Mpwayungu Village
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 14,304
- 29,831
Nipo katika hatua ya mwisho sasa kufanya maamuzi magumu kama hamtaniunga mkono basi nitaandamana peke angu potelea pote.
Ninafadhaika sana kuona nchi yenye maliasili zakutosha lakini tangu uhuru hatuoni mabadiliko yoyote, mada ni zilezile, agenda ni zilezile mpaka tunasikia kichefuchefu yaani mpaka leo tunakimbizana na matundu ya Choo mashuleni, watanzania wanakufa kwa kukosa madawa hospitalini, tunaishi maisha yakutisha mpaka aliyeko kuzimu anatucheka. Nasema hapana liwalo naliwe.
Hapa naongea na vijana, ebu tuangalie yafuatayo halafu tutajiuliza hii serikali inatuchukuliaje
1. Wabunge 19 waliofukuzwa uanachama na kamati kuu ya chadema wapo pale kwa katiba ipi. Naapa kama hamna majibu yenye tija tutaonana wabaya, ivi hizi ni akili au matope. Kama katiba imeeleza kuwa kama mbunge atafukuzwa uanachama naubunge wake utakoma hapo hapo sasa Kuna katiba ipi nyingine ambayo imewaweka hawa watu?
2. Hizi tozo za miamala wananchi wamekataa hali zao ni duni ila nyinyi mnafosi. Wananchi ndowenye maamuzi ya mwisho kama wameona swala la tozo ni maumivu kwao kwann mnafosi? Vyanzo vyamapato vipo vingi nendeni huko acheni tamaa Wananchi sio kwamba wamesahau swala la tozo ipo siku kitalipuka nahuo moto hamtaweza kuuzima.
3. Nisheria ipi mnayotumia kuzuia vyama vya upinzani kufanya mikutano na kuruhusu CCM kufanya mikutano. Kama hamna majibu yakutosha jiandaeni vijana tumechoka kuburuzwa na wazee wenye tamaa zakubaki madarakani milele.
4. Nisheria gani mnayotumia kuzuia maandamano ya Amani yakudai katiba mpya. Katiba mpya nimatakwa ya Wananchi sio mbowe wala chadema nasiyo kila mnayemuona anaandamana basi ni mpinzani lahasha. Kudai katiba mpya ni uzalendo uliopitiliza vijana tuamke tudai haki yetu.
NB. Haki haiombwi haki inapiganiwa vijana tuamke sisi ndowahanga wakila matatizo yenye maumivu makali, ukosefu wa ajira ni sisi, umasikini ni sisi, imefika wakati mpaka tunafedheheshwa na spika wa bunge kuwa hatuna uaminifu nawakati kashifa zote zauwizi wa mabilioni ya escrow epa Richmond kigoda rada ni wao halafu cha ajabu tumekaa kimya. Tupaze sauti zetu tudai haki zetu wasipotupa haki zetu tutajichukulia wenyewe.
Ninafadhaika sana kuona nchi yenye maliasili zakutosha lakini tangu uhuru hatuoni mabadiliko yoyote, mada ni zilezile, agenda ni zilezile mpaka tunasikia kichefuchefu yaani mpaka leo tunakimbizana na matundu ya Choo mashuleni, watanzania wanakufa kwa kukosa madawa hospitalini, tunaishi maisha yakutisha mpaka aliyeko kuzimu anatucheka. Nasema hapana liwalo naliwe.
Hapa naongea na vijana, ebu tuangalie yafuatayo halafu tutajiuliza hii serikali inatuchukuliaje
1. Wabunge 19 waliofukuzwa uanachama na kamati kuu ya chadema wapo pale kwa katiba ipi. Naapa kama hamna majibu yenye tija tutaonana wabaya, ivi hizi ni akili au matope. Kama katiba imeeleza kuwa kama mbunge atafukuzwa uanachama naubunge wake utakoma hapo hapo sasa Kuna katiba ipi nyingine ambayo imewaweka hawa watu?
2. Hizi tozo za miamala wananchi wamekataa hali zao ni duni ila nyinyi mnafosi. Wananchi ndowenye maamuzi ya mwisho kama wameona swala la tozo ni maumivu kwao kwann mnafosi? Vyanzo vyamapato vipo vingi nendeni huko acheni tamaa Wananchi sio kwamba wamesahau swala la tozo ipo siku kitalipuka nahuo moto hamtaweza kuuzima.
3. Nisheria ipi mnayotumia kuzuia vyama vya upinzani kufanya mikutano na kuruhusu CCM kufanya mikutano. Kama hamna majibu yakutosha jiandaeni vijana tumechoka kuburuzwa na wazee wenye tamaa zakubaki madarakani milele.
4. Nisheria gani mnayotumia kuzuia maandamano ya Amani yakudai katiba mpya. Katiba mpya nimatakwa ya Wananchi sio mbowe wala chadema nasiyo kila mnayemuona anaandamana basi ni mpinzani lahasha. Kudai katiba mpya ni uzalendo uliopitiliza vijana tuamke tudai haki yetu.
NB. Haki haiombwi haki inapiganiwa vijana tuamke sisi ndowahanga wakila matatizo yenye maumivu makali, ukosefu wa ajira ni sisi, umasikini ni sisi, imefika wakati mpaka tunafedheheshwa na spika wa bunge kuwa hatuna uaminifu nawakati kashifa zote zauwizi wa mabilioni ya escrow epa Richmond kigoda rada ni wao halafu cha ajabu tumekaa kimya. Tupaze sauti zetu tudai haki zetu wasipotupa haki zetu tutajichukulia wenyewe.