Vigogo TUCTA akiwemo Nicholaus Mgaya, wabwagwa

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Nicholaus Mgaya, ameshindwa kutetea kiti chake baada ya kugaragazwa na Dk Yahaya Msigwa katika uchaguzi uliofanyika na kumalizika usiku wa manane kuamkia jana.

Dk Msigwa anatoka katika Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE).

Kiongozi pekee aliyefanikiwa kutetea nafasi yake katika uchaguzi huo wa jana ni Mweka Hazina wa shirikisho hilo James Kalanje.

Akitangaza matokeo hayo jana asubuhi, Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Uchaguzi huo, Dk Salma Chande, alisema wajumbe wa mkutano huo walipiga kura usiku kucha pasipo kutokea kwa vurugu za aina yoyote.

Kwa majibu ya matokeo hayo, mshindi wa nafasi ya Urais, Tumaini Nyamkokya alipata kura 161 wakati Makamu wake Qambos Sulle alishinda kwa kura 175.

Katika uchaguzi huo aliyeukwaa Katibu Mkuu Dk Msigwa alipata kura 180 akimshinda Mgaya aliyepata kura 152 na naibu wake akipata kura 179.

Nafasi ya kamati ya wanawake, Rehema Ludanga alishinda kwa kura 105 na katibu wake Mtui ameshinda kwa kura 92 Msimamizi wa uchaguzi huo alikuwa alitangaza kura za washindi tu na nafasi hizo zilirudiwa kura mara mbili kwa sababu mara ya kwanza washindi hawakupata asilimia 50 kama katiba inavyotaka.

Kutokana na matokeo hayo msimamizi huyo alimtangaza Tumaini Nyamghokya kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) kuwa mshindi na kushika nafasi ya Rais wa Tucta akimrithi Gratian Mkoba aliyemaliza muda wake.

Aidha, Dk Chande alimtangaza Qambos Sulle kutoka Chama cha Walimu (CWT), kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tucta, Dk Msigwa (Katibu Mkuu), Kalanje (Mweka Hazina) na Rehema Ludenga kuwa Mwenyekiti Kamati ya Wanawake.

Aliwatangaza pia Noel Lotary kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO), Menson Mkwawa (CWT), Rehema Mbaga (Talgwu) na Marystella Kalwera, Kuwa wadhamini wa shirikisho hilo kwa kipindi cha miaka mitano.

"Tunashukuru uchaguzi umemalizika bila kuwapo na figisu figisu yoyote, uongozi mpya umejulikana, sasa tunawaachia waliochaguliwa waendelee na majukumu yao mapya," alisema Dk Chande.

Alisema uchaguzi huo ulikuwa na ushindani mkali kwa vile wajumbe walipata shida ya kuwatambua viongozi watakaowafaa kutokana na wengi wao kufanana sifa.

Akizungumza baada ya kuchaguliwa, Katibu Mkuu mteule wa shirikisho hilo, Dk Msigwa aliwashukuru wajumbe kwa kukesha ili waweze kupata viongozi bora watakaowafaa kuwatumika katika kipindi cha miaka mitano watakachokaa madarakani.

"Mmenichagua ili niwe Mtendaji Mkuu wa shirikisho, hivyo nawaahidi nitaongoza kwa kufuata kanuni, Katiba na sheria zilizopo ndani ya shirikisho letu," alisema Dk Msigwa.

Naye Rais mteule wa Tucta, Nyamghokya, aliwataka wanachama wanaounda shirikisho hilo kushirikiana ili kupata mafanikio makubwa zaidi.

Chanzo: Habari leo
 

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Nicholaus Mgaya, ameshindwa kutetea kiti chake baada ya kugaragazwa na Dk Yahaya Msigwa katika uchaguzi uliofanyika na kumalizika usiku wa manane kuamkia jana.

Dk Msigwa anatoka katika Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE).

Kiongozi pekee aliyefanikiwa kutetea nafasi yake katika uchaguzi huo wa jana ni Mweka Hazina wa shirikisho hilo James Kalanje.

Akitangaza matokeo hayo jana asubuhi, Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Uchaguzi huo, Dk Salma Chande, alisema wajumbe wa mkutano huo walipiga kura usiku kucha pasipo kutokea kwa vurugu za aina yoyote.

Kwa majibu ya matokeo hayo, mshindi wa nafasi ya Urais, Tumaini Nyamkokya alipata kura 161 wakati Makamu wake Qambos Sulle alishinda kwa kura 175.

Katika uchaguzi huo aliyeukwaa Katibu Mkuu Dk Msigwa alipata kura 180 akimshinda Mgaya aliyepata kura 152 na naibu wake akipata kura 179.

Nafasi ya kamati ya wanawake, Rehema Ludanga alishinda kwa kura 105 na katibu wake Mtui ameshinda kwa kura 92 Msimamizi wa uchaguzi huo alikuwa alitangaza kura za washindi tu na nafasi hizo zilirudiwa kura mara mbili kwa sababu mara ya kwanza washindi hawakupata asilimia 50 kama katiba inavyotaka.

Kutokana na matokeo hayo msimamizi huyo alimtangaza Tumaini Nyamghokya kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) kuwa mshindi na kushika nafasi ya Rais wa Tucta akimrithi Gratian Mkoba aliyemaliza muda wake.

Aidha, Dk Chande alimtangaza Qambos Sulle kutoka Chama cha Walimu (CWT), kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tucta, Dk Msigwa (Katibu Mkuu), Kalanje (Mweka Hazina) na Rehema Ludenga kuwa Mwenyekiti Kamati ya Wanawake.

Aliwatangaza pia Noel Lotary kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO), Menson Mkwawa (CWT), Rehema Mbaga (Talgwu) na Marystella Kalwera, Kuwa wadhamini wa shirikisho hilo kwa kipindi cha miaka mitano.

"Tunashukuru uchaguzi umemalizika bila kuwapo na figisu figisu yoyote, uongozi mpya umejulikana, sasa tunawaachia waliochaguliwa waendelee na majukumu yao mapya," alisema Dk Chande.

Alisema uchaguzi huo ulikuwa na ushindani mkali kwa vile wajumbe walipata shida ya kuwatambua viongozi watakaowafaa kutokana na wengi wao kufanana sifa.

Akizungumza baada ya kuchaguliwa, Katibu Mkuu mteule wa shirikisho hilo, Dk Msigwa aliwashukuru wajumbe kwa kukesha ili waweze kupata viongozi bora watakaowafaa kuwatumika katika kipindi cha miaka mitano watakachokaa madarakani.

"Mmenichagua ili niwe Mtendaji Mkuu wa shirikisho, hivyo nawaahidi nitaongoza kwa kufuata kanuni, Katiba na sheria zilizopo ndani ya shirikisho letu," alisema Dk Msigwa.

Naye Rais mteule wa Tucta, Nyamghokya, aliwataka wanachama wanaounda shirikisho hilo kushirikiana ili kupata mafanikio makubwa zaidi.

Source: Habari leo
Hiki chama kweli kina maslahi kwa wafanyakazi?mimi naona wanakula hela ya bure,hasa ikizingatiwa sasa kuwa ni mfumo wa soko huria na mwajiri ana nguvu zaidi kuhusu haki za mwajiriwa.Hichi chama kinakula tu makato ya wafanyakazi kwa kifupi hakimsaidii mfanyakazi
 
Hiki chama hakuna manufaa yeyote kwa wafanyakazi, hawana meno kabisa, wamekaa kupiga mpunga tu. Tena huyu Mgaya alikuwa anatoa vitisho tu bila practical action. Any how hata anayeingia wanatoka Jamii ilele ya wabena kama siyo mkinga. Hawa watu asili yao ni watu waoga na wako easily manipulated ie ni watu wa Yes to what they are told. Thus why pale ikulu wapo wengi just because of that.
 
Hizi trade unions sionagi umuhimu wake kwenye nchi kama Tanzania.

Umewahi kufanya kazi ya kuajiliwa na kukawa na chama kama hivyo? Kaka hivi vyama vya wafanyakazi vina umuhimu sana na vinasaidia sana. Ukiwa mwanachama wa vyama hivi kufukuzwa fukuzwa kazi kijinga kijinga hakupo ILA ukikuta viongozi wa chama hicho cha wafanyakazi waroho waroho wakinogewa kuhongwa na mwajili nyie wafanyakazi mtajuta!!!
 
Tena huyo waliemchagua ndio atakuwa bubu kabisa na kiziwi maana hatathubutu kukosoa serikali ambayo ndio imemuajiri, sijui hata wanachagua kwa vigezo gani hawa viongozi.
 
Hiki chama hakuna manufaa yeyote kwa wafanyakazi, hawana meno kabisa, wamekaa kupiga mpunga tu. Tena huyu Mgaya alikuwa anatoa vitisho tu bila practical action. Any how hata anayeingia wanatoka Jamii ilele ya wabena kama siyo mkinga. Hawa watu asili yao ni watu waoga na wako easily manipulated ie ni watu wa Yes to what they are told. Thus why pale ikulu wapo wengi just because of that.

Mkuu huyu Mgaya ni Mbondei wa Muheza sio mbena majina tu hayo, aliwahi kuweka nia ya kugombea ubunge pale Muheza kwa chama chenu akapigwa mweleka kura za maoni, hata hivyo sio msomi kama huyu Dr msigwa anaeingia time will tell
 
Hizi trade unions sionagi umuhimu wake kwenye nchi kama Tanzania.
Tatizo hao kina mgaya walikuwa ni wafuasi wa chama cha wacha waisome namba eee lalalala mbele kwa mbele na huyo mgaya ni mwanachama kabisa kwa hiyo ndiyo maana hakuwa na msimamo katika kutetea watumishi wanyonge na maslahi yao,sasa wacha wamsomeshe namba
 
Tatizo hao kina mgaya walikuwa ni wafuasi wa chama cha wacha waisome namba eee lalalala mbele kwa mbele na huyo mgaya ni mwanachama kabisa kwa hiyo ndiyo maana hakuwa na msimamo katika kutetea watumishi wanyonge na maslahi yao,sasa wacha wamsomeshe namba

umri umeenda hawezi tena kushika chaki pale Mkanyageni primary school Muheza
 
Mmeskia maruban huko Ujeruman wameweka ngumu wakitaka vijana waajiriwe kwenye sekta ya uruban na mpunga uongezwe.Huo mgomo wa kampuni moja tu
HADI LEO HAKUNA MAELEZO SAHIHI WHY WATUMISHI HAWAJAONGEZEWA SALARY KAMA MIKATABA INAVYOSEMA TUCTA WAPO KIMYAAAA
 
Hiki chama hakuna manufaa yeyote kwa wafanyakazi, hawana meno kabisa, wamekaa kupiga mpunga tu. Tena huyu Mgaya alikuwa anatoa vitisho tu bila practical action. Any how hata anayeingia wanatoka Jamii ilele ya wabena kama siyo mkinga. Hawa watu asili yao ni watu waoga na wako easily manipulated ie ni watu wa Yes to what they are told. Thus why pale ikulu wapo wengi just because of that.

Mgaya ni Mbondei bana.......
 
Back
Top Bottom