Vijana kutoka kimaisha kwenye Utawala wa Awamu ya 5 ni ndoto za mchana

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,320
Hua nasema kila siku, CCM hata wakipewa miaka 700 hakuna kitu watatufanyia watanzania zaidi ya kutufukarisha. Miaka na miaka CCM inazalisha mafukara wa kutupwa wanaoitwa wanyonge ambao mbaya zaidi ccm inawatumia tena kama stepping stone kwenye uchaguzi.

Kijana wa Kitanzania kutegemea utatoka kwenye serikali hii ya Awamu ya 5 ya wanyonge ni ndoto za mchana.

1. Miaka 5 hakuna ajira na wala hakuna mkakati wa kuondoa tatizo la ajira, ccm watakuja na jibu jepesi tu kua tatizo la ajira ni la kidunia. Waliomaliza vyuo toka mwaka 2015 99% hawana ajira ya kueleweka, na bado serikali wala haina mkakati mahsusi kupunguza hili tatizo.

2. Ukitegemea biashara, biashara hazieleweki, hazifanyiki, ukipata mtaji wako unaisha kabla hujaanza biashara, mara osha, tra, ushuru halmashauri, tfda, serikali za mtaa, bwana afya, kote huko unatakiwa kulipa kabla ya kuanza kufanya biashara. Gharama za hizo leseni mtaji umekata kabla hujaanza biashara.

3. Ukipata pesa yako ujenge kibanda simenti mfuko 25,000 hadi 35,000, gharama za ujenzi ziko juu sana, nondo, mabati, vigae, mbao bei ghali kama vile tunaagiza kutoka Malaysia. CCM watakupa majibu mepesi kua miradi ya maendeleo ndio umepandisha bei simenti, hawana mikakati endelevu kama ilivyo kawaida yao. Hapa kijana usitegemee utatoboa.

4. Huwezi kununua gari, kodi za magari ni mara 2 ya bei ya gari, ccm bado wanaamini gari ni anasa na sio basic need. Karne ya 21 bado ccm wanaamini gari ni luxury goods hivyo iwe highly taxed, bado wana mawazo ya karne ya 19. Hapa kijana usitegemee utatoka. Ukijikongoja sana utaishia kununua kimkweche cha mwaka 2003 ama 2004, 16 years old car.

5. Mitaji haipatikani, ukisema ukakope benki riba juu sana, 20%-24% na biashara hazitabiriki hivyo utaishia kufilisika tu. Hawana mkakati wowote kufanya benki zishushe riba.

Kijana kama unategemea utatoka chini ya serikali ya ccm unaota ndoto za mchana. Ndio maana pamoja na ccm kutawala miaka 60, 80% ya watanzania ni mafukara wa kutupwa. Juzi waziri Mpango amakiri kua pamoja na kua tuko uchumi wa kati ila umasikini ni mkubwa sana.

Hii mada inaendelea.
 
Mtoa mada nakuunga mkono. Vijana wanatakiwa wafanye utaratibu wa kusepa nchini. Kwa hali ilivyo ni nafuu kutafuta maisha ughaibuni wangali bado wana nguvu. Tanzania vijana wanajituma sana lakini matokeo ni hakuna. Ni wakati wa kuamka
 
Utasikia wanasema "vijana jiajirini msisubiri kuajiriwa". Ukienda kwenye financial institutions upate loan wanataka collateral wakati assets ninayomiliki ni degree yangu tu na wanasema haiwezi kutumika kama collateral. Nina simu nayo sio asset ni liability maana inanila hela ya vocha kila siku.

Simply ni upuuzi mtupu.
 
KAZI YA SERIKALI SIO KUWAPA WATU KAZI NI KUTENGENEZA MAZINGIRA MAZURI YA WANANCHI WAKE WATENGENEZE KAZI ILI KUJIAJIRI SASA HAYO MAZINGIRA YENYEWE NDO SHESHE TRA AKIJA KUKUKADIRIA KODI WANAPITILIZA HADI MTAJI
 
Mtoa mada nakuunga mkono. Vijana wanatakiwa wafanye utaratibu wa kusepa nchini. Kwa hali ilivyo ni nafuu kutafuta maisha ughaibuni wangali bado wana nguvu. Tanzania vijana wanajituma sana lakini matokeo ni hakuna. Ni wakati wa kuamka
Watanzania hawana munkari sana wa kusepa ughaibuni kama ilivyo kwa wakenya hivyo wana watu wachache sana waliokwisha tangulia kwa ajili ya kuwafanyia michakato.
 
Kama Kijana Ni Wajibu Wangu Kutoa MAPENDEKEZO bora ya nini kifanyike kuliko KULAUMU TU.

Sina maana ya WANAOLAUMU na KUKOSOA wanakosea....hasha lillah!!

Nchi ni yetu SOTE na KUIJENGA ni wajibu wa kila MMOJAWETU.

Katika kunusuru janga la UNEMPLOYMENT(kukosa ajira) haya ni bora TUKAYACHUKUA KIVITENDO;

1.FISCAL POLICY:
Kwa ufupi,mwaka wa fedha wa serikali ni bora ukapunguza sana KODI(TAXES) kwa BIDHAA zetu zote ili kuinua MANUNUZI KWA UPANA WAKE(aggregate demand).

Na unapopanua WIGO wa MANUNUZI basi tarajia GDP itaongezeka...hapa wala hakuna ELIMU YA UCHAWI ya kaka MNDENGEREKO Kitoabu, Mshana Jr. AMA ubishi "chronic" wa GODZILLA🤣🤣.

Muuza Al Kasus.
Tandale Mtogole

MAENDELEO HAYANA VYAMA.
 
TRA wanawaza kudai kodi kubwa kuliko mauzo
Unaanza kulipa kodi kabla hujaanza biashara, kodi inaitwa kodi ya mapato ila unatakiwa ulipe kabla hujaanza kuzalisha mapato, vituko. Hii iko Tanzania tu.

Unashangaa itafika wakati wafanyakazi wataambisa walipe kodi ya mshahara kabla ya kupokea mshahara.
 
Back
Top Bottom