Vigezo vitakavyotumika Kumuengua mgombea wa Igunga hivi hapa!

MgungaMiba

JF-Expert Member
Aug 28, 2011
999
815
Kuna vigezo vitano ambavyo CCM wameviandaa kwa kushirikiana na Mrugenzi wa Halmashauri ya Igunga (DED) ambae ndie msimamizi mkuu wa uchaguzi huu na Idara ya Elimu ambayo ndiyo muajiri wagombea huyo Mwl Kashindye kwa ajili ya kumuengua katika kinyang'anyiro kijacho. Hapa vitatajwa vipengele viwili vya kwanza ambavyo ni dhahiri vitamuengua visipofanyiwa kazi mapema, vitatu vilivyobaki havitatajwa hapa kwa sababu havina nguvu kisheria na vimelenga kuwa Character Assasination kwa mgombea huyo ili hata akiteuliwa vitumike kama propaganda material kumuharibia mgombea huyo wakati wa campaign, hivyo si busara kuvitaja hapa kwani itakuwa ni kusaidia kueneza propaganda hiyo Unwittingly.

1. Kigezo cha kwanza, ikumbukwe kuwa ili mtumishi yeyote wa serikali aweze kugombea ubunge, ni sharti apate kibali kutoka kwa mwajiri wake, ambaye ni serikali kupita idara husika, au achukue likizo ya bila malipo ili endapo akishindwa uchaguzi arejee kazini, au ajiuzulu kazi kabisa, ili akishindwa iwe imekula kwake. Mwl Kashindye baada ya kuteuliwa kuwa mgombea wa CHADEMA alianza utaratibu wa kupata idhini ya mwajiri wake, lakini cha kushangaza ni kuwa aliwekewa ngumu kupita kiasi (sidhani kama Dr Kafumu nae kafanyiwa hivyo) ilifika mahali Mwl Kashindye kutaka kujiuzulu, lakini pia ikawa ni mtihani, kwani alitakiwa kutoa notice ya mwezi mzima, kitu ambacho hakingewezekana kutokana na muda uliopo, ikabidi maskini Mwalimu huyo aamue kujiuzulu kwa notice ya 24hrs na alipe mshahara wa mwezi mmoja, ilipofikia hapo, akaagizwa aende mkoani Tabora ili aweze kupata likizo ya bila malipo.

Alikwenda Tabora na akapatiwa likizo hiyo na barua husika inayothibitisha hivyo. Mpaka hapo kila kitu kwa juujuu kinaonekana kuwa ni sawa, KOSA! Delays alizofanyiwa Mwl Kashindye zilikuwa ni za makusudi na very tactical, kwa maelekezo ya CCM, kwani under normal circumstances hakukuwa na sababu za kufanya hivyo. Wakati akizungushwa hivyo kumbe huku Maexpert wa kuchakachua walikuwa kazini wakidesign mtego utakaofyatuka wakati wa uteuzi ukifika, CCM kupitia mgombea wake itaweka pingamizi Mwl Kashindye asiteuliwe kwa kuwa ni mtumishi wa serkali, yeye atajitetea kuwa amefuata utaratibu wa kuchukua likizo bila malipo na barua yake ndio kielelezo chake, lakini haitasaidia kitu kwa kuwa barua hiyo, ambayo utayarishaji wake ulisimamiwa na wale Maexpert, itapingwa kuwa ina mapungufu mengi hivyo haikidhi haja, kwa hivyo Mwl Kashindye ataendelea kutambulika Kama mtumishi alie kazini bado kwa hiyo atapoteza sifa za kuwa mgombea!

Kigezo cha pili ambacho kitatumika kumuengua Mwl Kashindye, Kisha mwisho Kama hakutakuwa na interruption yoyote na kama charge itabakia, basi nitasuggest namna ya kupangua, lakini naamini kwa kuanika hadharani njama hizi, basi kutavunja nguvu sana utekelezaji wake.

2. Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa. Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.

Vipengele hivi viwili visipofanyiwa kazi (Wanasheria wanajua hivyo) hata kimojawapo tu kikipita kinatosha kuleta maafa na kilio, kulalamika na mikwara mingi baada ya mzinga kulia, havitasaidia. Kwa kuwa nachukia dhulma na kupenda haki itendeke, ingawa sina mamlaka yoyote ndani ya CDM, basi naomba tu wanasheria wa CDM waikague vizuri barua ya likizo ya Mgombea, kisha waiangalie zheria inayohusiana na utaratibu wa utoaji wa barua hiyo, kama vile, je, aliesaini barua hiyo Ana mamlaka hayo? Maelezo na mihuri yake inakidhi? Chronological factors zimekaa sawa? Hakuna errors zozote (typing or otherwise) ambazo zinaweza kupotosha maana hivyo kutoa mwanya wa barua hiyo kupingwa uhalali wake?

Pili, wahakikishe kuwa ni kweli kuwa katibu wa Wilaya wa CDM Bw Christopher hakuchaguliwa katika nafasi yake kwa mujibu wa katiba ya CDM, kama ndivyo, je ni utaratibu gani ulitumika wa kumuinstall, je document zilizomuhalalisha zipo na zipo valid hadi sasa?Kila ilivyo, wanasheria wazipuuze hata chembe ya factor yoyote inayoweza kutumiwa kumkwamisha mgombea, otherwise muda hautatosha kujitetea mahakamani kama ilivyokuwa kwa Wenje kule Mwanza, uchaguzi ule ulikuwa wa miezi mitatu lakini huu utakuwa wa wiki tatu tu, mahakama ikimaliza kusikiliza rufaa kabla haijatoa uamuzi uchaguzi utakuwa umekwisha, ngoma itabidi ije ianze upya!

MIBA YA MGUNGA HAIUCHOMI MGUNGA!
 
Hilo lisikusumbue. CCM haiwezi kutaka mgombea wa CUF au CHADEMA atoke kwenye race kwa sababu uwepo wao ni fursa zaidi kwa CCM. Actually CCM inataka kuwe na wagombea zaidi wa upinzani.
CCM ina kura zake fixed na inahitaji kudig kidogo kwa undecided voters ili ishinde. Tatizo ni kwamba undecided huwa wanalearn upinzani without specific party affiliation, kwahiyo kadri wapinzani wanavyoongezeka ndio ushindi wa CCM percentage wise unavyozidi kunona.

Katika uchaguzi huu CCM itatumia taaluma za siasa na uchaguzi. Planning ya ufunguzi wa kampeni inaonyesha jinsi uchaguzi huu utakavyokuwa sophisticated. Kama Mkapa aliweza kumuweka sawa Seif Shariff Hamad, hawezi kushindwa kuwaweka sawa ring leaders wa Igunga.
 
hopefully concerns zako zitafanyiwa kazi. ila usitegemee ccm kuona aibu kwa sababu mbinu zao zimewekwa wazi, CCM HAINA AIBU! dhambi inaleta usugu!
 
Likizo bila Malipo kwa mtumishi wa Umma hutolewa na Katibu Mkuu UTUMISHI, yeye tu ndiye mwenye madaraka hayo sasa kama hyo barua ilitolewa na maafisa wa serikali huko Tabora basi kuna makosa na ni vyema suala hili lifanyiwe kazi mapema.
 
2. Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa. Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.

makatibu kwenye vyama nao wanachaguliwa? Hawa siyo watendaji ambao wanapaswa kuteuliwa na vikao husika?.......................just wondering aloud.................................sina katiba ya chadema kusoma haya majibu ya maswali elekezi............
 
well, sina hakika kama CDM itashinda.........uchaguzi wa igunga sio mgumu ila gamba CCM ndo tatizo pale.
 
1. Kigezo cha kwanza, ikumbukwe kuwa ili mtumishi yeyote wa serikali aweze kugombea ubunge, ni sharti apate kibali kutoka kwa mwajiri wake, ambaye ni serikali kupita idara husika, au achukue likizo ya bila malipo ili endapo akishindwa uchaguzi arejee kazini, au ajiuzulu kazi kabisa, ili akishindwa iwe imekula kwake. Mwl Kashindye baada ya kuteuliwa kuwa mgombea wa CHADEMA alianza utaratibu wa kupata idhini ya mwajiri wake, lakini cha kushangaza ni kuwa aliwekewa ngumu kupita kiasi (sidhani kama Dr Kafumu nae kafanyiwa hivyo) ilifika mahali Mwl Kashindye kutaka kujiuzulu, lakini pia ikawa ni mtihani, kwani alitakiwa kutoa notice ya mwezi mzima, kitu ambacho hakingewezekana kutokana na muda uliopo, ikabidi maskini Mwalimu huyo aamue kujiuzulu kwa notice ya 24hrs na alipe mshahara wa mwezi mmoja, ilipofikia hapo, akaagizwa aende mkoani Tabora ili aweze kupata likizo ya bila malipo.

Alikwenda Tabora na akapatiwa likizo hiyo na barua husika inayothibitisha hivyo. Mpaka hapo kila kitu kwa juujuu kinaonekana kuwa ni sawa, KOSA! Delays alizofanyiwa Mwl Kashindye zilikuwa ni za makusudi na very tactical, kwa maelekezo ya CCM, kwani under normal circumstances hakukuwa na sababu za kufanya hivyo. Wakati akizungushwa hivyo kumbe huku Maexpert wa kuchakachua walikuwa kazini wakidesign mtego utakaofyatuka wakati wa uteuzi ukifika, CCM kupitia mgombea wake itaweka pingamizi Mwl Kashindye asiteuliwe kwa kuwa ni mtumishi wa serkali, yeye atajitetea kuwa amefuata utaratibu wa kuchukua likizo bila malipo na barua yake ndio kielelezo chake, lakini haitasaidia kitu kwa kuwa barua hiyo, ambayo utayarishaji wake ulisimamiwa na wale Maexpert, itapingwa kuwa ina mapungufu mengi hivyo haikidhi haja, kwa hivyo Mwl Kashindye ataendelea kutambulika Kama mtumishi alie kazini bado kwa hiyo atapoteza sifa za kuwa mgombea!

Kigezo cha pili ambacho kitatumika kumuengua Mwl Kashindye, Kisha mwisho Kama hakutakuwa na interruption yoyote na kama charge itabakia, basi nitasuggest namna ya kupangua, lakini naamini kwa kuanika hadharani njama hizi, basi kutavunja nguvu sana utekelezaji wake.


nilelewavyo ni kuwa ukishajaza fomu ya kugombea uongozi kupitia chama chochoe moja kwa zote umepoteza ajira kwenye taasisis yoyote ya umma..............na kama hili ni kweli hizo hoja zote ulizozitoa hazina msingi.................kwa kuongezea tu ni kuwa ajira ni hiari huhitaji kibali cha mwajiri kuthibitisha kuwa wewe siyo mwajiriwa.................tarehe ile ambayo umwemwandikia barua ya kuwa siyo mtumishi wake ndiyo inatambuliwa kisheria ya kuwa utumishi wako umekoma......................................................hili ina uhakika nalo na hivyo kufanya hoja hii kukosa makalio...................achilia mbali mashiko......................
 
2. Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa. Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.

hoja hii sanasana yaweza kuchelewesha uchaguzi wa Igunga kwa vile ni mahakama tu ndicho chombo chenye mamlaka ya kutengua ajira ya huyo katibu si NEC au msajili wa vyama mwenye mamlaka hayo au kutafsiri kama ajira yake imezingatia sheria.....................kwa hiyo malalamiko ya ccm kama yapo yapaswa kupelekwa mahakamani......................na kama hili likifanyika inamaanisha uchaguzi kwanza yabidi uahirishwe...................who loses if the election is postponed? tough question.................................the winner is the major casualty................
 
Hiyo mbona sasa inakuwa kinyume cha katiba kwa nini serikali au muajiri mwingine yeyote ang'ang'anie kukuajiri wakati wewe hutaki??????
 
Tafadhalini viongozi wa Chadema haya mambo yasipuuzwe hata kidogo yashughulikiwe haraka kwa ngazi ya kitaifa na mgombea apate muda wa kupumzika na kujipanga na kuwaandaa wapiga kura wake kwa ushindi mnono na siyo kuanza kukimbizana na barua za likizo .
 
makatibu kwenye vyama nao wanachaguliwa? Hawa siyo watendaji ambao wanapaswa kuteuliwa na vikao husika?.......................just wondering aloud.................................sina katiba ya chadema kusoma haya majibu ya maswali elekezi............
<br />
<br />
Penye rangi, mbona soft copy ya Katiba nzima ipo kwenye website ya CHADEMA! Kiurahisi google "Katiba ya CHADEMA", then nenda kwenye uongozi wa wilaya.
 
makatibu kwenye vyama nao wanachaguliwa? Hawa siyo watendaji ambao wanapaswa kuteuliwa na vikao husika?.......................just wondering aloud.................................sina katiba ya chadema kusoma haya majibu ya maswali elekezi............

Kwa mujibu wa katiba ya chadema katibu wa wilaya anachaguliwa na mkutano mkuu wa wilaya, lakini pia anaweza kuteuliwa kutokana na mazingira ama sababu fulani.
 
Kuna vigezo vitano ambavyo CCM wameviandaa kwa kushirikiana na Mrugenzi wa Halmashauri ya Igunga (DED) ambae ndie msimamizi mkuu wa uchaguzi huu na Idara ya Elimu ambayo ndiyo muajiri wagombea huyo Mwl Kashindye kwa ajili ya kumuengua katika kinyang'anyiro kijacho. Hapa vitatajwa vipengele viwili vya kwanza ambavyo ni dhahiri vitamuengua visipofanyiwa kazi mapema, vitatu vilivyobaki havitatajwa hapa kwa sababu havina nguvu kisheria na vimelenga kuwa Character Assasination kwa mgombea huyo ili hata akiteuliwa vitumike kama propaganda material kumuharibia mgombea huyo wakati wa campaign, hivyo si busara kuvitaja hapa kwani itakuwa ni kusaidia kueneza propaganda hiyo Unwittingly.

1. Kigezo cha kwanza, ikumbukwe kuwa ili mtumishi yeyote wa serikali aweze kugombea ubunge, ni sharti apate kibali kutoka kwa mwajiri wake, ambaye ni serikali kupita idara husika, au achukue likizo ya bila malipo ili endapo akishindwa uchaguzi arejee kazini, au ajiuzulu kazi kabisa, ili akishindwa iwe imekula kwake. Mwl Kashindye baada ya kuteuliwa kuwa mgombea wa CHADEMA alianza utaratibu wa kupata idhini ya mwajiri wake, lakini cha kushangaza ni kuwa aliwekewa ngumu kupita kiasi (sidhani kama Dr Kafumu nae kafanyiwa hivyo) ilifika mahali Mwl Kashindye kutaka kujiuzulu, lakini pia ikawa ni mtihani, kwani alitakiwa kutoa notice ya mwezi mzima, kitu ambacho hakingewezekana kutokana na muda uliopo, ikabidi maskini Mwalimu huyo aamue kujiuzulu kwa notice ya 24hrs na alipe mshahara wa mwezi mmoja, ilipofikia hapo, akaagizwa aende mkoani Tabora ili aweze kupata likizo ya bila malipo. KIPI NI KIPI?

Alikwenda Tabora na akapatiwa likizo hiyo na barua husika inayothibitisha hivyo. Mpaka hapo kila kitu kwa juujuu kinaonekana kuwa ni sawa, KOSA! Delays alizofanyiwa Mwl Kashindye zilikuwa ni za makusudi na very tactical, kwa maelekezo ya CCM, kwani under normal circumstances hakukuwa na sababu za kufanya hivyo. Wakati akizungushwa hivyo kumbe huku Maexpert wa kuchakachua walikuwa kazini wakidesign mtego utakaofyatuka wakati wa uteuzi ukifika, CCM kupitia mgombea wake itaweka pingamizi Mwl Kashindye asiteuliwe kwa kuwa ni mtumishi wa serkali, yeye atajitetea kuwa amefuata utaratibu wa kuchukua likizo bila malipo na barua yake ndio kielelezo chake, lakini haitasaidia kitu kwa kuwa barua hiyo, ambayo utayarishaji wake ulisimamiwa na wale Maexpert, itapingwa kuwa ina mapungufu mengi hivyo haikidhi haja, kwa hivyo Mwl Kashindye ataendelea kutambulika Kama mtumishi alie kazini bado kwa hiyo atapoteza sifa za kuwa mgombea!

Kigezo cha pili ambacho kitatumika kumuengua Mwl Kashindye, Kisha mwisho Kama hakutakuwa na interruption yoyote na kama charge itabakia, basi nitasuggest namna ya kupangua, lakini naamini kwa kuanika hadharani njama hizi, basi kutavunja nguvu sana utekelezaji wake.

2. Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa. Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.

Vipengele hivi viwili visipofanyiwa kazi (Wanasheria wanajua hivyo) hata kimojawapo tu kikipita kinatosha kuleta maafa na kilio, kulalamika na mikwara mingi baada ya mzinga kulia, havitasaidia. Kwa kuwa nachukia dhulma na kupenda haki itendeke, ingawa sina mamlaka yoyote ndani ya CDM, basi naomba tu wanasheria wa CDM waikague vizuri barua ya likizo ya Mgombea, kisha waiangalie zheria inayohusiana na utaratibu wa utoaji wa barua hiyo, kama vile, je, aliesaini barua hiyo Ana mamlaka hayo? Maelezo na mihuri yake inakidhi? Chronological factors zimekaa sawa? Hakuna errors zozote (typing or otherwise) ambazo zinaweza kupotosha maana hivyo kutoa mwanya wa barua hiyo kupingwa uhalali wake?

Pili, wahakikishe kuwa ni kweli kuwa katibu wa Wilaya wa CDM Bw Christopher hakuchaguliwa katika nafasi yake kwa mujibu wa katiba ya CDM, kama ndivyo, je ni utaratibu gani ulitumika wa kumuinstall, je document zilizomuhalalisha zipo na zipo valid hadi sasa?Kila ilivyo, wanasheria wazipuuze hata chembe ya factor yoyote inayoweza kutumiwa kumkwamisha mgombea, otherwise muda hautatosha kujitetea mahakamani kama ilivyokuwa kwa Wenje kule Mwanza, uchaguzi ule ulikuwa wa miezi mitatu lakini huu utakuwa wa wiki tatu tu, mahakama ikimaliza kusikiliza rufaa kabla haijatoa uamuzi uchaguzi utakuwa umekwisha, ngoma itabidi ije ianze upya!

MIBA YA MGUNGA HAIUCHOMI MGUNGA!

Toa ma-propaganda yako ya kitoto hapa... vigezo na masharti vimezingatiwa mara fomu ya katibu ajaze katibu wilaya IMEJAZWA zen oh hajachaguliwa kwa mujibu wa katiba ya chadema so kachaguliwa kwa mujibu wa katiba ya magamba...
pia we mzushi twenty four hour kuacha kazi ndio sheria ya kazi inavyosema mara umezusha likizo bila malipo wakati aliakuwa umesema karudisha mshahara ACHA PROPAGANDA ZISIZO NA MANTIKI MGOMBEA WETU KISHAPEWA NA HATI YA KUGOMBEA kula kona NGAMBA
 
kama malaria sugu vile kuandika mengi pontless anyway utajivua sana magamba mpaka majina lakini wapi
 
Haya sasa si madogo; well siasa ni mikakati; we have said it others have said it before. Huwezi kuombea ushindi kwenye siasa, unautengeneza.

Ndio tufauti ya chadema na CCM , sie chadema tunaomba nyie CCM mnatengeneza huo ushindi...
Nguvu ya umma haitengenezwi.... vipi umeshawatengenezea huo mkakati hao magamba? mtaiba kura ngapi? malori mangapi na vituo hewa vingapi? TUNAKUJA IGUNGU KULINDA KULA kwa nguvu ya umma ulizia Mwanza, Ubungo na Kawe wanakuambia hao wenzio wanamkakati
 
Mmmm kweli CDM washindwe kubaini hilo.Nakukumbusha sakata la kutunga la mbunge wa mwanza.Alienguliwa na jamaa akatangazwa anampinzani lakini haki ikapatikana mahakamani.Hoja zaifu saana
 
Back
Top Bottom