Vigezo na masharti kwa wanaotafuta wachumba JF

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
1. Waweke picha.
Tena zionyeshe pande zote, mbele nyuma, kwa pembeni. Kwenye hiyo picha isiwe umefanya make-up (wadada sanasana), na picha ziwe recent - not more than one month tangia zimepigwa

2. Waweke CV
Humo waonyeshe experience yao kwenye mapenz, aliwahi kubreak mioyo ya wangapi, nae alishabrekiwa mara ngapi.

3. Naomba memba muongeze vigezo.

Nasema hivi maana miezi michache iliyopita nilirespond kwenye tangazo la huku lakini kilichonikuta imebaki kuwa siri yangu...
 
Jamani jamani!!! Pole mwaya si ndio changamoto zenyewe hizo, lazima ukutane na pumba na ngano halafu upitishe mchujo upate mwenyewe. Kumbuka ukitupa nyavu baharini, wanaingia nyoka, minyoo,takataka za aina mbalimbali na samaki wenyewe wakubwa na wadogo lakini mwisho wa siku unabakia na samaki wako wazuri!! So usikatishwe tamaa na hayo.

Ila pia bado naamini mumu/mke mwema hutoka kwa Mungu. Tengeneza vizuri uhusiano wa na Mungu utafanikiwa tu!!
 
Jamani jamani!!! Pole mwaya si ndio changamoto zenyewe hizo, lazima ukutane na pumba na ngano halafu upitishe mchujo upate mwenyewe. Kumbuka ukitupa nyavu baharini, wanaingia nyoka, minyoo,takataka za aina mbalimbali na samaki wenyewe wakubwa na wadogo lakini mwisho wa siku unabakia na samaki wako wazuri!! So usikatishwe tamaa na hayo.

Ila pia bado naamini mumu/mke mwema hutoka kwa Mungu. Tengeneza vizuri uhusiano wa na Mungu utafanikiwa tu!!

Umenikumbusha wimbo wa Mwaitege anasema mke mwema anatoka kwa bwana. Siku jamaa anaargue , sasa kama anatoka kwa bwanaake, huyo ni mke mwema kweli? lol...
 
Waeleze kama walishawahi kuua(ke) au kushiriki mauaji(me) na ni mara ngapi ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom