge ukalipwa mshahara, posho na ukaamua kufungua projects mbalimbali kama vile ufugaji, uvuvi unaweza kuajiri wengi na ukawa umelijenga taifa kwa upana zaidi ya mkulima wa Biharamulo anayeng'ang'ania jembe la mkono.
Samahani kama nitakuwa tofauti...

Hili suala la vijana wengi kukimbilia SIASA nchi itajengwa na nani kwa maana vijana ndio tunawategemea kama NGUVU KAZI ya taifa kwenye shughuli mbalimbali za kimaendeleo na miradi ya kijamii...
 
Taifa hujengwa kwa namna nyingi ndugu. Hata ukiwa mbunge ukalipwa mshahara, posho na ukaamua kufungua projects mbalimbali kama vile ufugaji, uvuvi unaweza kuajiri wengi na ukawa umelijenga taifa kwa upana zaidi ya mkulima wa Biharamulo anayeng'ang'ania jembe la mkono.
sawa hapo kwenye ajira..kundi lipi linategemewa kati ya haya...watoto, vijana au wazee?
 
Back
Top Bottom