Vigezo anavyotumia Rais Magufuli kuteua majaji wa Tanzania vinatia shaka, vinaondoa heshima kwa majaji

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,129
18,740
Rais ana mamlaka ya kuteua jaji, hilo hakuna anaepinga. Lakini linalotia shaka ni vigezo vinavyotumika hadi Rais kuamua kuteua mtu fulani kuwa jaji. Sasa hili haliwezi kuwa jambo la ksiasa, au hisia tu za Rais kuhusu anampenda nani au hakimu gani kamfurahisha hadi aamue kumteua kuwa jaji. Rais anapaswa kufahamu wazi kwamba uteuzi wa mtu kuwa jaji haupaswi kufanywa bila kuzingatia vigezo vinavyostahili, au kuteua mtu kuwa jaji kama vile kumzawadia kwa jambo fulani alilofanya.

Kama vigezo hivyo havipo basi ni wakati muafaka wa kupigania viwepo ili kumwongoza Rais katika kufanya uteuzi wa majaji. Na kama vipo lakini Rais anavipuuza katika kuteua majaji basi tunapaswa kutafuta namna moja au nyingine kuzuia hili, ikiwezekana hata kada za sheria kuitisha mgomo dhidi ya majaji wanaoteuliwa kimazingaombwe.

Enzi za awamu ya kwanza jaji alikuwa ni mtu mwenye kuheshimika sana, akiwa nje na ndani ya mahakama. Nakumbuka tulivyokuwa tunawaheshimu majaji kama Korosso, Mapigano, Ruhumbika, Maina nk. Siku hizi baadhi ya majaji wanaonekana kama makanjanja tu, yeboyebo, watu walioteuliwa kwa vigezo vyenye kutilia shaka, au pengine hata kutokana na ushabiki wao wa kisiasa.

Tusipokuwa waangalifu na suala hili basi tutaishia kuwa na mfumo wa mahakama Tanzania ambao si tu utakuwa hautoi haki za kisheria bali pia utakuwa ni kichekesho cha ulimwengu. Tutakuwa na taasisi ya sheria ambayo itakuwa inawadharau baadhi ya majaji. Haya ni mambo ambayo wadau wa sheria nchini, pamoja na TLS, wanapaswa kuyapigania kwa kila namna, badala ya kuona gari la sheria nchini linaenda kutumbukia shimoni na kuamua kutofanya lolote kwa kuwa Rais Magufuli hapangiwi na mtu. Huo ni utumwa mamboleo wa kifikra. Magufuli ni Rais wa Tanzania, sio Tanzania ni ya Rais Magufuli. Kama haelewi hili anapaswa kueleweshwa kwa namna moja au nyingine.
 
Ukiisoma sentensi moja ya hukumu ya Hakimu Mteite aliyemfunga Sugu..jpm anaetaka kumpa ujaj..i lazima uombe maji ya kunywa.
 
Ukiisoma sentensi moja ya hukumu ya Hakimu Mteite aliyemfunga Sugu..jpm anaetaka kumpa ujaj..i lazima uombe maji ya kunywa.
Hivi ile ndio hukumu ya Sugu, nimeiona! Hivi unawezaje hata kufanya reference kwenye ile hukumu? Na kwa nini Sugu hakukata rufaa? Hukimu anatoa hukumu based na "I thin" badala ya vifungu vya sheria!!!
 
Hivi ile ndio hukumu ya Sugu, nimeiona! Hivi unawezaje hata kufanya reference kwenye ile hukumu? Na kwa nini Sugu hakukata rufaa? Hukimu anatoa hukumu based na "I thin" badala ya vifungu vya sheria!!!
Mkuu ndio ile hukumu ya Sugu..
Haikuwa hukumu ila ni takataka.
 
Mashauri from hakimu to judge- criteria- Shughulikia Mbowe hadi anyee ndoo! tunakuongezea na 25m.
Grrrrrrrrrrrrrr! Jiwe must go before we are screwed as a nation!!!!
 
Majaji wa UPE
Nahisi hata kati ya majaji kwa majaji watakuwa na "judge classification", jaji wa Nyerere (kama bado wapo), jaji wa Mwinyi, jaji wa Mkapa, jaji wa Kikwete, na jaji wa Magufuli.

Utasikia jaji anasema "umesoma hukumu ya jaji so and so, yaani ni rubbish" Jaji mwingine anajibu si jaji wa Magufuli yule, unashangaa nini!
 
There is a need to change our judicial system to form . judicial commission which will be responsible for choosing chief justice and judges basing on raid down qualifications instead of choosing a judge basing on simple trivial merits.Judicial Commission should not be out weighted by Executive pillar
 
Back
Top Bottom