Vijana mtaani maisha magumu sana.Sisi wenye ajira tumeshindwa kuwapunguzia makali ya kimaisha?

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Nafikiria kundi kubwa la watu ambao wako mtaani hawana ajira hasa wale vijana wetu waliotoka vyuoni ,kwa takribani miaka 3 sasa. Wamepiga kelele, wamelia ,wamesononeka, wameandika kwenye mitandao ya kijamii mpaka imefikia mahali sasa wameamua kunyamaza wao wenyewe. Kimya kama hawapo mtaani.

Nimeshuhudia vijana wengi sana ambao ni degree holder, wameanza kulima kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia pump za petrol au diesel, wanafundisha shule private, wanachoma chips, kufyatua matofali nk. Kuna wale wengine ambao wako kwa wazazi, mjomba/shangazi, wifi au shemeji. Huku vyeti vyao vikiwa kwenye bahasha za kaki.

Ukitembelea mabonde mengi ya umwagiliaji, unakutana na degree za Engineering, Sociology, Accounts, nk..vijana wameungana ilimradi mkono uingie kinywani.

Kuna vijana hawaamini kama watakuja kuzitumikia taaluma zao.

Mtaani vijana wanapata shida sana. Kuna kijana nilikutana Mae ameniomba hela ya sabuni na vocha, TZS 2,500. Nikampatia elfu 50. Kijana kapauka sana. Nimemwahidi kufanya nae kazi za projects zangu akiwa anakaa kwangu ili aanze kujijenga na kupata mizizi yake.

Swali ambalo najiuliza, hivi ni kweli wasomi wote chini tumeshindwa kuwabeba vijana wetu mtaani ambao wengi wana vyeti vyao vizuri? Mpaka ajira za serikali jamani?
 
Hali ni mbaya kwetu sote. Tunawaza kesho yetu na ya watoto wetu itakuwaje. Sasa hivi si rahisi kutoa support kwa kila mmoja. Mishahara midogo, biashara zinafungwa kwa kodi kubwa, stahili za wafanyakazi ikiwamo madeni serikali hailipi... tutawasaidiaje. Wazazi nao wanategemea wenye kazi. Hali tete sana
 
Nimeshuhudia vijana wengi sana ambao ni degree holder, wameanza kulima kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia pump za petrol au diesel, wanafundisha shule private, wanachoma chips, kufyatua matofali nk. Kuna wale wengine ambao wako kwa wazazi, mjomba/shangazi, wifi au shemeji. Huku vyeti vyao vikiwa kwenye bahasha za kaki.
?
Hawa ndio mabilionea wa baadaye!...
 
mm nawasaidia kuwapa ushauri wa kujiajiri....japo najua hana hata mia ya capital wala mm siwezi kujiajiri......
 
Wacha wajifunze ili wakati wa uchaguzi wajielewe.wanataka nani na kwanini.
 
Sasa hivi kila mtu anahangaika nyumbani chakula kisikosekane basi.hayo mengine ni anasa.
 
Back
Top Bottom