Vigezo vya kuandaa 'Seniority list' katika utumishi

Stanley.

JF-Expert Member
Sep 6, 2011
660
298
Ndugu zangu wanajamvi mliokatika utumishi hasa wa umma ninaomba kuelekezwa namna Seniority list au TANGE inavyoandaliwa na mpangalio wake unakuwaje. Nawasilisha.
 
Ndugu zangu wanajamvi mliokatika utumishi hasa wa umma ninaomba kuelekezwa namna Seniority list au TANGE inavyoandaliwa na mpangalio wake unakuwaje. Nawasilisha.
Mkuu yaani mambo ya TANGE umeyaleta humu ndani basi naamini wataibuka wajuzi wa Exel watakuja.
 
Ndugu zangu wanajamvi mliokatika utumishi hasa wa umma ninaomba kuelekezwa namna Seniority list au TANGE inavyoandaliwa na mpangalio wake unakuwaje. Nawasilisha.

Cheo, tarehe ya kuthibitishwa, tarehe ya kuajiriwa, tarehe ya cheo cha sasa, elimu, mwaka wa kuzaliwa na jina. Iwapo watumishi wamelingana kwa kila kitu, basi angalia majina yao. Mf. Asha ni senior kwa Kaumza. Na wengine huwa wakitoka katka cheo,.j
 
Cheo, tarehe ya kuthibitishwa, tarehe ya kuajiriwa, tarehe ya cheo cha sasa, elimu, mwaka wa kuzaliwa na jina. Iwapo watumishi wamelingana kwa kila kitu, basi angalia majina yao. Mf. Asha ni senior kwa Kaumza. Na wengine huwa wakitoka katka cheo, unaangalia check number.

Nashukuru kwa ufafanuzi wako, nimekuelewa kabisa pasi na shaka. Nataka kufahamu je Elimu inatofautisha nani atangulie na nani afuate?
 
Cheo, tarehe ya kuthibitishwa, tarehe ya kuajiriwa, tarehe ya cheo cha sasa, elimu, mwaka wa kuzaliwa na jina. Iwapo watumishi wamelingana kwa kila kitu, basi angalia majina yao. Mf. Asha ni senior kwa Kaumza. Na wengine huwa wakitoka katka cheo, unaangalia check number.

mkuu unataka kutuambia nini sisi wenye watoto waitwao
1. Zebedayo
2. Zuhura
3. Zurufa
4. Zurukheli
5. Zawadi
6. Zaituni
na mengineyo yanayofanana na hayo!
 
mkuu unataka kutuambia nini sisi wenye watoto waitwao
1. Zebedayo
2. Zuhura
3. Zurufa
4. Zurukheli
5. Zawadi
6. Zaituni
na mengineyo yanayofanana na hayo!

Ngoja mtaalam Kaumza atakuja kukufafanulia lakini bila shaka utafuata alphabet moja moja kwa kila jina mpaka jina la mwisho litapatikana kwa mpangilio wa abcdefghijklmn... kwa herufi zinazofuata. Kaumza naona unapitia naomba unisaidie pia kama elimu inaweza kusaidia mpangilio wa seniority lists Mfano mwenye stashahada kama ameanza kuingia kazini je mwenye shahada aliyemfuata kuingia kazini atatangulia katika list au ataendelea kuwa nyuma.
 
Nashukuru kwa ufafanuzi wako, nimekuelewa kabisa pasi na shaka. Nataka kufahamu je Elimu inatofautisha nani atangulie na nani afuate?

Iwapo mnalingana kwa vigezo vyote nilivyovitaja, basi wanaangalia elimu. Mwenye elimu kubwa anakuwa senior. Na iwapo elimu mmekuwa sawa, wanaangalia jinsia. Mwenye jinsia ke anakuwa senior kwa me. Na iwapo jinsia ni sawa wanaangalia check namba. Mwenye check namba kubwa(mwenye namba ndogo) ndo anakuwa senior. Huo ndo mwisho
 
Ngoja mtaalam Kaumza atakuja kukufafanulia lakini bila shaka utafuata alphabet moja moja kwa kila jina mpaka jina la mwisho litapatikana kwa mpangilio wa abcdefghijklmn... kwa herufi zinazofuata. Kaumza naona unapitia naomba unisaidie pia kama elimu inaweza kusaidia mpangilio wa seniority lists Mfano mwenye stashahada kama ameanza kuingia kazini je mwenye shahada aliyemfuata kuingia kazini atatangulia katika list au ataendelea kuwa nyuma.

Chukua mfano huu: X ni legal officer daraja 2 na ameajiriwa 2009 na ana digrii ya kwanza ya sheria. Y ana masters ya sheria, ameajiriwa 2010 kama legal ofisa daraja 2 ktk ofisi moja na X. Hapa senior ni X. Ila Y atakuwa na advantage ya increment 2 za mshahara kila mwaka. Mf. Kama nyongeza ya mshahara kwa mwaka ni sh 20000, Y atapata 2*20000.
 
Nashukuru kwa ufafanuzi wako, nimekuelewa kabisa pasi na shaka. Nataka kufahamu je Elimu inatofautisha nani atangulie na nani afuate?

Iwapo mnalingana kwa vigezo vyote nilivyovitaja, basi wanaangalia elimu. Mwenye elimu kubwa anakuwa senior. Na iwapo elimu mmekuwa sawa, wanaangalia jinsia. Mwenye jinsia ke anakuwa senior kwa me. Na iwapo jinsia ni sawa wanaangalia check namba. Mwenye check namba kubwa(mwenye namba ndogo) ndo anakuwa senior. Huo ndo mwisho
 
Iwapo mnalingana kwa vigezo vyote nilivyovitaja, basi wanaangalia elimu. Mwenye elimu kubwa anakuwa senior. Na iwapo elimu mmekuwa sawa, wanaangalia jinsia. Mwenye jinsia ke anakuwa senior kwa me. Na iwapo jinsia ni sawa wanaangalia check namba. Mwenye check namba kubwa(mwenye namba ndogo) ndo anakuwa senior. Huo ndo mwisho

Nashukuru ndugu yangu kwa ufafanuzi wako. umekuwa kisima cha kuchota maarifa. Utanisaidia pia kwa wakati mwingine ahsante sana!
 
Nashukuru ndugu yangu kwa ufafanuzi wako. umekuwa kisima cha kuchota maarifa. Utanisaidia pia kwa wakati mwingine ahsante sana!

Usijali. Kwa msaada wa kisheria au utumishi wa umma, unaweza kuni-PM. Tutasaidiana kwa kile tutakachojaaliwa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom