Vifo vya watoto usingizini: Uchawi au ujinga…?

Nimesoma na nimeguswa sana! Mwaka huu mwanangu alifariki mara tu baada ya kuzaliwa na mama yake hakuiona hata maiti ya mtoto wake! Hapa nilipo machozi yananilengalenga!

Mimi pia mwanangu alifariki masaa machache kabla hajazaliwa kwa kweli nikiona mtoto au nikisikia habari za vifo vya watoto inanikumbusha machungu. Mungu tusaidie wote tuliopitia wakati kama huo tusipite tena si kama tupendavyo bali uypendavyo wewe.
Ombi moja kwa Mtambuzi, naomba kama una uelewa wowote kuhusu Pressure ya ujauzito ( PIH) unipe msaada maana ilikuwa ndo chanzo cha kumkosa mtoto na siku hizi tatizo hili limeondoa kina mama wengi sana.
Naomba kuwasilisha hoja.
 

Kwani Mungu si yupo Mtambuzi??basi na shetani yupo vile vile..tena huku Africa ndio tumemvaa tele..

Mimi naona kama ambavyo sio vifo vyote vya watoto vinatokana na ulozi, sio vyote vinatokana na uzembe wa uleaji vile vile...wengine mama zetu walianza kulea watoto mwaka 1971 huko, tena huko vijijini kusiko na mazingira mazuri ya ulalaji, vyakula etc na hakuna hata mmoja wetu aliyedhurika...iwe leo kwa kiasi kikubwa hivo??

Ulozi upo...na wabongo tumeuendekeza kweli kweli..asiyeamini asiamini, ila aamini kitu kingine kitakachomlinda nao
 
Last edited by a moderator:
Thanks kutupa somo i hope akina dinnah na gea wataitangaza redioni mwao na waandishi wa magazeti wameinyaka na wataipublish kny magazeti yao ili habari iwafikie wider audiance ili na sie tupunguze hivyo vifo kwa asilimia hamsini km wenzetu
 
Bwana MTAMBUZI umenipa kitu ambayo sijawai ipata darasani wala mtaani, hakika jf ipo juu. ukizingatia I am expected kuwa baba, so me and ma wife tutazingatia elimu hii ya bwelele.
 
hello,wana jf niko na furaha saana kujiunga na hili jamvi la wenye busara na wanaotaka kupunguza na hata kuondoa kabisa wale maadui wetu watatu (ujinga, umasikini na maradhi). Bwana MTAMBUZI umenipa kitu ambayo sijawai ipata darasani wala mtaani, hakika jf ipo juu. ukizingatia I am expected kuwa baba, so me and ma wife tutazingatia elimu hii ya bwelele.
 
Nashukuru sana wana JF, kwani hayo yamewahi kunitokea. Na kweli alikuwa mtoto wa kiume. Kwa vile mimi na mke wangu ni wamini MUNGU hakuna mchawi yeyote tuliye hisi. Idd Amini alikuwa akipenda kusema thank u very much, nami pia nasema THANK U VERY MUCH KWA MTOA MADA HII.
 
Back
Top Bottom