Nicas Mtei
JF-Expert Member
- Dec 21, 2010
- 11,556
- 7,082
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
kweli mkuu ni vizuri kuwe na elimu angalau kuanzia shule msingi ili vijana wetu wakue wakiwa na upeo mkubwa kuhusu jambo hili.Nakubaliana na wewe mkuu, na mtu kama Dr. Riwa anahusika sana.............
Mimi nilishauriwa na Dr. pale Morocco kwa Massawe lkn siyo Masawe ni mwingine ana jina la kiislamu, kuwa hiyo ni mbaya kwani inaathiri IQ ya mtoto kasema nisimpe. alishauri mama yake amnyonyeshe akiwa amekaa na akaaonyesha jinsi ya kumshika mtoto( hivyo mtembelee, si rahisi kuonyesha hapa), pia akashauri kuakikisha mtoto anacheua baada ya kunyonya, alishauri mimi (baba yake) nimbebe kifuania kwani kipo flat, baada ya haya tatizo lilipunguaMtoto tunamcheulisha sana, na sasa tumeamua kutumia dawa inaitwa 'infacol'
Chali ni kulala kwa kutumia sehemu ya nyuma ya mwili i.e kulalia mgongo wakati kifudifudi ni kujilaza kwakutumia sehemu ya mbele ya mwili yaani unalalia tumbo ,na ndio maana ni rahisi kwa mtoto kuishiwa hewa haswa hao ambao hawawezi kujigeuza maana wawezakaweka uso kiupande lkn katika kuhangaika ndo hivyo tena anawezalalaia hata uso ambao unainlude puaSamahani chali na kifudifudi ina tofauti gani?
hata mimi ndo naisikia leo kuwa ulalaji wa chali ni salama pia....Dah, hadi niiformat brain yangu niamini chali ni salama kwa mtoto si leo.
Sie tulikuwa tunafundishwa kumlanza mtoto kifudi fudi, afu kichwa kinalazama pembeni, kwa usalama wake.
Kuna watoto ambao hucheua wakiwa usingizini, kama kalala chai uwezekano wa kupaliwa ni mkubwa, ila kama kalaa kifudifudi mcheo hutoka.
Anyway, kama utamlaza mtoto chali, basi hakikia umemcheulisha baada ya kunyonya.
Ila kwa mie, mtoto halali mbali na mie, eti nimemlaza chumba cha nane mie niko sebuleni, hapana kama nina kazi bora nimbebe mgongoni niendelee na shughuli zangu.
Mtoto mtamu jamani.
Mtambuzi, nakubaliana na wewe kabisa. Watoto wengi wanasumbuliwa na lishe duni, mie hata 'kubemenda' nakuhusisha na kwashiorkor ama marasmus
Afu wamama wabishi tu, ila mtoto akinyonyeshwa maziwa ya mama bila kula kitu kingine kwa miezi 6 ya mwanzo, angalau basi minne haugui na afya yake inaimarika mno.
itabidi Mtambuzi utueleweshe vizuri zaidi, kumbe siko peke yangu nayeamini kulaza kifudifudi.
Umewasikia FP na nyumba kubwa pia.
jamani kama mtoto unamtaka, mimba ikiharibika hata wa wiki 1, roho inauma sana! nilipata two miscarriages za miezi mi3 na mi4! nikuwa nalia kama nimefiwa mtoto kabisaaaaaaa, yaani ndugu zangu walikuwa wanapata kazi ya ziada kunibembeleza!! ndio MUNGU akanizawadia twins baada ya hiyo misuko misuko!
kwa kweli kulea watoto chini ya mwaka mmoja ni ngumu, na inahitaji ulezi wa mama mwenyewe na si hausgal, kama mama yupo na ni mzima, jamani tujitahidi kulea wenyewe, hausgal awepo tu kama msaidizi, kufua, kuchemsha vyombo vya watoto etc! nilipopata twins, niliacha kazi!! for two years nimelea mwenyewe!! wanaanza baby class wana miaka mitatu, ndio na mimi nikarudi kazini!
hii ilinipunguzia kuuguza mara kwa mara! maana nasimamia kila kitu mwenyewe, neti ziwe safi, chupa zifungiwe kwenye container, no mbu wala inzi chumbani kwa watoto, maji ya kunywa ya watoto yachemshwe etc!!
kuhusu kulala watoto, kwakweli walipokata kitovu tu, niliwaanzisha kulala kifudifudi, ila nahakikisha hakuna nguo yoyote pembeni, namlaza juu ya godoro bila shuka, vile vigodoro vya watoto, mpaka walipozoea nadhani mwaka mmoja na nusu, ndio nikaanza kutandika mashuka! ila ukimlaza kifudifudi analala zaidi kuliko ukimlaza chali!!
MUNGU WETU AWALINDE WATOTO WETU WAKUE, WATUZIKE! Amen!
amen darling. A big Amen na pole kwa misukosuko ulopata. You have really inspired me.
Unayoyasema kuhusu hali duni ya uchumi na makazi duni kusababisha vifo vya aina hiyo nakubaliana na wewe.
Nakumbuka miaka ya 80 wakati naisha Mwananyamala vifo vya wa watoto wachanga vilikuwa vinatokea sana na watu walikuwa wanashikana uchawi ile mbaya.
Baada ya kusoma huo utafiti ndio nikagundua kwamba ule ulikuwa ni ujinga tu. Kunahitajika elimu hii itolewe wakati kina mama wanapohudhuria kliniki............