Bowie
JF-Expert Member
- Sep 17, 2016
- 4,372
- 6,078
Baada ya kufuatilia hotuba nyingi za Vyama vya Upinzani ninapenda kuwasihi vijana kuwa na tahadhari kwa ahadi zisizoweza kutekelezeka.
Nikianzia suala la ajira ni tatizo la sehemu kubwa duniani watu wamepoteza kazi kwa hali mbaya ya kiuchumi pamoja na tatizo la ugonjwa huu wa COVID19 ulipojitokeza.
Suala la kusema kuwa wakishika madaraka wataruhusu wananchi wataruhusiwa kwenda kuishi kwenye hifadhi ni la upotoshaji mkubwa kwani tukiruhusu utekelezaji huo ina maana utalii utakufa.
Ninatoa mfano nchi ya Misri 2011 wananchi walimuondoa madarakani Rais Hussein Mubarak kupitia chama cha Muslim Brotherhood baada ya chama hicho kutoa ahadi nyingi zisizoweza kutekelezeka kufika mwaka 2013 wananchi hao hao waliiingia mitaani kupinga hicho chama matokeo Jeshi la nchi hiyo likatwaa madaraka tena.
Tumeona hapa majirani zetu Kenya baada ya kuiondoa KANU madarakani na kupata katiba mpya leo wakenya wanaikumbuka KANU kwani Ufisadi na ukabila umekuwa mkubwa sana kufikia kuhatarisha umoja wa nchi hiyo. Katika uchaguzi wa mwaka 2007 wananchi kupitia vyama hivyo vilipigana vita vya kikabila na maelfu ya wananchi walipoteza maisha.
Kwa mustakabali wa nchi yetu Tanzania bado CCM ni chama pekee kinachoweza kuipeleka nchi katika uchumi mzuri na umoja wa kitaifa.
Tusijaribu kufanya kosa kubwa la kutoipigia kura CCM na haswa Rais Magufuli ambaye ameleta mageuzi makubwa ndani ya chama hicho na serikali kwa ujumla.
Nikianzia suala la ajira ni tatizo la sehemu kubwa duniani watu wamepoteza kazi kwa hali mbaya ya kiuchumi pamoja na tatizo la ugonjwa huu wa COVID19 ulipojitokeza.
Suala la kusema kuwa wakishika madaraka wataruhusu wananchi wataruhusiwa kwenda kuishi kwenye hifadhi ni la upotoshaji mkubwa kwani tukiruhusu utekelezaji huo ina maana utalii utakufa.
Ninatoa mfano nchi ya Misri 2011 wananchi walimuondoa madarakani Rais Hussein Mubarak kupitia chama cha Muslim Brotherhood baada ya chama hicho kutoa ahadi nyingi zisizoweza kutekelezeka kufika mwaka 2013 wananchi hao hao waliiingia mitaani kupinga hicho chama matokeo Jeshi la nchi hiyo likatwaa madaraka tena.
Tumeona hapa majirani zetu Kenya baada ya kuiondoa KANU madarakani na kupata katiba mpya leo wakenya wanaikumbuka KANU kwani Ufisadi na ukabila umekuwa mkubwa sana kufikia kuhatarisha umoja wa nchi hiyo. Katika uchaguzi wa mwaka 2007 wananchi kupitia vyama hivyo vilipigana vita vya kikabila na maelfu ya wananchi walipoteza maisha.
Kwa mustakabali wa nchi yetu Tanzania bado CCM ni chama pekee kinachoweza kuipeleka nchi katika uchumi mzuri na umoja wa kitaifa.
Tusijaribu kufanya kosa kubwa la kutoipigia kura CCM na haswa Rais Magufuli ambaye ameleta mageuzi makubwa ndani ya chama hicho na serikali kwa ujumla.