Vigogo wachunguzwa ufisadi wa Sh86 bilioni IPTL

Patriote

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
1,718
1,047
SERIKALI inawachunguza baadhi ya maofisa wake waandamizi kwa tuhuma za wizi wa dola50 milioni za Marekani sawa na Sh86 bilioni, zilizotengwa kwa ajili ya ununuzi wa mafuta mazito ya kuzalishia umeme kwa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), katika kipindi hiki nchi inapokabiliana na tatizo la uhaba wa nishati hiyo.

IPTL inayozalisha megawati 100 za umeme iliingia mkataba na Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco), lakini utendaji wake umekuwa na mkanganyiko.Chanzo kutoka serikalini kililiambia gazeti dada la The East African la Februari 12, kwamba kuna ushahidi wa kutosha kwamba baadhi ya maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Hazina na Tanesco, wanahusika katika mpango huo wa wizi.

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alipoulizwa alijibu, “Ndiyo naweza kuthibitisha upo uchunguzi unaoendelea, lakini ndiyo kwanza upo katika hatua za awali.” Tayari taarifa za awali za ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), zinaonyesha kumekuwa na maelezo yaliyokiuka utaratibu wa fedha zilizolipwa na Serikali kwa ajili ya usambazaji wa mafuta mazito kutoka kampuni za ndani.

Ukosefu wa nishati ya umeme unaoikabili nchi kwa sasa unaifanya Tanesco kulipa IPTL dola12 milioni za Marekani sawa na Sh19.2 bilioni kila mwezi, kwa uzalishaji wa megawati 60 badala ya megawati 100.

Mwaka 1995, Tanesco iliingia mkataba na IPTL, mkataba ambao uliihusisha kampuni ya nchini Malaysia , Mechmar Corporation na wawekezaji wa ndani, na VIP Engineering and Marketing Company kwa ajili ya kuzalisha megawati 100 kwa kutumia mitambo inayotumia dizeli kwa miaka 20.Katika mkataba huo, VIP ina hisa ya asilimia 30 na ile ya Mechmar ya Malaysia ikiwa na hisa ya asilimia 70.Serikali ilikubali kulipa kwa ajili ya uzalishaji huo kwa kuwa haikuwa na njia nyingine.

Mpango wa kuifilisi IPTLTayari hivi karibuni Mahakama iliamua IPTL ifiilisiwe na jukumu hilo lilikabidhiwa kwa Wakala wa Ufilisi, Vizazi na Vifo (Rita).Hata hivyo, baadhi ya benki zinazoidai IPTL ziliweka zuio mahakamani zikitaka kwanza kulipwa fedha zao ambazo kampuni hiyo ilikopa.IPTL inakadiriwa kuwa na Sh200 bilioni zilizopo Benki Kuu (BoT) ambazo kama ikifilisiwa zingeangukia mikononi mwa Serikali. Kampuni hiyo imekuwa ikiitafuna Tanesco mabilioni ya shilingi tangu kuingia mkataba huo ambao umekuwa ukitajwa kama wa kifisadi, kuliko hata wa Richmond. Ends

Hivi huu ufisadi utaisha lini nchi hii jamani??na hao wanatuibia wanaishi wapi??mbona hatujawahi wakamata??mimi nadhani kuna haja ya kuhoji huu uvumilivu wetu mana nahisi tumerogwa, nini tufanye kukabiliana na UFISADI??
 
huyu jamaa aitwaye tanzania ameliwa sana hadi amebakia mifupa tuuu,na hata mifupa nayo inatafutwa kwa mbinde..... duh!Mungu atunusuru watz na hao mafisadi mafisi
 
Ni vizuri sana kuwa awamu hii ya Kikwete tunasikia watu wakifilisiwa, kupelekwa mahakamani, kuchunguzwa na wengine kufungwa kwa tuhuma mbali mbali za kuharibu, kuiba, rushwa za Serikalini, awamu za nyuma ukisikia kesi moja ya namna hiyo ujuwe hapo imebidi tu. Hongera JMK.

Mtu akishtakiwa maana yake IMEBIDI ashtakiwe. Serikali yeyote worth it's salt inatakiwa kuwa makini na kuchukua hatua zinazostahili kuhakikisha watuhumiwa wa uhalifu wa aina yeyote wanafikishwa mbele ya sheria.
Naelewa upo kazini kwa hivyo ni wajibu wako kuleta "sread" kama hii. lakini hebu tufafanulie: kama serikali hii iko makini kama unavyojitahidi kutuaminisha iweje wahusika wa tuhuma zenye ushahidi hawapelekwi mahakamani? Hapa naongelea kwa uchache Kagoda, Meremeta na ununuzi wa rada (achilia mbali IPTL ambayo huyo uliemsifia alishiriki kwa kiwango kikubwa kufanikisha mkataba wake akiwa waziri wa nishati na madini).
 
huyu jamaa aitwaye tanzania ameliwa sana hadi amebakia mifupa tuuu,na hata mifupa nayo inatafutwa kwa mbinde..... duh!Mungu atunusuru watz na hao mafisadi mafisi

Ni kama gari bovu lilowekwa juu ya mawe! Karibu itashindikana hata kulifufua. Sijui litatupwa wapi!
 
Ni vizuri sana kuwa awamu hii ya Kikwete tunasikia watu wakifilisiwa, kupelekwa mahakamani, kuchunguzwa na wengine kufungwa kwa tuhuma mbali mbali za kuharibu, kuiba, rushwa za Serikalini, awamu za nyuma ukisikia kesi moja ya namna hiyo ujuwe hapo imebidi tu. Hongera JMK.


Hebu tutajie waliofungwa.
Pia unajua hii nchi imeshafilisika?https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/220818-government-in-cash-crisis-says-kikwete.html
Kukumbuka neti wakati mbu wameshakutafuna na asubuhi imefika ni ujanja?
 
Waziri mwenyedhamana,wizara na serikali iliyo madarakani ni mzigo kwa watanzania, mpaka nathubutu kusema ccm na serikali yake ni janga la kitaifa. Nchi imekuwa shamba la bibi, watu wanachuma, no one to sentenced. Days are numbered. God bless revolutionalists.
 
SERIKALI inawachunguza baadhi ya maofisa wake waandamizi kwa tuhuma za wizi wa dola50 milioni za Marekani sawa na Sh86 bilioni, zilizotengwa kwa ajili ya ununuzi wa mafuta mazito ya kuzalishia umeme kwa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), katika kipindi hiki nchi inapokabiliana na tatizo la uhaba wa nishati hiyo.

IPTL inayozalisha megawati 100 za umeme iliingia mkataba na Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco), lakini utendaji wake umekuwa na mkanganyiko.Chanzo kutoka serikalini kililiambia gazeti dada la The East African la Februari 12, kwamba kuna ushahidi wa kutosha kwamba baadhi ya maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Hazina na Tanesco, wanahusika katika mpango huo wa wizi.

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alipoulizwa alijibu, “Ndiyo naweza kuthibitisha upo uchunguzi unaoendelea, lakini ndiyo kwanza upo katika hatua za awali.” Tayari taarifa za awali za ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), zinaonyesha kumekuwa na maelezo yaliyokiuka utaratibu wa fedha zilizolipwa na Serikali kwa ajili ya usambazaji wa mafuta mazito kutoka kampuni za ndani.

Ukosefu wa nishati ya umeme unaoikabili nchi kwa sasa unaifanya Tanesco kulipa IPTL dola12 milioni za Marekani sawa na Sh19.2 bilioni kila mwezi, kwa uzalishaji wa megawati 60 badala ya megawati 100.

Mwaka 1995, Tanesco iliingia mkataba na IPTL, mkataba ambao uliihusisha kampuni ya nchini Malaysia , Mechmar Corporation na wawekezaji wa ndani, na VIP Engineering and Marketing Company kwa ajili ya kuzalisha megawati 100 kwa kutumia mitambo inayotumia dizeli kwa miaka 20.Katika mkataba huo, VIP ina hisa ya asilimia 30 na ile ya Mechmar ya Malaysia ikiwa na hisa ya asilimia 70.Serikali ilikubali kulipa kwa ajili ya uzalishaji huo kwa kuwa haikuwa na njia nyingine.

Mpango wa kuifilisi IPTLTayari hivi karibuni Mahakama iliamua IPTL ifiilisiwe na jukumu hilo lilikabidhiwa kwa Wakala wa Ufilisi, Vizazi na Vifo (Rita).Hata hivyo, baadhi ya benki zinazoidai IPTL ziliweka zuio mahakamani zikitaka kwanza kulipwa fedha zao ambazo kampuni hiyo ilikopa.IPTL inakadiriwa kuwa na Sh200 bilioni zilizopo Benki Kuu (BoT) ambazo kama ikifilisiwa zingeangukia mikononi mwa Serikali. Kampuni hiyo imekuwa ikiitafuna Tanesco mabilioni ya shilingi tangu kuingia mkataba huo ambao umekuwa ukitajwa kama wa kifisadi, kuliko hata wa Richmond. Ends

Hivi huu ufisadi utaisha lini nchi hii jamani??na hao wanatuibia wanaishi wapi??mbona hatujawahi wakamata??mimi nadhani kuna haja ya kuhoji huu uvumilivu wetu mana nahisi tumerogwa, nini tufanye kukabiliana na UFISADI??

Nashukuru kw tarifa yako pia naomba kukumbusha kua waheshimiwa.zitto,j makamba, mnyika waliwahi kuiyomba wizara husika kufanya uchunguzi iptl na tuliletewa hapa.mleta mada hiyo alikua na lengo lakupotosha kua kwakua umeme unapatikana hapakua na haja yakuhoji matumizi yake.leo tumemeona matokeo yaliyopatikana.naomba kuchukua nafasi hii kuwapongeza waheshimiwa hao pamoja na mleta mada hii
 
Ni vizuri sana kuwa awamu hii ya Kikwete tunasikia watu wakifilisiwa, kupelekwa mahakamani, kuchunguzwa na wengine kufungwa kwa tuhuma mbali mbali za kuharibu, kuiba, rushwa za Serikalini, awamu za nyuma ukisikia kesi moja ya namna hiyo ujuwe hapo imebidi tu. Hongera JMK.

Hivi huyu FF ameolewa ? Nina mashaka sana kama kuna mwanamme anaweza kuona na kuishi na huyu mwanadamu. Lazima atakuwa ameolewa na Magamba, maana lazima apinge any comment ambayo inaonekana constructive ambayo inakosoa serikali au Magamba. Kuwa +ve sometime sio lazima upinge kila hoja. Sio lazima uchafue hali ya hewa hata kwenye hoja za msingi.
 
Days are numbered. God bless revolutionalists.
songht2.jpg
songgd.jpg

songjh.jpg
 
Ni vizuri sana kuwa awamu hii ya Kikwete tunasikia watu wakifilisiwa, kupelekwa mahakamani, kuchunguzwa na wengine kufungwa kwa tuhuma mbali mbali za kuharibu, kuiba, rushwa za Serikalini, awamu za nyuma ukisikia kesi moja ya namna hiyo ujuwe hapo imebidi tu. Hongera JMK.

FF,

Inaelekea kuwa wewe ni Binti dogo sana ila huo ushungi na sura ya kumaa inawafanya watu wafikiri kaumri kamepanda kidogo. Kwa taarifa zako awamu zilizopita tumeshuhudia watu wakijiuzulu, kupelekwa mahakamani na kufungwa.

Sasa hii ya kuja kutoa pongezi kwa baba mkwe wakati hatujaona kigogo yeyote akipelekwa Ukonga zaidi ya kutufanyia mazingaombwe pale Kisutu, tunashindwa kukuelewa. Hao dagaa waliopelekwa Ukonga tumesikia wakiwasiliana na Rais kwa simu za mkononi tokea huko huko gerezani. Sasa kweli unataka tuamini kuna kazi inaendelea hapo??
 
Sikuianzisha mimi hiyo, soma post #1 utajuwa ni nani aliyeianzisha.

Hizo zoooote pumba ambazo Kikwete ndio amezishghulikia, ni madudu yaliyofanywa wakati wa Mkapa, au na hilo hulijui?

I was making reference on YOUR OWN RESPONSE, japo kama kawaida yenu umeamua kujifanya hujui ninachokisema. IPTL ni mradi ulioanzishwa wakati kiwete, oops sorry kikwete akiwa waziri wa madini na nishati. Nakubaliana na wewe kuwa Mkapa alifanya madudu mengi tu lakini kati ya hayo la kumteua kikwete kuwa waziri wa madini na nishati hakulifanya.
 
IPTL  Alli hassan mwinyi, jakaya kikwete, and co.
Hao wala watu walituletea janga lililo kazini kwa karibu miaka ishirini sasa, na hata baada ya mkataba huo kuisha madhara yake yataendelea kwa miaka na miaka... Walaaniwe wezi wote.
 
Back
Top Bottom