Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,694
Huyu anasema hatarudia tena huu ujinga!,...Anasimulia....Walipokua wanaishi baba yake alimwomba jirani amfundishe udereva huyu dogo.....Anasema....Nakumbuka jion siku ya tukio alikua ameenda bar kupata moja baridi baada ya mikiki mikiki ya kujifunza kuendesha lori la mchanga huku nae akiwasaidia kazi ile!Wakati anakunywa,dada mmoja alinyanyuka kwenda kuwasha gari lake ili aondoke,mara gari likagoma kuwaka,kijana akanyanyuka kwenda kumsaidia na akafanikiwa,gari likawaka,yule dada akataka kumlipa jamaa akakataa badala yake akaomba namba ya simu,akapewa,dada akamuuliza kama anaishi maeneo yale jamaa akajibu 'hapana mimi huwa nakuja huku kukagua miradi yangu' jamaa baada ya wiki ya mazoea akarusha huku akidai ana miradi mingi.Siku ya 'noma' ikawadia,walipeleka mchanga saiti,wakiwa wanasawazisha mchanga na makoleo huku jamaa amechafuka 'kinoma' mwenye saiti akafika mara akasalimia,kumbe ni yule dada,yule dada alimtazama sana jamaa akataka kusema jambo akaghairi nadhani alifikiri amemfananisha.Dereva ambae ni mwalim wake akaharibu kila kitu alimwita kwa jina akisema"malizia fasta tunadaiwa tripu tano hapa"yule dada alimwambia jamaa"kumbe ni wewe nini kimetokea tena?"jamaa alishindwa kujibu akawa amepigwa butwaa,kisha yule dada akamwambia"tutaongea kwenye simu"jamaa anasema alizima simu wiki nzima.Siku hizi akiulizwa kazi anasema ya kweli!