Vifo Tabora: Uongozi wa NSSF Makao Makuu Uwajibike

Gembe umenena!!!Hilo nadhani hata mwanakijiji ndilo alilokuwa anajaribu kusema lakini kimtindo,MWISLAM!!!gEMBE UMENENAAAAAA!!!!NA KILA ANAPOKAA MWISLAM BASI HAPAISHI SHUTUMAAAA KWA SABABU TU MWISLAM,SASA NCHI HII MNATAKA MUONGOZE PEKEE YENU???
 
Sijauona huo mkataba. Wewe umeuona?

Matumizi ya jengo hayategemei mkataba. Mabadiliko ya matumizi makubwa kama haya ni lazima landlord ahusishwe. Hii haikuwa private party inayotokea mara moja kwa mwaka. Huyu mpangaji amegeuza sehemu aliyopanga kuwa disko kwa zaidi ya miaka miwili. Mara mbili ajali zimetokea kwenye eneo bado mnasema landlord ni innocent? Mbona unawaingiza polisi kwenye hili? Polisi wanahusika vipi? Huko kwenu, kila kwenye disko kunakuweko na polisi? Ingekuwa hivyo basi wasingekuwa wanafanya kama tenda ya ziada katika wakati wao binafsi. Hili lilikuwa disko la kawaida lenye theme ya Disko toto. Polisi wangeendaje bila kualikwa na mwenye disko? Mbona hamwataji TRA? Si na wao wanatoa leseni kama wanavyotoa manispaa? Kinachogomba hapa na ambacho ni wajibu wa manispaa peke yake ni kibali cha matumizi ( au ndiyo mnaita leseni). Kwenye majengo ya "public" inabidi idara ya zimamoto na yenyewe itoe baraka kuhakikisha kuwa tahadhari zote zimechukuliwa. Kama mabadiliko ni makubwa kama haya ( kutoka matumizi binafsi kwenda public) inabidi muombaji aambatanishe na michoro ya kuonyesha mabadiliko hayo( kupanua milango, kuongeza ngazi, kuweka sprinkler systems n.k.). Hauwezi kufanya yote haya bila ridhaa ya mwenye jengo.

Kwa vile hatufanyi hivi na vibali vinatolewa kama pipi, hakubadilishi sheria.

Kwangu mimi kuwajibika ni pamoja na mwenye jengo kuchunguzwa. Ndiyo maana ingekuwa busara kwake kuanza mwenyewe kufanya uchunguzi ndani ya oganaizesheni yake kujua wapi walikosea na kuweka system ili janga kama hili lisitokee tena.

Kwa maana hiyo basi kwa fact hizi za leo,line of responsiblity inagawanyika sehemu mbili kati ya waendeshaji disco kama occupiers kwa kushindwa kuthibiti idadi ya watoto waliomo ukumbini na kuchukua tahadhari muhimu,mf.uwepo wa paramedic jirani kwa first aid,na nssf kama co-occupiers kwaajili ya kuhakikisha hitilafu zote ukumbini humu zinakuwa rectified kabla ya kumpa mpangaji (hapa seria inayotumika ni ile ya ardhi ya mwaka 1999 inayotoa detailed analysis ya majukumu ya landlord and tenant).FACT TOKA KWENYE SHERIA Hiyo zitatumika kuibana nssf,hata hivyo hazitamuoindolea responsibility muendesha disco kwa kuwa alichangia vifo vya watoto kutokana na omission yake ya kutotake responsibility on his part.9HII INAITWA CONRIBUTORY NEGLIGENCE)

Wakati katika criminal law,kuna kanuni inaitwa "THE DOCTRINOF CAUSALITY OR THE DOCTRINE OF CAUSATION".Hii itatumika endapo police wataamua kuwafikisha wahusika mahakamani kwa kusababisha vifo bila kukusudia yaani manslaughter.
 
2008-10-03 12:39:23
By Bilham Kimati



My Take:

Now I know kwanini NSSF iliwahi kutoa rambirambi na kwanini Mkurugenzi wake alihakikisha anatokea mazikoni. Kumbe wapiga disko hawakuwa wapangaji wa kudumu wa ukumbi huo. Waliukodii kwa siku hiyo tu. Na sasa najua kwanini mtu mmoja humu hataki Dr. Dau na NSSF iguswe. It make a whole lot of sense. Hakuna mkataba kati ya kina Patel na NSSF ni makubaliano tu, at least that is the initial info.


Nilichelea kidogo kwa kuwa sikuona uwajibikaji wa Dau lakini nimegundua kuwa hafanyi lolote pale NSSF. Nashawishika kuwa NSSF ni kichaka.

He must go......
 
at least sasa unaanza kuonyesha wisdom lakini huyo aliyeanzisha hili balaa naona kaamua kuuchuna na mijigambo yake kisa eti yuko Detroit. Hivi nani kamwambia kuwa Detroit mbali?

Dunia ya leo kama kuna ishu ni kukutana na kufanya naye small tea talk sidhani kama kuna haja ya mtu kwenda kule physically, unaweza ukactivate jamaa tuu kule kisha atakunywa naye hiyo chai ya saa kumi kisha bas

ES i can assure you Slander na innuendos si kwa Dr Dau tuu bali sasa hivi ni all out war kwa hizi supermarket Journalism anazotuletea Mwanakijiji humu maana sie wengine tushachoka na mwenyewe hilo analijua


enough is enough and i really care less sasa hivi unajua

kwanini hiwe hivyo, ni uandishi wake tu ambao unakufanya wewe ufikie hata kusema hayo? ama kuna ambayo atuyajui?
siamini macho yangu kama kweli sisi tumefikia kuwa hivyo
 
at least sasa unaanza kuonyesha wisdom lakini huyo aliyeanzisha hili balaa naona kaamua kuuchuna na mijigambo yake kisa eti yuko Detroit. Hivi nani kamwambia kuwa Detroit mbali?

Dunia ya leo kama kuna ishu ni kukutana na kufanya naye small tea talk sidhani kama kuna haja ya mtu kwenda kule physically, unaweza ukactivate jamaa tuu kule kisha atakunywa naye hiyo chai ya saa kumi kisha bas

ES i can assure you Slander na innuendos si kwa Dr Dau tuu bali sasa hivi ni all out war kwa hizi supermarket Journalism anazotuletea Mwanakijiji humu maana sie wengine tushachoka na mwenyewe hilo analijua


enough is enough and i really care less sasa hivi unajua


Acheni vitisho vya kitoto hivi. Wabongo bwana! Kumtetea Dr masau kwa sababu tu ni ayatollah. Mtakumbatia dini kandamizi hizi mpaka lini?
 
Heshima zako zipo noted nami nakurudishia zinazokustahili.
Nashukuru sana kwa clear case ya namna hiyo.Katika historia ya common law ambayo hata marekani inatumika japo with modifications,kuna sheria kuu mbili zinazoweza kutawala mazingira haya tunayoyazungumzia,ya kwanza ni jinai na ya pili ni sheria ya madhara(yaani law of torts).Sheria hizi zimekuwa zikitumika sana duniani na effect zake ni very serious compared na sheria nyingine yoyote ile.Naweza kusema katika construction industry kwa upande wa responsibility hizi ndio sheria mama.
Katika makosa ya jinai, te main principle ni kwamba ili mtu awe ametenda kosa au kutiwa hatiani lazima vitu viwili vioane yaani tendo(actus reus) na nia ya kutenda kosa ambayo huwa tutaiita nia ovu(ill will au kwa lugha ya kitaalamu mens rea).Na kwa maana hiyo basi kanuni ni "actus non facit reum nisi mens sit rea" [which means that "the act does not make a person guilty unless the mind is also guilty"] kwa maana no one will be held responsible unless there is a meeting(concurrence) of the act and the mind(kwa lugha rahisi),kwa maana hiyo basi kitu kigumu katika kuthibitisha makosa ya jinai sio tendo bali ni kuoanisha nia na tendo.
Katika kesi iliyopo mbele yetu,kitendo ni kufa kwa watoto,lakini nia bado hatuijui(kwa maana kwamba je,kulikuwapo na nia ya kuua hao watoto?).Nia hiyo yaweza kuwa implied wakati mwingine kutokana na omission(yaani kuzembea kuchukua hatua kwa mtu mwene wajibu wa kufanya hivyo).Ndio maana basi ili kuthibitisha nia ovu prosecution mara nyingi inaipata mens rea kwa kuangalia kama kulikuwa na 1.recklessness 2.conduct or omission 3.intention au intent 4.negligence.

Nimebold maneno negligence na recklessness kwa maana nzuri tu.Kwa sisi waswahili tutasema kwamba recklessness na negligence ni uzembe lakini sio kweli,hivi ni vitu viwili tofauti.Recklessness ni upuuzi au papara wakati negligence ni uzembe.Sasa upuuzi au papara maana yake nini?lini mtu anakuwa mpuuzi(reckless).Upuuzi ni pzle ambapo mtu anaona kitu na anajua madhara yake lakini hachukui hatua au anasema hata ikitokea ni ajali kazini.Mathalani unataka kwenda kazini asbh unajaribu gari unaona halina breki sawasawa lakini unasema anyway tutafika tu ngoja niende hivyo hivyo,hii ni recklessness na upo responsible.

Sasa kwa upande wa nssf tujiulize walikuwa reckless?au je,ni mpangaji wa ukumbi ndio alikuwa reckless?

Negligence,ngeligence nayozungumzia hapa sio civil negligence bali criminal negligence.Negligence maana yake ni kutochukua hatua za tahadhari hata kama hukujua matokea ya tendo lako,jambo la msingi ni kuwa ulikuwa na wajibu na hukutimiza wajibu.Mathalani umejifunza udereva vema na umeendesha labda hata miaka 5,lakini asubuhi wee unaondoka tu na gari hucheki oil,wala breki wala kama kuna loose nuts zozote hutake precaution yoyote,unaondoka huu ni uzembe na ukipata ajali au tatizo lolote you are criminally responsbile.
The test ya criminal negligence ni kwamba "a reasonable person with the same abilities and skills as the accused would have foreseen and taken precautions to prevent the loss and damage being sustained". what or who is a reasonableman is a question of fact,to be determined by court.

Tukirudi kwenye mada je,nssf walikuwa na criminal negligence kama reasonable men?nawaachia ninyi wadau.
N.B.Kesi nyingi za majengo kuanguka dar,polisi hubase katika criminal negligence kuwafikisha watu mahakamani.sasa sijui hawa wa huko Tabora inakuwaje.
MATOKEO YA PROCESS HIYO YAPO JUU NI KIFUNGO AU FAINI AU VYOTE KWA PAMOJA


CIVIL OR TORTIOUS NEGLIGENCE.
Civil negligence imekudefined kama "The breach of a legal duty to take
care, resulting in damage to the claimant which was not desired by the defendant" au Negligence is the omission to do something which a reasonable man, guided upon those considerations which ordinarily regulate the conduct of human affairs, would do, or doing something which a prudent and reasonable man would not do"

MATOKEO YA KESI ZA NAMNA HII SIO KIFUNGO BALI NI MALIPO YA FIDIA KWA MAPESA MENGI,KAMA NI KAMPUNI INAWEZA HATA KUFILISIWA.LAKINI ILI USHINDE TORT OF NEGLIGENCE UNATAKIWA KUTHIBITISHA YAFUATAYO
1.Kwamba "the defendant had a duty"(mdaiwa alikuwa na wajibu kisheria)
kivipi?ili kuestablish duty maswali ya kujiuliza ni haya
a.Whether the consequences of the defendant's act were reasonably foreseeable
b.Whether there is a relationship of proximity between the parties, ie a
legal relationship or physical closeness
3.Whether in all the circumstances it would be fair, just and reasonable
that the law should impose a duty.
kama majibu yote ni yes basi unaenda hatua ya pili


2.Wajibu huo hakuutekeleza au alikiuka wajibu huo(breach of duty)
The Standard Expected
Negligence is falling below the standard of the ordinary
reasonable person. Specific rules apply if the defendant is
a child, a learner or a professional:Mahakama itafikiria
a.The degree of risk involved and likelihood of harm occurring
b.The seriousness of harm. Sometimes, the risk of harm
may be low but this will be counter-balanced by the gravity of harm to a particularly vulnerable claimant
c.The practicability of taking precautions. The courts expect people to take
only reasonable precautions in guarding against harm to others.
d.The social importance of the risky activity.If the defendant's actions served a socially useful purpose then he may have been justified in taking greater risks.
The claimant must produce evidence which infers a lack of
reasonable care on the part of the defendant. However, if no such
evidence can be found, the necessary inference may be raised by
using the maxim res ipsa loquitur, ie the thing speaks for itself


3.Uthibitishe madhara yaliyotokana na mdaiwa kutotekeleza wajibu wake(DAMAGE CAUSED BY THE BREACH) mf.madhara huko tabora ni kupotea kwa maisha ya watoto.Ukishindwa kuthibitisha madhara kunakuwa hatuna tort.

Baada ya kuyafanyia kazi mambo hayo hapo juu,basi ndio unaweza kuconclude kwamba fulani anatakiwa kuwajibika katika sheria ya madhara.SASA SWALI LA KUJIULIZA NI JE,NSSF MASWALI HAYO YANAWAINGIA ILI WAYAJIBU?
Tort of negligence inahusisha mambo mengi sana ikiwamo professional negligence

SHERIA nyingine ndogondogo zinzoweza kumwajibisha mtu katika mazingira haya ni pamoja na administrative law ambayo inategemea na specific piece of legislation inayoestablish na kudisestablish madaraka ya mtu husika.lakini effect hapa ni kufukuzwa kazi tu,kujiuzulu ama kushushwa cheo lakini sio kwenda mahakamani.[hii inawahusu zaidi watendaji walioko kwenye utumishi wa umma]

Kanuni nyingine ya responsibility hapa ni political au ministerial responsibility ambayo hii inawahusu mawaziri,ambapo madhara yake ni waziri kujiuzulu tu basi.watoto wamekufa,waziri anajiuzulu,so what?imekwisha au kama sivyo basi mamlaka husika,na hapa kwetu polisi wampeleke mahakamani criminally ambapo ataishia kufungwa,kulipa faini au kuachiwa huru.Lakini hawawezi kumshitaki kwenye tort kwa kuwa hawana mamlaka hayo,wenye mamlaka hayo ni ndugu wa wafiwa.

Ndugu zangu hayo ndiyo maeneo makuu manne yanayotawala vifo hivyo vya TABORA ksheria.
ANGALISHO:
Kwenye tort of negligence hasa occupiers liability,inamtaka mtu awe makini na mazingira yake ili yasilete madhara kwa wengine.Mfano,ukijenga nyumba ukaweka madirisha ukazungushia waya wa umeme ili majambazi wasing'oe nondo,lazima uweke bango kwa tahadharisha kuwa kuna umeme,ili wakija wawe makini,usipoweka wakanaswa wakafa,bado mwenye nyumba upo responsible kwa kusababisha kifo kwa uzembe.Mazingira yako hayakuwa secure enough for visitors.you must always anticipate visitors.
Visitors hapa ni pamja na watoto wadogo,majambazi,kama una watoto wa kike teenagers,wanaume wanaokuja kuwatongoza nao ni visitors ili wanaporuka ukuta wasiumie,na watu wowote unaowaalika kwenye sherehe nyumbani kwako.And that is the reason why ukipita sehemu nyingi utakuta zimeandikwa "MIND YOUR HEAD",MIND YOUR FEETS,SLIPERY FLOOR,MBWA MKALI,ELECTRIC FENCE,DANGER,CCTV IN OPERATION NK.Huu ni wajibu unaotokana na law of torts(sheria ya madhara).kwa faida tu ya wanaopenda kusoma naambatanisha na OCCUPIERS LIABILITY ACT YA TANZANIA

NAOMBA KUWASILISHA.

Mkuu sioni Dau anahusika vipi wakati sheria ya occupiers liability inampa liability mwendeshaji wa ukumbi na sio mmiliki wa jengo.Ingekuwa watoto wamekufa kutokana na kitu kudondoka katika jengo hilo yaani fault ya jengo inayotokana na ubovu wa miundo mbinu ulisababishwa na uzembe wa NSSF katika construction hapo sawa,lakini taarifa za magazeti zinasema ukumbi huo unae mwendeshaji,that means umekodishwa kwa mtu mwingine, huyo mtu ndio yupo responsible kwa security ya eneo alilolikodisha. In this respect i beg (for the first time) though with due respect to differ,unless more explanation are brought to my attention through jf.Salama mkuu lakini?

Doctrines za tort law inawezekana hazihusiki hapa, na unaweza kuwa unachanganya sheria zisizohusiana. Raisi amesema wahusika watachukuliwa hatua kali. Sidhani alikuwa anaongelea watu kudaiwa hela. Tort law inahusiana na hela, madai, money!

Wanapofanya kazi ya kutafuta makosa katika matukio kama maafa chombo kama tume sidhani kinachambua kwa kina sana doctrines za kisheria, hususan sheria za kesi za madai. Ndio maana Tume zinaweza kuwa hazina mwanasheria hata mmoja, ila statesman anaekubalika kama upstanding member of the community.

Wanaangalia uzembe wa kikazi, hususan majukumu yako administratively, nadhani.

( Kwa hapa ingesaidia sana kujua majukumu ya NSSF administratively kama mpangisha majengo, kitu ambacho sielewi NSSF inaiingia ingia vipi katika kukodisha majengo).

Moja ya sababu ya kwa nini tort law inaweza kuwa haihusiki hapa ni kwa sababu sanctions za tort law ni kulipa hela tu. Matokeo (hukumu) ya tume hii inaweza kuwaweka watu kwenye jeopardy za kupoteza kazi au kufungwa jela, sanctions ambazo sio madhumini wala eneo la tort law. Sababu ya pili ni kwamba tort law haifuatishi misingi ya haki kwa kina kirefu, kama vile kiwango cha ushahidi kinachohitajika ("clear and convincing evidence," au "preponderance of evidence," badala ya "beyond a reasonable doubt" inayotakiwa kwenye kesi za jinai). Haki za Ibara ya 13 ya Katiba zinataka chombo chochote kinachokaa ku determine interests za mtu kifuate misingini ya equal protection ( au tunaweza kusema due process). Itakuwa ni kukiuka misingi ya due process, nadhani, kama utatumia misingi ya tort law ku determine interests na haki za mtu ambazo zinaweza kupelekea kupoteza zaidi ya hela, yaani kazi yake na kufungwa jela.

Yet sababu nyingine ya kwa nini unaweza kuwa unachanganya sheria zisizohusika hapa ni kwamba unaziunganisha sehemu ambazo zinaweza kuwa hazipikiki chungu kimoja. Unasema NSSF na wapiga disco wapangishwaji watakuwa co-occupiers halafu unasema kwa sababu hiyo ni landlord-tenant provisions za Land Act 1999 ndio zitahusika. Nadhani unahusisha provisions na, au, definitions za occupiers kutoka Occupiers Liability Act ambayo umeiongelea siku nzima, halafu unaziunganisha na land act. Kwa maneno mengine hizi sheria unazisoma pamoja wakati Land Act haikusema kwamba isomwe pamoja na Liability Act. Na sidhani Land Act inaweza kusomwa pamoja na sheria inayotoka kwenye tort law. Isitoshe hizo definitions na doctrines za tort law hujasema, na huwa una kawaida ya kutosema, authority zake. Ni statutory law zipi hizo, au precedents kutoka maamuzi gani. Chimbuko na kiini cha nyingi ya sheria zote hizo kwa ujumla ni ile ile common law, ziwe na Kenya, Australia, Tanzania, UK, Zambia na commonwealth jurisdictions nyingine, lakini bado kuna tofauti za msingi kutoka jurisdictions moja mpaka nyingine. Na siku zinavyozidi kwenda ndio jurisdictions za common law zinazidi kutofautiana kwa sababu kila sehemu inajiandikia statutory law upya kivyake, badala ya kufuatisha maamuzi ya majaji wa Kiingereza wa karne lukuki zilizopita. Ndio maana ni muhimu kujua tunaongelea sheria za wapi hasa. Hizi tort doctrines ulizoziainisha wazitoa wapi ?

Kuhusu jinai, chombo kama tume, ambayo ndio hatua tuliyopo sasa hivi, inaweza kupendekeza criminal prosecutions lakini haiwezi kuingia sana katika uchambuzi wa mens rea na actus rea, kwa sababu hayo mambo huwa yanaendewa kwa kina mahakamani, ambako mtuhumiwa ana haki zote za due process kuya confront, tofauti na kwenye tume (au kwenye mahakama za press, pamoja na baraza la JF!). Kesi hii haijafika huko bado, sidhani. Contract law nayo ni vigumu kuichambua kiundani kwa sababu hatujui, sidhani, NSSF na wapiga disco walikubaliana nini.
 
Unapoona viongozi wetu wanashinda Kilimani kwenye nyama choma, na kwenye kumbi za mikutano ya kimataifa; mauti na hatihati zinazojongea sio rahisi kwao kuziona; hata kiama cha moto wa Sodoma na Gomora wanaweza kukipokeo kwa vifijo wakidhani ni moto wa kuokea nyama. Kwa kifupi hali ni ngumu, na viongozi wetu wako busy kuirudisha Tarime kundini bila kujua nini cha kuifanyia baada ya kuirudisha kundini.
 
Endapo habari za vifo vya watu karibu ishirini kwenye ukumbi wa NSSF zitakuwa ndivyo zilivyo mtu wa kwanza kuwajibika itabidi awe Mkurugenzi wa NSSF Dr. Ramadhani Dau.
Mzee mwanakiji mimi sioni kama iko sababu ya dr Dau kuwajibika kwa kuwa hilo disco halikuwa likiendeshwa na NSSF
 
mkuu mmj heshima mbele naomba huu mjadala uishe hapa, hayo yamepita enough said, again naomba huu mjadala ufike mwisho hapa tuwape hawa watoto waliopoteza maisha na familia zao nafasi kidogo ya kupumua, huku na sisi tukitafakari ya mbele yetu ambako ninaona giza tayari,

hii ngoma naona imelia sana sasa inataka kufkia mwisho, naomba niwe mkweli kuwa i am very troubled na yanayoendelea hapa kwamba i am going to review my stay here na kuona kama ni worthy, my instinct inaniambia kua kuna something bigger going on here na binafsi i could be walking on my last days hapa, nothing personal lakini siku zote kuna tulio na akili za kuona nje ya picture na kutumia busara kutoyatema nje kwa pupa, lakini alyways one step ahead!

Again naomba kuwashukuru wana-jf kwa yote tuliyokwisha yafanya in the name of wanyonge na walalahoi kwa ajili ya taifa letu, ninaamini kuwa mungu was always here na bado yupo pia, lakini behind the scene sasa ninaona a lot of things telling me kwamba huenda tumefika kwenye junction ya this game, i could be wrong lakini mara nyingi huwa ninakuwa right kuliko wrong, unless kutokee a miracle ninaamini kuwa siku zangu hapa zinaelekea mwishoni kama sio ukingoni, ingawa my commitment na thread ya picha bado ipo pale pale nita-stick wioth it mpaka wmisho.

Salaaam kwa wakuu wote na hasa mkuu invisible, ninaamini katika my stay hapa na wengine wote tumefanya ya kutosha kwa the course ya masikini, wanyonge na walalahoi na tutaendelea na hiyo tabia popote pale tulipo.

Mungu aibariki tanzania yetu, na jf pia.

Wasalaaaaam!

mkuu hakuna haja ya kukimbia labda ukimbie uje na jina lingine uanze vituko vingine , hiyo nayo inakubalika hapa we dare to talk open lakini kama umesema uwongo na kusingizia watu uwongo halafu unaambiwa ukweli unataka kukimbia jukwaa eti unaonewa hiyo pia hulitendei haki jukwaa hili pamoja na watu wote wanaoangalia jukwaa hili mara kwa mara

nakuomba ubadilishe uamuzi wako haraka sana kuna vituko vingi sana vinatokea hapa watu hawakimbii wanaendelea kuongea na kubadilishana mawazo vitu vingi hatuvichukulii personal humu haya ni mambo ya mpito tu ni maandishi tu unasoma unayaacha -- kwani maandisha yanauwa

wewe soma changia kisha log out kafanye kazi zako usinyimwe usingine na maandishi tu

duh yamekuwa haya
 
Asante Mwanakijiji kwa clue hii muhimu ambayo ilikuwa inakosekana.
Hata hivyo pamoja na aironditioners za ukumbi kufeli hiyo haiwezi kuwa-exonerate waendeshaji disco from responsibility kwani katika law of torts na hata criminal negligence kuna "rule of apportionment of damage" ambapo chanzo chavifo kinaonekana kuwa ni watoto kuingia wengi kuliko idadi inayotakiwa ukumbini hapo,hata hivyo vifo viliongezeka kutokana na state of panic ya watoto hivyo kukimbia ovyo wakijinusuru maisha yao hapo ndipo wakakanyagana na hivyo vifo kuwa vingi zaidi.

Kwa maana hiyo basi kwa fact hizi za leo,line of responsiblity inagawanyika sehemu mbili kati ya waendeshaji disco kama occupiers kwa kushindwa kuthibiti idadi ya watoto waliomo ukumbini na kuchukua tahadhari muhimu,mf.uwepo wa paramedic jirani kwa first aid,na nssf kama co-occupiers kwaajili ya kuhakikisha hitilafu zote ukumbini humu zinakuwa rectified kabla ya kumpa mpangaji (hapa seria inayotumika ni ile ya ardhi ya mwaka 1999 inayotoa detailed analysis ya majukumu ya landlord and tenant).FACT TOKA KWENYE SHERIA Hiyo zitatumika kuibana nssf,hata hivyo hazitamuoindolea responsibility muendesha disco kwa kuwa alichangia vifo vya watoto kutokana na omission yake ya kutotake responsibility on his part.9HII INAITWA CONRIBUTORY NEGLIGENCE)

Wakati katika criminal law,kuna kanuni inaitwa "THE DOCTRINOF CAUSALITY OR THE DOCTRINE OF CAUSATION".Hii itatumika endapo police wataamua kuwafikisha wahusika mahakamani kwa kusababisha vifo bila kukusudia yaani manslaughter.

Kumbe hapa tuna wana sheria kibao??!! Hivi siku zote uko wapi Augustoons? Kila leo huwa tunatafuta ushauri wa kisheria tuwashughulikie mafisadi na wewe umejificha kweli?
Tukiitaji tena consultation ya kisheria PLZ uwe karibu.
 
mambo yanazidi kufumuka. Sikia hii;

Uongozi wa halimashauri ya manispaa ya tabora sasa unadai kuwa hawakutoa kibali kwa ajili ya kupiga disco la watoto siku hiyo. Kaimu mkurugenzi, bwana Leopaord Ulaya amesema kuwa mmiliki wa ukumbi wa Bubbles alipewa kibali cha miezi minne kuanzia mwezi juni hadi oktoba mwaka huu ambacho hakihusishi kupigisha disco la watoto.

Pia mmiliki wa ukumbi huo Shash Patel alipewa kibali cha kuendesha disko kuanzia saa mbili usiku hadi saa nane usiku na siyo mchana na tena si kwa ajili ya kwa watoto wadogo kama ilivyo fanyika.

Mmiliki wa One Top Ten disco, Projestus Mwiga, alipewa kibali tarehe Septemba 30, 2008 kwa ajili ya kuendesha disco kuanzia Oktoba Mosi hadi 3 kuanzia saa tisa mchana hadi saa saba usiku.

kaimu Mkurugenzi huyo anasema kwa mujibu wa sheria vibali vya maonesho ya sanaa na sherehe, ambavyo vilitolewa siku hizo, hakuna ambacho kilitolewa kwa ajili ya disco la watoto.
 
Wanabodi,

Pamoja na sheria zote ambazo zimetumika humu ukweli bado kabisa haijafikia kiwango cha sisi wachangiaji kutoa hukumu hasa upande wa mwandalizi wa hilo Disco...
Navyoifahamu mimi chombo chochote cha biashara ambacho kinakodishwa huwa na mkataba, mkataba ambao sio tu unawekwa sahihi bali pia kunakuwepo na ufuatiliaji wa karibu kwa pande zote mbili kwa sababu mara nyingi insurance humwajibisha mweye mali hiyo..
Yeye anaweza kumtoza mkodishaji kiwango fulani kwa siku ya matumizi hivyo inategemea sana kama mweye mali NSSF alikuwa na insurance.. hilo kwanza. Pili mara nyingi kumbi za Tanzania wenye kumiliki ukumbi hutaka kugawana mapato na mkodishaji kwa sababu mara nyingi wakodishaji huwa ni wajuzi wa kupiga debe tu. hao tunao waita - Promoter kina Kim and The boyz!
Kisha ni katika mkataba huo tunaweza kuona kipengele kinachozungumzia idadi ya watu, ikiwa na maana kuna vyombo ambavyo vinapima idadi ya watu kwa kutumia uzito na kadhalika..
Je, ni kweli ukumbi huo umepitishwa kisheria kuwa ukumbi wa Disco ama ni maamuzi tu ya mamlaka ya wamiliki kuufanya ukumbi huo uwe wa Disco hali haukupewa kibali...Tukumbuke tu kwamba kibali ndicho kinaweza kumweka mtu wa Tatu (serikali) ktk maamuzi ya kutoa kibali wakati ukumbi wenyewe haufai kabisa kwa maandilizi ya shughuli hiyokulingana na Usalama (safety)... ikiwa ni pamoja na Aircondition, Emergence Exits, Vyoo, Sound Proof - if necessary na kadhalika.
Sasa ikiwa mwenye ukumbi aliamua yeye mwenyewe kukodisha ukumbi huo bila kuwa na kibali halali cha kufanya biashara ya Kukodisha, tena kama ukumbi wa disco basi bila shaka NSSF inatangulia kubeba mzigo huo kisheria kwa sababu hapa Ulaya kumbi nyingi sana zimefungwa na kunyimwa kibali cha kuendelea kupiga Disco kutokana na kifo cha mtu ama watu ambao kifo chao (kuchomana visu ama kupigwa risasi) hakihusiani kabisa na Ukumbi isipokuwa maswala ya Usalama..

Mimi ningependa tu kufahamu katika matukio mengi duniani ambayo majukwaa ya viwanja huanguka na watu wakafa..hata kama sababu ilikuwa kuzidisha kwa watu ktk jukwaa na state of panic, pengine kuna kesi hata moja iliyowashtaki waandilizi wa mechi badala ya mamlaka ya kiwanja hicho!..
 
Mkandara,
The closest I can remember ni ile night club iliyowaka moto New Jersey wakati bendi ilikuwa inapiga muziki na kuwasha mionzi ya moto. Nadhani owner wa club pamoja na promoter wa bendi wote walifikishwa mahakamani.
 
Jasusi na Mkandara, katika kipindi cha hivi karibuni (mwezi September 2008) huko China ulitokea moto kwenye night club uliosababishwa na miale ya moto performer. Kilichotokea mwenye ukumbi ndo amekuwa wakwanza kuwajibika then aliyeendesha disco na mwisho meya amefukuzwa kazi.

Kwetu sisi anakamatwa mwendesha disco tu na mmiliki anatoa rambirambi halafu yanakuwa yamekwisha. Huo mfano wa uwanja wa michezo ni mzuri kuelewekwa, eti anakamatwa mwandaaji wa pambano na mmiliki wa uwanja anaachwa salale!

ila kunawatu wanatumia hoja ya nguvu hapa ndo maana Mwanakijiji na FMES wameamua kuachana na mjadala huu, very sad.
 
Kinachotokea hapa ni kujaribu kuiondoa NSSF kwenye kuwajibika at all costs. Hakuna mtu ambaye atapinga kuwa waendesha disco wanawajibika kijinai. Hili halina shana na ni very obvious. Kwangu mimi ni kuonesha what seems to be obvious but is there. Msishangae mkisikia kuwa Makao Makuu NSSF hawakuwa na habari kuwa jengo lao linatumika kama sehemu ya kupigia muziki. Watasimama na kusema mkataba wao ni wa mambo ya mikutano tu na disko la watu wazima siku za weekend. Watarudisha lawama kwa Tabora. Sasa kama ingekuwa ni mara hii tu hoja hiyo inaweza kuwa na nguvu lakini mara mbili kabla?
 
what is this!kumbe hii ndo JF sikujua thread karibu nne sasa zinazungumzia kitu kimoja!this is nonsense!mnatuchanganya sasa!

"kitu kimoja" cha kipuuzi siyo; kuna thread ngapi zinazungumzia vitu vikubwa kama uchaguzi wa Tarime; ngapi kuhusu RA, ngapi kuhusu Mbowe, ngapi kuhusu chadema, ngapi kuhusu CCM? Hili la kuanzisha la watoto baada ya zile nyingine kuunganishwa jana linakuuma kweli; kwamba kwanini tunajili vifo vya watoto hawa kwenye thread zisizozidi tatu? Au tuombe ihamishwe pia itoke kwenye siasa kwa sababu inakukera tumeiweka kwenye siasa!

It makes no sense hakuna outrage na hasira! We are doomed!
 
mkuu hakuna haja ya kukimbia labda ukimbie uje na jina lingine uanze vituko vingine , hiyo nayo inakubalika hapa we dare to talk open lakini kama umesema uwongo na kusingizia watu uwongo halafu unaambiwa ukweli unataka kukimbia jukwaa eti unaonewa hiyo pia hulitendei haki jukwaa hili pamoja na watu wote wanaoangalia jukwaa hili mara kwa mara

nakuomba ubadilishe uamuzi wako haraka sana kuna vituko vingi sana vinatokea hapa watu hawakimbii wanaendelea kuongea na kubadilishana mawazo vitu vingi hatuvichukulii personal humu haya ni mambo ya mpito tu ni maandishi tu unasoma unayaacha -- kwani maandisha yanauwa

wewe soma changia kisha log out kafanye kazi zako usinyimwe usingine na maandishi tu

duh yamekuwa haya

Huu ndio mwanzo na mwisho wa upeo wako wa kuona na kufikiri, lakini haibadili ukweli ulioko mbele yetu na unaujua vizuri sana, masikini ya Mungu maneno yako haya ndio mwisho wa level ya upeo wako wa kufikiri, very sad indeed!

Pamoja na maneno yako mafupi na very low, mimi ninaendelea kuwaomba kina GT na wenzake, kukaa pembeni, na ninashukuru Mungu kua so far wananisikia, na nitaendela kuwaomba na baadhi ya wengine pia, ili wewe uweze kujadili hii topic kwa amani kama unavyofanya sasa!

I realize kua siku hizi umeongezeka mapembe, lakini you should know better kua sio wote tunaoweza kuzugika kwa urahisi na hiyo new found "heshima" yako hewa ambayo ni temporary tu, chezea wajinga wenzako unaocheza nao huko mikifiri hatujui mnachofanya, hapa kwangu utaungua na ukome kama huwezi kushika adabu, ninatafuta amani na thank to God kwamba inakuja!

Na ninawashukuru sana Mkuu GT na Mkuu YRSIMNE, kwa kunielewa na Mungu awabariki
Ahsante Mkuu!
 
Back
Top Bottom