tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,793
- 18,216
Awali ya yote natoa pole kwa familia za Lemtuz na Membe kwa kuondokewa na wapendwa wao. Kifo ni fumbo kubwa. Vifo hivi vimetokea ghafla, hasa kipindi hiki ambacho baridi imeanza kukolea.
Le Mutuz na Membe wakati wakiwa hai (Chanzo:Mtandao)
Kwa mujibu wa daktari wa familia, kifo cha Membe inasemekana kimesababishwa na virusi vilivyoshambulia mfumo hewa vilivyopelekea damu kuganda. Na kama tujuavyo, virusi huwa active zaidi wakati wa baridi, kama ilivyowahi kutokea mwaka 2019.
Taarifa za kifo cha Lemtuz hazijaeleweka vizuri lakini nimesikia tetesi kuwa alikuwa na shida ya moyo. Na kwa kuwa virusi hushambulia zaidi wazee na watu ambao afya zao zimedhoofishwa na magonjwa mengine, sasa naanza kuunganisha nukta kuwa ipo haja ya watanzania kuendelea kuchukua tahadhari, kama tulivyowahi kuchukua siku za nyuma, hasa wakati huu tunapoisogelea miezi ya baridi (Juni na Julai).
Turejee utamaduni wetu ule tuliofanya kipindi kile ili kuokoa afya zetu na tumuombe Mungu aendelee kutupigania kwa kuwa Yeye ndiye muweza wa yote. Amina.
Nawasilisha.
Kwa mujibu wa daktari wa familia, kifo cha Membe inasemekana kimesababishwa na virusi vilivyoshambulia mfumo hewa vilivyopelekea damu kuganda. Na kama tujuavyo, virusi huwa active zaidi wakati wa baridi, kama ilivyowahi kutokea mwaka 2019.
Taarifa za kifo cha Lemtuz hazijaeleweka vizuri lakini nimesikia tetesi kuwa alikuwa na shida ya moyo. Na kwa kuwa virusi hushambulia zaidi wazee na watu ambao afya zao zimedhoofishwa na magonjwa mengine, sasa naanza kuunganisha nukta kuwa ipo haja ya watanzania kuendelea kuchukua tahadhari, kama tulivyowahi kuchukua siku za nyuma, hasa wakati huu tunapoisogelea miezi ya baridi (Juni na Julai).
Turejee utamaduni wetu ule tuliofanya kipindi kile ili kuokoa afya zetu na tumuombe Mungu aendelee kutupigania kwa kuwa Yeye ndiye muweza wa yote. Amina.
Nawasilisha.