Kilasi Mkuu
JF-Expert Member
- Nov 25, 2013
- 2,325
- 719
Katika taarifa ya habari Channel ten vijana wamesema wanajiandikisha kwenye daftari la kudumu ili kumuunga mkono Lowassa.
Wanasema wanajua amekatwa lakini wao watashikamana na baba yao Lowassa.
Kwa ujumla wake tukiongezea na mkolezo wa Kingunge japo yeye Lowassa hajasema kitu kwa sasa hali ni tete ndani ya CCM .
Ule umati wa Lowassa ulikuwa mkubwa mno kwa nchi nzima, huwezi kuuzima kwa kumweka tu Magufuli tena kwa kukiuka taratibu.
Mimi naiona hali hiyo kama hali ileile ya muda kuwadia wa kifo cha CCM.
Kiukweli miaka yote CCM hawajawahi kutofautiana kwa kiasi hiki. Maana Kingunge anasema mtu alikuja na majina yake tu na kuyapenyeza kamati kuu.
Naona mtu mwenyewe atakuwa JK tu maana hupenda mambo ya kienyeji kama alivyo kuwa akiendesha Nchi.
Wanasema wanajua amekatwa lakini wao watashikamana na baba yao Lowassa.
Kwa ujumla wake tukiongezea na mkolezo wa Kingunge japo yeye Lowassa hajasema kitu kwa sasa hali ni tete ndani ya CCM .
Ule umati wa Lowassa ulikuwa mkubwa mno kwa nchi nzima, huwezi kuuzima kwa kumweka tu Magufuli tena kwa kukiuka taratibu.
Mimi naiona hali hiyo kama hali ileile ya muda kuwadia wa kifo cha CCM.
Kiukweli miaka yote CCM hawajawahi kutofautiana kwa kiasi hiki. Maana Kingunge anasema mtu alikuja na majina yake tu na kuyapenyeza kamati kuu.
Naona mtu mwenyewe atakuwa JK tu maana hupenda mambo ya kienyeji kama alivyo kuwa akiendesha Nchi.