MgungaMiba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2011
- 999
- 815
Kuna vigezo vitano ambavyo CCM wameviandaa kwa kushirikiana na Mrugenzi wa Halmashauri ya Igunga (DED) ambae ndie msimamizi mkuu wa uchaguzi huu na Idara ya Elimu ambayo ndiyo muajiri wagombea huyo Mwl Kashindye kwa ajili ya kumuengua katika kinyang'anyiro kijacho. Hapa vitatajwa vipengele viwili vya kwanza ambavyo ni dhahiri vitamuengua visipofanyiwa kazi mapema, vitatu vilivyobaki havitatajwa hapa kwa sababu havina nguvu kisheria na vimelenga kuwa Character Assasination kwa mgombea huyo ili hata akiteuliwa vitumike kama propaganda material kumuharibia mgombea huyo wakati wa campaign, hivyo si busara kuvitaja hapa kwani itakuwa ni kusaidia kueneza propaganda hiyo Unwittingly.
1. Kigezo cha kwanza, ikumbukwe kuwa ili mtumishi yeyote wa serikali aweze kugombea ubunge, ni sharti apate kibali kutoka kwa mwajiri wake, ambaye ni serikali kupita idara husika, au achukue likizo ya bila malipo ili endapo akishindwa uchaguzi arejee kazini, au ajiuzulu kazi kabisa, ili akishindwa iwe imekula kwake. Mwl Kashindye baada ya kuteuliwa kuwa mgombea wa CHADEMA alianza utaratibu wa kupata idhini ya mwajiri wake, lakini cha kushangaza ni kuwa aliwekewa ngumu kupita kiasi (sidhani kama Dr Kafumu nae kafanyiwa hivyo) ilifika mahali Mwl Kashindye kutaka kujiuzulu, lakini pia ikawa ni mtihani, kwani alitakiwa kutoa notice ya mwezi mzima, kitu ambacho hakingewezekana kutokana na muda uliopo, ikabidi maskini Mwalimu huyo aamue kujiuzulu kwa notice ya 24hrs na alipe mshahara wa mwezi mmoja, ilipofikia hapo, akaagizwa aende mkoani Tabora ili aweze kupata likizo ya bila malipo.
Alikwenda Tabora na akapatiwa likizo hiyo na barua husika inayothibitisha hivyo. Mpaka hapo kila kitu kwa juujuu kinaonekana kuwa ni sawa, KOSA! Delays alizofanyiwa Mwl Kashindye zilikuwa ni za makusudi na very tactical, kwa maelekezo ya CCM, kwani under normal circumstances hakukuwa na sababu za kufanya hivyo. Wakati akizungushwa hivyo kumbe huku Maexpert wa kuchakachua walikuwa kazini wakidesign mtego utakaofyatuka wakati wa uteuzi ukifika, CCM kupitia mgombea wake itaweka pingamizi Mwl Kashindye asiteuliwe kwa kuwa ni mtumishi wa serkali, yeye atajitetea kuwa amefuata utaratibu wa kuchukua likizo bila malipo na barua yake ndio kielelezo chake, lakini haitasaidia kitu kwa kuwa barua hiyo, ambayo utayarishaji wake ulisimamiwa na wale Maexpert, itapingwa kuwa ina mapungufu mengi hivyo haikidhi haja, kwa hivyo Mwl Kashindye ataendelea kutambulika Kama mtumishi alie kazini bado kwa hiyo atapoteza sifa za kuwa mgombea!
Kigezo cha pili ambacho kitatumika kumuengua Mwl Kashindye, Kisha mwisho Kama hakutakuwa na interruption yoyote na kama charge itabakia, basi nitasuggest namna ya kupangua, lakini naamini kwa kuanika hadharani njama hizi, basi kutavunja nguvu sana utekelezaji wake.
2. Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa. Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.
Vipengele hivi viwili visipofanyiwa kazi (Wanasheria wanajua hivyo) hata kimojawapo tu kikipita kinatosha kuleta maafa na kilio, kulalamika na mikwara mingi baada ya mzinga kulia, havitasaidia. Kwa kuwa nachukia dhulma na kupenda haki itendeke, ingawa sina mamlaka yoyote ndani ya CDM, basi naomba tu wanasheria wa CDM waikague vizuri barua ya likizo ya Mgombea, kisha waiangalie zheria inayohusiana na utaratibu wa utoaji wa barua hiyo, kama vile, je, aliesaini barua hiyo Ana mamlaka hayo? Maelezo na mihuri yake inakidhi? Chronological factors zimekaa sawa? Hakuna errors zozote (typing or otherwise) ambazo zinaweza kupotosha maana hivyo kutoa mwanya wa barua hiyo kupingwa uhalali wake?
Pili, wahakikishe kuwa ni kweli kuwa katibu wa Wilaya wa CDM Bw Christopher hakuchaguliwa katika nafasi yake kwa mujibu wa katiba ya CDM, kama ndivyo, je ni utaratibu gani ulitumika wa kumuinstall, je document zilizomuhalalisha zipo na zipo valid hadi sasa?Kila ilivyo, wanasheria wazipuuze hata chembe ya factor yoyote inayoweza kutumiwa kumkwamisha mgombea, otherwise muda hautatosha kujitetea mahakamani kama ilivyokuwa kwa Wenje kule Mwanza, uchaguzi ule ulikuwa wa miezi mitatu lakini huu utakuwa wa wiki tatu tu, mahakama ikimaliza kusikiliza rufaa kabla haijatoa uamuzi uchaguzi utakuwa umekwisha, ngoma itabidi ije ianze upya!
MIBA YA MGUNGA HAIUCHOMI MGUNGA!
1. Kigezo cha kwanza, ikumbukwe kuwa ili mtumishi yeyote wa serikali aweze kugombea ubunge, ni sharti apate kibali kutoka kwa mwajiri wake, ambaye ni serikali kupita idara husika, au achukue likizo ya bila malipo ili endapo akishindwa uchaguzi arejee kazini, au ajiuzulu kazi kabisa, ili akishindwa iwe imekula kwake. Mwl Kashindye baada ya kuteuliwa kuwa mgombea wa CHADEMA alianza utaratibu wa kupata idhini ya mwajiri wake, lakini cha kushangaza ni kuwa aliwekewa ngumu kupita kiasi (sidhani kama Dr Kafumu nae kafanyiwa hivyo) ilifika mahali Mwl Kashindye kutaka kujiuzulu, lakini pia ikawa ni mtihani, kwani alitakiwa kutoa notice ya mwezi mzima, kitu ambacho hakingewezekana kutokana na muda uliopo, ikabidi maskini Mwalimu huyo aamue kujiuzulu kwa notice ya 24hrs na alipe mshahara wa mwezi mmoja, ilipofikia hapo, akaagizwa aende mkoani Tabora ili aweze kupata likizo ya bila malipo.
Alikwenda Tabora na akapatiwa likizo hiyo na barua husika inayothibitisha hivyo. Mpaka hapo kila kitu kwa juujuu kinaonekana kuwa ni sawa, KOSA! Delays alizofanyiwa Mwl Kashindye zilikuwa ni za makusudi na very tactical, kwa maelekezo ya CCM, kwani under normal circumstances hakukuwa na sababu za kufanya hivyo. Wakati akizungushwa hivyo kumbe huku Maexpert wa kuchakachua walikuwa kazini wakidesign mtego utakaofyatuka wakati wa uteuzi ukifika, CCM kupitia mgombea wake itaweka pingamizi Mwl Kashindye asiteuliwe kwa kuwa ni mtumishi wa serkali, yeye atajitetea kuwa amefuata utaratibu wa kuchukua likizo bila malipo na barua yake ndio kielelezo chake, lakini haitasaidia kitu kwa kuwa barua hiyo, ambayo utayarishaji wake ulisimamiwa na wale Maexpert, itapingwa kuwa ina mapungufu mengi hivyo haikidhi haja, kwa hivyo Mwl Kashindye ataendelea kutambulika Kama mtumishi alie kazini bado kwa hiyo atapoteza sifa za kuwa mgombea!
Kigezo cha pili ambacho kitatumika kumuengua Mwl Kashindye, Kisha mwisho Kama hakutakuwa na interruption yoyote na kama charge itabakia, basi nitasuggest namna ya kupangua, lakini naamini kwa kuanika hadharani njama hizi, basi kutavunja nguvu sana utekelezaji wake.
2. Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa. Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.
Vipengele hivi viwili visipofanyiwa kazi (Wanasheria wanajua hivyo) hata kimojawapo tu kikipita kinatosha kuleta maafa na kilio, kulalamika na mikwara mingi baada ya mzinga kulia, havitasaidia. Kwa kuwa nachukia dhulma na kupenda haki itendeke, ingawa sina mamlaka yoyote ndani ya CDM, basi naomba tu wanasheria wa CDM waikague vizuri barua ya likizo ya Mgombea, kisha waiangalie zheria inayohusiana na utaratibu wa utoaji wa barua hiyo, kama vile, je, aliesaini barua hiyo Ana mamlaka hayo? Maelezo na mihuri yake inakidhi? Chronological factors zimekaa sawa? Hakuna errors zozote (typing or otherwise) ambazo zinaweza kupotosha maana hivyo kutoa mwanya wa barua hiyo kupingwa uhalali wake?
Pili, wahakikishe kuwa ni kweli kuwa katibu wa Wilaya wa CDM Bw Christopher hakuchaguliwa katika nafasi yake kwa mujibu wa katiba ya CDM, kama ndivyo, je ni utaratibu gani ulitumika wa kumuinstall, je document zilizomuhalalisha zipo na zipo valid hadi sasa?Kila ilivyo, wanasheria wazipuuze hata chembe ya factor yoyote inayoweza kutumiwa kumkwamisha mgombea, otherwise muda hautatosha kujitetea mahakamani kama ilivyokuwa kwa Wenje kule Mwanza, uchaguzi ule ulikuwa wa miezi mitatu lakini huu utakuwa wa wiki tatu tu, mahakama ikimaliza kusikiliza rufaa kabla haijatoa uamuzi uchaguzi utakuwa umekwisha, ngoma itabidi ije ianze upya!
MIBA YA MGUNGA HAIUCHOMI MGUNGA!