Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu yaani mambo ya TANGE umeyaleta humu ndani basi naamini wataibuka wajuzi wa Exel watakuja.Ndugu zangu wanajamvi mliokatika utumishi hasa wa umma ninaomba kuelekezwa namna Seniority list au TANGE inavyoandaliwa na mpangalio wake unakuwaje. Nawasilisha.
Tange inajieleza yenyewe yaani kuanzia the most senior mpaka most journer.Kada ipi?
Nimeeleza hapo juu sekta ya umma. Kama pia na sekta binafsi wanautaratibu mwingine nikijulishwa itakuwa fresh!
Ndugu zangu wanajamvi mliokatika utumishi hasa wa umma ninaomba kuelekezwa namna Seniority list au TANGE inavyoandaliwa na mpangalio wake unakuwaje. Nawasilisha.
Cheo, tarehe ya kuthibitishwa, tarehe ya kuajiriwa, tarehe ya cheo cha sasa, elimu, mwaka wa kuzaliwa na jina. Iwapo watumishi wamelingana kwa kila kitu, basi angalia majina yao. Mf. Asha ni senior kwa Kaumza. Na wengine huwa wakitoka katka cheo, unaangalia check number.
Cheo, tarehe ya kuthibitishwa, tarehe ya kuajiriwa, tarehe ya cheo cha sasa, elimu, mwaka wa kuzaliwa na jina. Iwapo watumishi wamelingana kwa kila kitu, basi angalia majina yao. Mf. Asha ni senior kwa Kaumza. Na wengine huwa wakitoka katka cheo, unaangalia check number.
mkuu unataka kutuambia nini sisi wenye watoto waitwao
1. Zebedayo
2. Zuhura
3. Zurufa
4. Zurukheli
5. Zawadi
6. Zaituni
na mengineyo yanayofanana na hayo!
Nashukuru kwa ufafanuzi wako, nimekuelewa kabisa pasi na shaka. Nataka kufahamu je Elimu inatofautisha nani atangulie na nani afuate?
Ngoja mtaalam Kaumza atakuja kukufafanulia lakini bila shaka utafuata alphabet moja moja kwa kila jina mpaka jina la mwisho litapatikana kwa mpangilio wa abcdefghijklmn... kwa herufi zinazofuata. Kaumza naona unapitia naomba unisaidie pia kama elimu inaweza kusaidia mpangilio wa seniority lists Mfano mwenye stashahada kama ameanza kuingia kazini je mwenye shahada aliyemfuata kuingia kazini atatangulia katika list au ataendelea kuwa nyuma.
Nashukuru kwa ufafanuzi wako, nimekuelewa kabisa pasi na shaka. Nataka kufahamu je Elimu inatofautisha nani atangulie na nani afuate?
Iwapo mnalingana kwa vigezo vyote nilivyovitaja, basi wanaangalia elimu. Mwenye elimu kubwa anakuwa senior. Na iwapo elimu mmekuwa sawa, wanaangalia jinsia. Mwenye jinsia ke anakuwa senior kwa me. Na iwapo jinsia ni sawa wanaangalia check namba. Mwenye check namba kubwa(mwenye namba ndogo) ndo anakuwa senior. Huo ndo mwisho
Nashukuru ndugu yangu kwa ufafanuzi wako. umekuwa kisima cha kuchota maarifa. Utanisaidia pia kwa wakati mwingine ahsante sana!