Vifo vya Samaki Mto Mara: Taarifa ya Kamati ya Jaffo inakinzana na taarifa ya awali ya Mamlaka ya Bonde la Mali la Ziwa Victoria

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,968
Taarifa ya Kamati ya Jaffo inakinzana na taarifa ya awali ya Mamlaka ya Bonde la Mali la Ziwa Victoria.

Mamlaka ya Bonde walidai utafiti wa awali wa kimaabara unaonyesha uwepo wa mafuta kwenye maji. Kamati ya Jaffo inasema ni kinyesi (tani 1.8) & mkojo (Lita 1.5 bilioni) wa mifugo pamoja na maozo ya mimea.

Taarifa hizo mbili haziwezi zote kuwa za kweli ni dhahiri moja wapo ni ya uongo. Nani anadanganya? Mwenye akili na afikiri.

Pia, muhtasari wa taarifa ya kamati, kama ulivyosomwa leo, unaeleza kuwa Barrick North Mara hawahusiki na uchafuzi huo.

Swali la msingi ni je, kwanini taarifa ije na utetezi wa mgodi moja kwa moja?, je, kuchunguza kama mgodi unahusika ilikuwa ni moja ya hadidu za rejea?

Taarifa ya Kamati ya Jaffo inaeleza kuwa video za samaki waliokufa na kuelea kwenye maji meusi sio za Mto Mara. Swali ni je, ni video za wapi? Kama ni Tanzania, kwanini zikaliwe kimya?

Pia, nani anawajibu wa kufuatilia ubora wa maji ya Mto Mara? Alikuwa wapi kwa miezi 8 mpaka kinyesi cha mifugo kimechafua mto? Usalama wa Mito mingine nchini iliyoko kwenye jamii za wafugaji ukoje?

Tuna maswali mengi ya msingi; tutauliza wakati sahihi na wakati sahihi u mbioni, umekaribia.

Pia, soma;

Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini
 
Taarifa ya Kamati ya Jaffo inakinzana na taarifa ya awali ya Mamlaka ya Bonde la Mali la Ziwa Victoria.

Mamlaka ya Bonde walidai utafiti wa awali wa kimaabara unaonyesha uwepo wa mafuta kwenye maji. Kamati ya Jaffo inasema ni kinyesi (tani 1.8) & mkojo (Lita 1.5 bilioni) wa mifugo pamoja na maozo ya mimea.
Kwa sababu bonde ndio wataalam wa maji basi nitafwata taarifa ya bonde.

Swali la kujiuliza, kwann iundwe tume wakati bonde walisha fanya au walikua wanafanya utafiti wao?
 
Na kinachoniuma hiyo kamati ishapiga pesa za maana na kuja na majibu mandazi km haya.Ndo huku tushafika km taifa kila kitu ni tume
 
Kinyesi cha Ng'ombe ni vigumu kufika kwenye maji ya mto kina Decomposer wengi....Mtu kala mlungula hapa
 
Tujiulize maswali kadhaa kabla hatujaendelea sana
1. Hao mifugo huwa wanajisaidia kinyesi chao mtoni ?
2. Hao mifugo huwa wanakojoa hump daima.
3. Kama Khali ni hii mito mingine Iko katika hali gani?
Ni vizuri wasomi wetu wekatumia usomi wao kuliokoa taifa hapa Kuna uwezekano mkubwa wa kumkumbuka Mbunge wa jimbo la Geita vijijini Mhe Joseph Kasheku Msukuma huwa anaimba Kila Leo wasomi wetu hawalisaidii taifa
 
Nawahurumia sana watanzania..kwa aina za viongozi na wasomi wa nchii...ambao wanaamini na kuwategemea.

#MaendeleoHayanaChama
 
Taarifa ya Kamati ya Jaffo inakinzana na taarifa ya awali ya Mamlaka ya Bonde la Mali la Ziwa Victoria.

Mamlaka ya Bonde walidai utafiti wa awali wa kimaabara unaonyesha uwepo wa mafuta kwenye maji. Kamati ya Jaffo inasema ni kinyesi (tani 1.8) & kojo
Mto Mara siyo kuwa uko Tanzania peke yake huu mto unaanzia Kenya palee Mlima Kenya Je kwa nini samaki wetu tu ndo wafe na wale wa kenya hawafi??.....Ok!! mifugo yetu tu ndo ina kinyesi sumu ya Kenya hapana si ndiyo!! kwani majani ni tofauti??

Yaani ningekuwa karibu huyo prof ningemzaba kibao faster nifungwe! mnabahati mnafanya kwa siri siri vikao vyenu vya kijinga ivo!
 
Hivi kinyesi na mikojo ya Ng'ombe inauwaje samaki? Yani ni sumu? Nahama Tz aisee
Kama kinyesi ni kina sumu kingeanza kuua biringisa mavi wale wadudu wanao sukuma mavi ya ng'ombe wale!....na wakurya wangekufa sana maana wao wanakula kinyesi cha ng'ombe wanakiita kichure! muraaa!!

Prf kajikoroga sana hata!! hajui kudanganya....tatizo prof mzaramo hakujua wenzake mara kinyesi cha ng'ombe ni lishe mwanana! maarufu km kichure!
 
Masikini akisoma kidogo tu tena kwa shida km zooote anaona wenzake wooote ni wajinga!.......pia maskini anadhania huko serikalini ni uongo uongo tu! huyu alisoma ili ale!!!!!
 
Back
Top Bottom