Vigogo wa serikali waingilia kati sakata la mauji south beach

mwanaone

JF-Expert Member
Apr 2, 2011
637
760
Mauaji ya South Beach yazua utata


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 20 April 2011



MAZINGIRA yanatengenezwa kwa watuhumiwa wa mauaji ya mkazi wa Kigamboni jijini Dar es Salaam , Lillah Hussein (25) kuachiwa huru, MwanaHALISI limeelezwa.

Lillah alifariki dunia Jumamosi usiku akiwa amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), baada ya kupata majeraha ya moto baada ya kumwagiwa petroli huku akiwa amevikwa tairi shingoni.

Tukio hilo lilitokea kwenye hoteli ya South Beach, Kigamboni, Dar es Salaam ambako mhanga huyo alifika kwa ajili ya kupata burudani ya muziki. Inadaiwa alitaka kuingia ukumbini bila ya kulipa kiingilio.

MwanaHALISI limeelezwa kuwa mara baada ya tukio hilo la kuchomwa moto, watendaji wawili waliohusishwa na tukio hilo , walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi Mjimwema, Kigamboni.

Taarifa zinasema walifikishwa mahakamani juzi Jumatatu, kwa mashitaka mawili tofauti yasiyokuwa ya mauaji kama alivyoahidi Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, ACP David Misime.

Pia, meneja wa hoteli hiyo, Salum Nassoro na mtuhumiwa mwingine katika kesi hiyo, nao wamekamatwa tayari na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote wiki hii.

Kwa mujibu wa hati ya Mahakama ya Wilaya ya Temeke ambayo gazeti hili limefanikiwa kuiona, watuhumiwa hao wawili; John Ambumbulwisye na Salum Nathoo Chipata, walifunguliwa kesi kwa mashitaka tofauti ya kushambulia na kujeruhi.

“Haiwezekani watu wamwagie mtu mafuta ya petroli na kumfunga tairi halafu useme walitaka kujeruhi. Hawa walitaka kuua na mashitaka yao ilibidi yaseme kutaka kuua na si kujeruhi,” alisema Laetitia Petro, mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).

LHRC imechunguza tukio hilo tangu lilipotokea 10 Aprili 2011 na kubaini kasoro nyingi katika namna lilivyoshughulikiwa na vyombo vya dola.

Kwa mfano, Laetitia alieleza juzi Jumatatu kuwa watuhumiwa hao wa mauaji walipewa dhamana na mahakama hiyo kwa kutumia hati isiyokuwa na nguvu yoyote kwenye misingi ya kisheria.

Nakala ya hati hiyo haina jina la mahakama iliyoitoa, namba ya kesi husika wala mwaka. Pia haina muhuri wa mahakama, mambo ambayo LHRC inaona yanalenga kupoteza mwelekeo wa kesi.

Katika tukio hilo, Lillah ambaye wakazi wa Kigamboni wanadai hakuwa mwizi, alikamatwa na kuchomwa moto kabla ya kuokolewa baada ya mwenyewe kwenda kujitupa baharini kuokoa maisha yake.

Lillah aliyekuwa mfanyabiashara maarufu wa nguo za kuogelea na vitu vya kitamaduni kwenye fukwe za bahari eneo la Kigamboni, aliharibiwa katika sehemu za siri, mwilini na kichwani.

Alikumbwa na mkasa huo baada ya kukutwa ukumbini bila ya tiketi maalum inayovaliwa mkononi na wale wanaoingia ndani kupata burudani.

Baada ya kukamatwa, alipigwa kabla ya kupelekwa kwa Chipata anayetajwa kuamuru Lillah achomwe.

LHRC inaamini kuwa kuna ushahidi unaoonesha kuwa baadhi ya walinzi wa hoteli hiyo walikuwa wakimfahamu Lillah na hawakutaka achomwe moto na ndiyo waliotoa taarifa kwa wananchi kuwa anachomwa.

Tukio la kuchomwa moto kwa Lillah lilichafua amani maeneo ya Kigamboni, kiasi kwamba wananchi walifikia hatua ya kutaka kuichoma moto hoteli hiyo yenye utata mkubwa.

Kuna madai kuwa wakazi wengi hawafurahishwi na kuwepo kwa hoteli hiyo iliyojengwa baada ya kubomolewa makaburi ya wenyeji bila ya kulipwa fidia.

Inadaiwa kuwa hoteli hiyo imekuwa ikipiga muziki mfululizo nyakati za usiku; ikiwamo mara baada ya tukio la kuchomwa moto kwa Lillah, jambo lililopandisha hasira za wananchi wa Kigamboni ambao wameumizwa na ukatili uliofanyika kwa mwenzao huyo.

Wakati tukienda mitamboni, MwanaHALISI liliarifiwa kuwa baadhi ya viongozi waandamizi serikalini walikuwa wanajitahidi kutaka kuhakikisha wahusika hawashitakiwi kwa kosa zito kwa kuwa ni wawekezaji na huenda kushitakiwa kwao kukachafua shughuli za uwekezaji.

Mmoja wa maofisa wa jeshi la polisi ambao wanalifahamu sakata hilo kwa undani amelithibitishia gazeti hili kuwa kuna baadhi ya vigogo ndani ya serikali na polisi wanajaribu kuzuia haki kutendeka.

Kwa sasa, kesi hiyo iko katika Mahakama ya Wilaya Temeke ambayo kisheria haina uwezo wa kusikiliza kesi ya mauaji zaidi tu ya kufanya uchunguzi wa awali.

Lakini, kitendo cha mtuhumiwa mmoja kufunguliwa mashitaka ya shambulio na mwingine kujeruhi, na kwa kupewa dhamana haraka kinyume na maombi ya polisi, kimezidisha hofu kwa watetezi wa haki za binadamu kuwa huenda kuna jitihada za kuzuia haki kutendeka.
 

Mtanzania anachomwa moto, Serikali haichukui hatua kali kuhakikisha kwamba sheria zinachukua mkondo wake.! Hii Serikali ya Kikwete na CCM wathubutu hata kuwaachia huru watuhumiwa wa mauaji siku chache tu baada ya tukio!! Hii ndiyo Serikali ya CCM inayosema inatetea maisha ya watanzania ??

Ufisadi umekuwa mkubwa mno siyo tu kwa CCM bali pia kwa serikali inayoundwa na CCM kiasi kwamba maisha ya watanzania hayana thamani kama pesa wanazohongwa nazo !
 
Hapana. Serikali ya Kikwete inatetea wale wanaoitwa wawekezaji hata kama hawana chochote cha kuwekeza ila kuchota tu. Uwekezaji chini ya Kikwete umekuwa kama ni umungu mtu, kitu cha kusujudiwa. Sitashangaa kabisa kama kesi hii itaisha kimya kimya tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hapa Kova possibly atakuwa kapata new financial sources za kujenga au kumalizia Mansion yake au kuongeza mitaji kwenye biashara zake.

Rahma Al-Kharoosi adhamini Kamanda Kova Cup.

_MG_9778.JPG
 
OK mtasema , CCM CCM Kila kitu CCM ubadhilifu uoneaji nakula kibaya, haya sasa hao CHADEMA wako wapi ,si ndio watenda Mema na ndio Mkombozi wa Taifa hili ,hahahahaha, ngoma ile ile wafrica wote tuko hivyo hivyo , hakuna cha Chadema wala CCM MDundo ule ule. kila mmoja wao ame IGNORE hii ishu .
 
huu ujinga wa serikali utaisha lini! Haya hivi hapo raia wakiamua kuwaua hao wapuuzi waliopewa dhamana kwa kesi ya mauaji mtawalaumu? Wakati mwingine huwa naona majaji na mahakimu ni maadui wakubwa kwa jamii ya tz na hata wanasheria ni washenz sana hawana uzalendo wanajali pesa tu. Pumbavu zao
 
Very sad, serikali inatetea wahalifu wa kigeni na kuwanyima haki raia wake. Kweli Tanzania ni nchi pekee ambayo haki inauzwa kwa bei rahisi sana. Wawekezaji wanafanya walitakalo kwa kuwa serikali yetu imewekwa mfukoni mwao.
 
OK mtasema , CCM CCM Kila kitu CCM ubadhilifu uoneaji nakula kibaya, haya sasa hao CHADEMA wako wapi ,si ndio watenda Mema na ndio Mkombozi wa Taifa hili ,hahahahaha, ngoma ile ile wafrica wote tuko hivyo hivyo , hakuna cha Chadema wala CCM MDundo ule ule. kila mmoja wao ame IGNORE hii ishu .
Sasa chadema wafanye nini? Kwan wao ndo wenye serikali? Inayoongoza polisi na mahakama? Viongozi wa serikali ya ccm ndo hao wanchumia tumbo kwa kututelekeza wananchi since ni issue ya mtu mmoja huwezi sema eti chadema wavalie njuga waandae maandamano la! Ila chadema inapinga kwa ujumla unyanyasaji wa raia ndani ya nchi yao na haki ya kuishi. Acha ushabiki na umaandazi ccm inahusika moja kwa moja na kutaka haki ipindishwe inahusika coz wanachama na viongozi wake kwa ajili ya njaa njaa zao wanawakumbatia wezi na mafisadi kwa kuwapa jina la wawekezaji
 
Mimi sielewi hawa ndugu zetu wa sheria kama wanafanya kazi zao vizuri maana wapo kimaslahi zaidi.
 
Chomeni moto hiyo hotel. Hawa jamaa wanatudharau sana. Purely apartheid. Wawekezaji (manyang'au) pamoja na serikali wanatufanya kama MBWEHA. Rip ndugu yangu
 
OK mtasema , CCM CCM Kila kitu CCM ubadhilifu uoneaji nakula kibaya, haya sasa hao CHADEMA wako wapi ,si ndio watenda Mema na ndio Mkombozi wa Taifa hili ,hahahahaha, ngoma ile ile wafrica wote tuko hivyo hivyo , hakuna cha Chadema wala CCM MDundo ule ule. kila mmoja wao ame IGNORE hii ishu .

we ni mtoto wa kiume mpuuzi! Aliyekufa ni raia haijalishi kabila lake,dini yake wala chama cha siasa! Apa hatuitaji ucdm wenu wala uccm,hapa kinadaiwa haki. Msizozee kuchangia kila kitu kisiasa na kimzaha kama wapuuzi. Juzi tu,mhindi kamkata kata raia na kumweka kwenye begi na kwenda kumtupa J mall pale,sasa uyu anamchoma moto raia mpaka anakufa,huu ni uwekezaji au uuaji? Ni mambo ya ajabu kuleta siasa hapa,inatakiwa haki itendeke hapa! Hatutakubali tuendelee kuuawa na wale wanaojiita wakishua!hapana!
 
bado inabaki kwa WANANCHI na Wateja kushughulikia suala la South Beach. Nafasi ipo, labda hakuna utashi tu.
 
hao wanaitwa wadekezwaji na si wawekezaji. LHRC isimamie haki si tu itendeke, bali ionekane kutendeka. isije ikawa kama ile issue ya ndugu wawili waliouwawa na wahindi waliokuwa wakitetewa na lamwai, baadaye serikali ikafuta mashtaka!!!!!
 
Jamani jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Suala hili linafuatiliwa kwa karibu sana na Serikali na Mbunge. Hata jana Afande Kova na Mbunge wa Kigamboni walikuwepo Mjimwema wakiongea na wakazi wa kule kuhusu sakata hili. Haki itatendeka na uwekezaji mzima kuangaliwa upya.
 
Jamani hapa ni wana kigamboni kufanya mipango yao chini kwa chini kisha wakipata ukweli Hoteli ifungwe. kwani pasipo na haki vitendo hulipa. Inakuwaje mtu anauawa halafu askari wanamlinda muuwaji?! Kwa kuwa inakuwa hivyo kila mtu awe na pesa yake ya kuhonga kila mara. Lakini kosa lilianzia pale muuwaji wa dereva wa daladala alipoachiwa kwa dhamana na wanasheria wakanyamaza kimya, huku wakisifu kuwa Ikulu haiingilii uhuru wa mahakama.
 
OK mtasema , CCM CCM Kila kitu CCM ubadhilifu uoneaji nakula kibaya, haya sasa hao CHADEMA wako wapi ,si ndio watenda Mema na ndio Mkombozi wa Taifa hili ,hahahahaha, ngoma ile ile wafrica wote tuko hivyo hivyo , hakuna cha Chadema wala CCM MDundo ule ule. kila mmoja wao ame IGNORE hii ishu .

what do you smoke?
 
OK mtasema , CCM CCM Kila kitu CCM ubadhilifu uoneaji nakula kibaya, haya sasa hao CHADEMA wako wapi ,si ndio watenda Mema na ndio Mkombozi wa Taifa hili ,hahahahaha, ngoma ile ile wafrica wote tuko hivyo hivyo , hakuna cha Chadema wala CCM MDundo ule ule. kila mmoja wao ame IGNORE hii ishu .

Someone has lost his life mercylessly and that is all u can say. What a shame!!
 
ni kuichoma hotel moto and thats it. mambo ya mahakama noana waachane nayo at this stage!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom