Pope
Senior Member
- Dec 3, 2007
- 117
- 0
HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) imewaachisha uongozi rasmi viongozi wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ambao ni Mwenyekiti Abiud Maregesi, makamu wake Ramadhan Nzori na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu, Cosmas Hinju. Maregesi ameachishwa uongozi kutokana na ubadhirifu wa fedha za jumuiya hiyo Sh milioni 63.3 na kutumia vibaya madaraka yake.
Nzori ameachishwa kazi kutokana na kosa la ubadhirifu wa Sh milioni 7.5, wakati Hinju anatuhumiwa kutafuna Sh milioni tano na matumizi mabaya ya madaraka. NEC imeagiza kuwa viongozi hao wa wazazi warejeshe fedha za jumuiya hiyo walizochukua kinyume cha kanuni za fedha za jumuiya hiyo. Halmashauri Kuu pia imemteua Badru Bushako kuwa Kaimu Katibu Mkuu.
Nzori ameachishwa kazi kutokana na kosa la ubadhirifu wa Sh milioni 7.5, wakati Hinju anatuhumiwa kutafuna Sh milioni tano na matumizi mabaya ya madaraka. NEC imeagiza kuwa viongozi hao wa wazazi warejeshe fedha za jumuiya hiyo walizochukua kinyume cha kanuni za fedha za jumuiya hiyo. Halmashauri Kuu pia imemteua Badru Bushako kuwa Kaimu Katibu Mkuu.