Vifo Tabora: Uongozi wa NSSF Makao Makuu Uwajibike

Hili ni sikitiko kwa wazazi, ndugu, marafiki na Taifa. Ila tu wazazi inakuwaje wanaruhusu watoto cha kushangaza miaka mitano kwenda disco????? Inabidi tuwe serious na malezi, something wrong here. Child Protection and Safety iko wapi na inaishia miaka mingapi Tanzania???? Hii iwe ni fundisho kwa Familia na Taifa ili kuweka by-laws kwa wazazi na waendeshaji wa maeneo ya starehe.

Sorry kwa wale ambao nitawaudhi but tabia ya kuwaacha watoto kuzagaa ipo sana kwa Waswahili. natumaini kwa wengi mtanielewa nikisema watoto wa USWAHILINI. Wazazi hawa nionavyo mimi wako loose sana na watoto wao kiasi kwamba unajiuliza mama unakuwa na raha gani mwanao wa say under 18 yuko anazagaa tu wala huna wasiwasi sembuse wa miaka mitano na chini ya hapo.

Unashangaa wakati wa sikukuu kubwa kama Eid, Christmass na kidogo Pasaka watoto wanaongozana barabarani kwa makundi mchanganyiko wa miak 2, 3, 4, ..... bila uangali wa watu wazima. Eti mtoto wa miaka 5,6,... anaambiwa mchunge mdogo wako. Sasa hii ni hatari na lichukuliwe kuwa ni tatizo la jamii ili lipatiwe ufumbuzi haraka sana.

Poleni sana wafiwa.

Ok, Kuna uvumi kuwa kulikuwa na harufu kali kama ya sumu kabla ya watoto hao kuanguka na kuanza kuzirai!!!!!
 
By the way:
Yaani msiba umetokea jana juzi, Waziri Mkuu anaendelea na mkutano wake Ghana; Rais ilibidi amalizie Idi pili na Makamu wa Rais alikuwa alikokuweko. Halafu wameuachia mkoa kusimamia hili. Do these people even know what a national tragedy is? Halafu wanamtuma Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana (ambaye NSSF iko chini yake).

Mengine ya kusema nimeyasema hapa, maana kuandika tu hakuelezei ninachosema hasa.

http://www.klhnews.com/images/podcasts/tabora.mp3

Mwanakijiji...

Hivi umekula nini mzee wangu wakati huo wa Eid....

Tofautisha kati ya majanga ambayo yanahitaji kuokoa watu.... kwa maana resources needed to rescue people or casualities...

na

vifo ambavyo vimetokea na kilichobaki ni kutoa ubani na salamu za Rambi rambi...

Hilo tu mkuu; acha kukariri mambo ya Zamani... no wonder issue zako nyingi ni kwa kuwa unafikiri kijima.
 
Hili ni sikitiko kwa wazazi, ndugu, marafiki na Taifa. Ila tu wazazi inakuwaje wanaruhusu watoto cha kushangaza miaka mitano kwenda disco????? Inabidi tuwe serious na malezi, something wrong here. Child Protection and Safety iko wapi na inaishia miaka mingapi Tanzania???? Hii iwe ni fundisho kwa Familia na Taifa ili kuweka by-laws kwa wazazi na waendeshaji wa maeneo ya starehe.

Sorry kwa wale ambao nitawaudhi but tabia ya kuwaacha watoto kuzagaa ipo sana kwa Waswahili. natumaini kwa wengi mtanielewa nikisema watoto wa USWAHILINI. Wazazi hawa nionavyo mimi wako loose sana na watoto wao kiasi kwamba unajiuliza mama unakuwa na raha gani mwanao wa say under 18 yuko anazagaa tu wala huna wasiwasi sembuse wa miaka mitano na chini ya hapo.

Unashangaa wakati wa sikukuu kubwa kama Eid, Christmass na kidogo Pasaka watoto wanaongozana barabarani kwa makundi mchanganyiko wa miak 2, 3, 4, ..... bila uangali wa watu wazima. Eti mtoto wa miaka 5,6,... anaambiwa mchunge mdogo wako. Sasa hii ni hatari na lichukuliwe kuwa ni tatizo la jamii ili lipatiwe ufumbuzi haraka sana.

Poleni sana wafiwa.

Maoni yako ni sahihi lakini kwa upande mwingine naona watawala na watendaji wetu hawawatendei haki watoto wetu. Naamini ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa katika kila miji yanatengwa maeneo kwa ajili ya burudani na shughuli za michezo kwa watoto. Miaka ya nyuma haya maeneo yalikuwepo lakini kwa sasa mengi yameuzwa na kubadilishwa kwa ajili ya matumizi mengine. Wazazi wana jukumu la kulea lakini kuna wakati watoto nao wanataka kufurahi na wenzao. Serikali yetu haiwajali hawa watoto. Angalia kama DSM kipindi cha sikukuu watoto wengi hukimbilia beach ambayo ni sehemu pekee wanayoyoweza kucheza na wenzao lakini kwa mtizamo wa haraka sio sehemu salama sana. Mwanza waliuza uwanja wa Nyamagana pasipo kujali kuwa unawafaa watoto wa eneo hilo na hata wakubwa pia. Kwa hili naona Serikali yetu inahitaji lawama zaidi kuliko wazazi wa watoto waliofariki
 
Hawa jamaa hawapo makini kabisa kuhusu maisha ya watu maana hata huku Dodokuna ukumbi upo katika Petrol station na watu wanavutia sigara nje kwenye eneo ambalo ndio kuna matanki ya mafuta. Serikali hailioni hilo mpaka maafa yatokee. WHY?
 
pia nadhani na familia ziwe makini katika malezi ya watoto wao maana haiwezekani unamwachia mttoto wa miaka 5 aende kwenye kumbi za disco tena sio disco ni Night club hata kama ni mchana haya kwa kweli sio malezi mema.
 
Mwanakiji huna nyimbo,LAZIMA ukubali kuwa ulikurupuka na MIJAZBA yako ya chuki Binafsi,sie tunakujua wewe kuwadi wa Chadema,sasa tunakwambia CHADEMA HOYEEEE!!!!Unajua unapokuja ktk forum kama hizi,kwanza unatakiwa uache unazi wako wa chadema,uweke pembeni,maana tayari umeshatoa na article kwenye magazeti Dr Ramadhani dau ajiuzulu,wewe unasema kuwa ngoja tuone?haya na tuone.
Hivi Dr Dau amekuudhi nini hasa?Maana dah ulivyokurupuka na speed ya awajibike!!sie sote tunaokuona wewe mwandishi uliyekomaa tukajua kweli chadema inakutoa akili.Inaonyesha una mtandao mkubwa Mwanakijiji na influence kubwa ktk Serikali,umekuwa na kibri kiasi hiko?
ATC mwaka jana waliharibu mambo ya Hijja,mbona David Mattaka hakujiuzulu?Au yule mtu jumapili?
Acha Jazba zako na chuki zako,njoo na hoja na sio VILOJA.
Humu ndani tunataka ku discuss issues sio chuki zako zisizo na mpango.
Labda nikuulize,kama Dr Dau hajawajibika utafanya?Utampiga au utamuwajibisha?Au uta muuwa?au uta mkubenea?Maana tunakuona umeshabikia sana awajibike!!!!
Naomba kwa Mola niwe hai mpaka issue hii itakapomalizika hali ya kuwa Dr Dau hajawajibika anadunda kama kazi.
Mwanakijiji acha Fitna,bado hujakomaa katika Fitna,shabikia chadema na uandike andike makala upate rizki yako.
 
mwanakijiji,ili raisi awajibike kitokee nini?
Gari la Nssf limegonga Dr Dau awajibike!!!!
Stafff wa Nssf amefariki Dr Dau awajibike!!!!
Gari la Nssf halijakwenda service Dr Dau awajibike!!!
Mbona husemi Pinda awajibike?na yeye ndio mtendaji mkuu wa serikali?
Mbona mkuu wa mkoa husika husemi awajibike?
Mbona husemi RPC wa mkoa husika awajibike?Na yeye ndio muhusika wa ulinzi wa mkoa?
 
Hawa jamaa hawapo makini kabisa kuhusu maisha ya watu maana hata huku Dodokuna ukumbi upo katika Petrol station na watu wanavutia sigara nje kwenye eneo ambalo ndio kuna matanki ya mafuta. Serikali hailioni hilo mpaka maafa yatokee. WHY?

Jamani riserikari letu ndivyo lilivyo,viwanja vingi vya kuchezea watoto vilivyo karibu na shule/Hospitali Tanzania yote wamekunywa!!! Sehemu za wazi nazo wametia ndani ingawa walishindwa Mnazi mmoja baada ya wenye nchi kuchukia, pia angalia usalama usivyozingatiwa kwa abiria kwani hoteli zote zinazotumika kwa abiria Dar-Mwanza, Dar-Arusha etc kuna Petrol stations ambazo ni hatari kwa abiria lakini kwa vile ndivyo tulivyo hakuna mtu toka serikalini wa kuhoji wala kukemea wala kutoa ushauri wa bure kuwa si salama abiria wengi kuwa karibu na hatari ya moto kwani wengine wakishakula huvuta sigara hapo
 
Sasa huu utitiri wa thread wa nini wakati suala hili tayari linajadiliwa kule? Hii kuruka ruka hakufanyi hoja yako kuwa na nguvu.

MODS pls unganisha hii na ile ya kule tuwe na mtiririko mzuri...
 
Last edited:
Mzee Mwanakijiji naomba kupingana nawe ktk hili kwa kuzingatia haki ya asili ambayo ndugu na kaka yangu mzamivu Dau anahaki ya kuhifadhiwa nayo.

Kimsingi ukumbi huo ni mali ya NSSF lakini ni vema tukatambua kuwa mwendeshaji wa ukumbi huo ni aidha NSSF wenyewe au mtu binafsi(kama vile pale THI ya sasa), Tabora kama mkoa una kamati ya Ulinzi na usalama ambayo Mh.Mwinyi mussa ndie M/kiti wake na wajumbe ni wana usalama wote mkoani humo ambao ni wataeule wa mkuu wa nchi kupitia idara zao.

Dkt Dau ni mwendeshaji kiongozi wa mfuko huu kwa nchi nzima na haimpi mamlaka za kidola ktk hili lililojitokeza Tabora, lakini yeye kama mwendeshaji kiongozi atawajibika kuwawajibisha wanaomsaidia kuiendesha NSSF Tabora pale itakapobainika kuwa wameshiriki ktk mauaji hayo kwa makusudi na kama Bodi ya NSSF itaona hawa jamaa wa Tabora wanayo hoja dhidi ya Mkuu wao Dkt Dau ktk mauaji haya vema watawajibika kumuomba mteuzi wake kumuwajibisha kijana huyu msomi lakini pia na wao wakijivua ukurugenzi wao bodini mara moja.

Picha hii naamini unayo mkuu wangu Mwanakijiji na wafahamu wazi kuwa huyu bwana si chanzo cha mauaji yale aidha ya makusudi au bahati mbaya (Tutajua) lakini kwa sababu ya U-DG wake pale anakuwa scapegoat ktk janga hili ktk media.

Nadhani M/kiti wa Bodi yao bado ni Mzee Kaboyonga Siraju kama sikosei ambaye pia ni Mbunge wa Tabaora mjini.

Hili ni janga tena kwa watoto wadogo, sisi wadogo zako ndio tumeanza rasmi familia na tunao hao watoto wadogo ambao kwao sherehe ni gatherings na makelele mengi na ndicho kilichowakutanisha watoto wengi pale Tabora na ktk hali isiyotarajiwa na wazazi wao wamefikwa na umauti, tunaomboleza, tunawalilia na tunajutia yaliyojitokeza siku hiyo lakini sisi ni nani kuhoji utashi wa mungu? Tunakuomba sana umpe nafasi Dkt Dau kuomboleza msiba huu kwa amani, usimjengee wasifu wa kiuuaji wa kinyama kwa kiwango hiki.

Ni hayo tu kaka Mwanakijiji.
 
Kwa kweli inasikitisha sana, hivi niandikavyo tume imeanza kuwa hoji wamiliki wa kumbi hizo ambao wapo ndani toka juzi,
 
Last edited:
Hapa nadhani tutalumbana sana, lakini muhimu ni kutafuta nani mzembe kwa hili. Manake hatuwezi kukubali roho za wenetu ziishie hivihivi. Hapa kwa haraka haraka kuna mzembe ama wazembe.
1. Ukijenga ukumbi ukawa wa mkutano na ukasemekana unaingiza watu 100, hiyo haimaanishi kuwa hauwezi badilishwa kuwa ukumbi wa disko ukaingiza watu 200. Ikumbukwe ukumi wa mikutano una viti ambavyo vinafaa mtu kukaa kwa nafasi. Lakini jee walipobadili kuwa ukumbi wa disko walifuata sheria zinazokubalika. Na hapa anayehusika kutoa leseni kwa ukumbi wa disco si NSSF, bali kuna watoa leseni. Mfano kama wangeamua kuweka hospitali hapo, watoa leseni si NSSF, na hata kama hiyo hospitali haikidhi matakwa, huwezi kuwalaumu NSSF (wakodishaji), bali nji bodi uhusikayo kutoa leseni ya hiyo biashara.


Mfumwa,
Nafikiri hukusoma makala za nyuma au hata juu yake. Hii imeelezewa sana. Mtu wa kwanza kutoa kibali sehemu kuwa na DISCO ni NSSF. Baadaye walipelekewa MANISPAA kutoa baraka zao. Nafikiri kuna haja hapa waongezwe watu wa FIRE BRIGADE na hawa wawe na wahandisi wao wanaojua sheria za ujenzi wa PUBLIC buildings. Watu waliojenga hilo jengo ni NSSF. Wao wana michoro yote yaani kutoka kwa Architecturer na Structural Engineers. Kutoka kwa Structural Engineer hapa hana shida kwani pamoja na watu kuwa wengi ghorofani na kucheza Disco, jengo halikuanguka. Hongera mhandisi wa hilo jengo. Tatizo ni michoro ya Architecturer. Hii ndiyo inaweza KUWAHUKUMU jamaa wa NSSF. Hii inachorwa kutokana na mahitaji ya jengo. Hawa wana sheria zao kama kuweka milango ya kutokea, madirisha, ventilations, nk. Sasa kama ukumbi ulikuwa wa mkutano na baadaye ukabadilishwa, je walibadilisha hivyo vitu juu? Kama huyu Architecturer aliambiwa abadilishe na yeye akafanya usanii, basi unaweza kukuta badala ya NSSF kukamatwa ni huyu bwana kwani alichezea kazi.
Kwangu mie hapa hata tume haitasaidia. Hili jambo liende MAHAKAMANI. Huko ni SHERIA tu zitaongelewa. Hebu soma mfano huu chini:-
==>> Jengo moja lilipata cracks. Tatizo lilikuwa ni kwamba wakati wa winter owner wa jengo waliamua kuvunja ukuta na kuweka mlango. Kutokana na baridi kuingia kwa haraka, jengo likacrak. Sasa kesi ikaenda mahakamani na kujulikana hayo. Mhandisi akasema kuwa Owner wa jengo ndiyo mwenye kosa kwani alivunja jengo wakati wa winter na kusababisha tofauti ya haraka ya joto. Ila hakimu alimuuliza, je kama jengo zima heating system zingeligoma na kufanya jengo liwe baridi na wakati huo jamaa wanataka kuweka mlango, si ingelikuwa kitu kilekile? Wee Mhandisi ulitakiwa kujua kuwa INAWEZEKANA siku moja kitu kama hiki kikatokea.
Tatizo kubwa hapa ni kuwa watu wengi tunaingilia FANI ya watu. Hapa wanatakiwa waseme WACHORAJI majengo, Wahandisi wa ujenzi waliosomea au wanaodeal na sheria za UJENZI na Wanasheria. Ila Wote inabidi waende Tabora na kujionea wenyewe na kuangalia MKATABA mzima na jengo la DISCO na hapo ndipo MAHAKAMA ianze kazi. Vinginevyo wengi hapa tunaFIKIRI tu bila kuwa na ukweli kamili.
 
Mkuu Agustoons,

Heshima mbele sana, umenielimisha sana hapa kwenye huu mjadala ila ninaomba kuongeza hamisni zangu, miaka ya nyuma in the 90s nikiwa NY, iliwahi kutokea this kind of seke seke, tena mara mbili ya kwanza ilikua kwenye Disco moja linaitwa Rose Disco, na lingine lilitokea City College, hili lilitayarishwa na Puffy Daddy na Mkulu Heavy D,

Ninachojua ni kwamba katika ishu zote mbili watu walikufa, kwenye ishu ya Rose mmiliki wa Club alikula miaka jela lakini sio owner wa jengo, kwenye ishu ya Sean Comb, ambaye ndiye aliyekua mtayarishaji wa ile concert, alionwa kutokuwa na makosa mbele ya sheria, kwa sababu shughuli ilifanyika uwanjani wa Basketball na the rst of story!

Sasa hapa nafikiri kuwa kama wenye jengo wakithibitisha kua wametimiza masharti yote kisheria ya umiliki wa jengo, basi ni mtayarishaji wa hili Disco ndiye anayewajibika hapo, au?

I mean wale wenye hii elimu tumwagieni, mkuu Augostoons ninashukuru sana kwa elimu yako nzito na please endelea kutumwagia zaidi, na ubarikiwe pia kwa huo moyo wako!

Asante sana Mkuu FMES
Heshima zako zipo noted nami nakurudishia zinazokustahili.
Nashukuru sana kwa clear case ya namna hiyo.Katika historia ya common law ambayo hata marekani inatumika japo with modifications,kuna sheria kuu mbili zinazoweza kutawala mazingira haya tunayoyazungumzia,ya kwanza ni jinai na ya pili ni sheria ya madhara(yaani law of torts).Sheria hizi zimekuwa zikitumika sana duniani na effect zake ni very serious compared na sheria nyingine yoyote ile.Naweza kusema katika construction industry kwa upande wa responsibility hizi ndio sheria mama.
Katika makosa ya jinai, te main principle ni kwamba ili mtu awe ametenda kosa au kutiwa hatiani lazima vitu viwili vioane yaani tendo(actus reus) na nia ya kutenda kosa ambayo huwa tutaiita nia ovu(ill will au kwa lugha ya kitaalamu mens rea).Na kwa maana hiyo basi kanuni ni "actus non facit reum nisi mens sit rea" [which means that "the act does not make a person guilty unless the mind is also guilty"] kwa maana no one will be held responsible unless there is a meeting(concurrence) of the act and the mind(kwa lugha rahisi),kwa maana hiyo basi kitu kigumu katika kuthibitisha makosa ya jinai sio tendo bali ni kuoanisha nia na tendo.
Katika kesi iliyopo mbele yetu,kitendo ni kufa kwa watoto,lakini nia bado hatuijui(kwa maana kwamba je,kulikuwapo na nia ya kuua hao watoto?).Nia hiyo yaweza kuwa implied wakati mwingine kutokana na omission(yaani kuzembea kuchukua hatua kwa mtu mwene wajibu wa kufanya hivyo).Ndio maana basi ili kuthibitisha nia ovu prosecution mara nyingi inaipata mens rea kwa kuangalia kama kulikuwa na 1.recklessness 2.conduct or omission 3.intention au intent 4.negligence.

Nimebold maneno negligence na recklessness kwa maana nzuri tu.Kwa sisi waswahili tutasema kwamba recklessness na negligence ni uzembe lakini sio kweli,hivi ni vitu viwili tofauti.Recklessness ni upuuzi au papara wakati negligence ni uzembe.Sasa upuuzi au papara maana yake nini?lini mtu anakuwa mpuuzi(reckless).Upuuzi ni pzle ambapo mtu anaona kitu na anajua madhara yake lakini hachukui hatua au anasema hata ikitokea ni ajali kazini.Mathalani unataka kwenda kazini asbh unajaribu gari unaona halina breki sawasawa lakini unasema anyway tutafika tu ngoja niende hivyo hivyo,hii ni recklessness na upo responsible.

Sasa kwa upande wa nssf tujiulize walikuwa reckless?au je,ni mpangaji wa ukumbi ndio alikuwa reckless?

Negligence,ngeligence nayozungumzia hapa sio civil negligence bali criminal negligence.Negligence maana yake ni kutochukua hatua za tahadhari hata kama hukujua matokea ya tendo lako,jambo la msingi ni kuwa ulikuwa na wajibu na hukutimiza wajibu.Mathalani umejifunza udereva vema na umeendesha labda hata miaka 5,lakini asubuhi wee unaondoka tu na gari hucheki oil,wala breki wala kama kuna loose nuts zozote hutake precaution yoyote,unaondoka huu ni uzembe na ukipata ajali au tatizo lolote you are criminally responsbile.
The test ya criminal negligence ni kwamba "a reasonable person with the same abilities and skills as the accused would have foreseen and taken precautions to prevent the loss and damage being sustained". what or who is a reasonableman is a question of fact,to be determined by court.

Tukirudi kwenye mada je,nssf walikuwa na criminal negligence kama reasonable men?nawaachia ninyi wadau.
N.B.Kesi nyingi za majengo kuanguka dar,polisi hubase katika criminal negligence kuwafikisha watu mahakamani.sasa sijui hawa wa huko Tabora inakuwaje.
MATOKEO YA PROCESS HIYO YAPO JUU NI KIFUNGO AU FAINI AU VYOTE KWA PAMOJA


CIVIL OR TORTIOUS NEGLIGENCE.
Civil negligence imekudefined kama "The breach of a legal duty to take
care, resulting in damage to the claimant which was not desired by the defendant" au Negligence is the omission to do something which a reasonable man, guided upon those considerations which ordinarily regulate the conduct of human affairs, would do, or doing something which a prudent and reasonable man would not do"

MATOKEO YA KESI ZA NAMNA HII SIO KIFUNGO BALI NI MALIPO YA FIDIA KWA MAPESA MENGI,KAMA NI KAMPUNI INAWEZA HATA KUFILISIWA.LAKINI ILI USHINDE TORT OF NEGLIGENCE UNATAKIWA KUTHIBITISHA YAFUATAYO
1.Kwamba "the defendant had a duty"(mdaiwa alikuwa na wajibu kisheria)
kivipi?ili kuestablish duty maswali ya kujiuliza ni haya
a.Whether the consequences of the defendant’s act were reasonably foreseeable
b.Whether there is a relationship of proximity between the parties, ie a
legal relationship or physical closeness
3.Whether in all the circumstances it would be fair, just and reasonable
that the law should impose a duty.
kama majibu yote ni yes basi unaenda hatua ya pili


2.Wajibu huo hakuutekeleza au alikiuka wajibu huo(breach of duty)
The Standard Expected
Negligence is falling below the standard of the ordinary
reasonable person. Specific rules apply if the defendant is
a child, a learner or a professional:Mahakama itafikiria
a.The degree of risk involved and likelihood of harm occurring
b.The seriousness of harm. Sometimes, the risk of harm
may be low but this will be counter-balanced by the gravity of harm to a particularly vulnerable claimant
c.The practicability of taking precautions. The courts expect people to take
only reasonable precautions in guarding against harm to others.
d.The social importance of the risky activity.If the defendant’s actions served a socially useful purpose then he may have been justified in taking greater risks.
The claimant must produce evidence which infers a lack of
reasonable care on the part of the defendant. However, if no such
evidence can be found, the necessary inference may be raised by
using the maxim res ipsa loquitur, ie the thing speaks for itself


3.Uthibitishe madhara yaliyotokana na mdaiwa kutotekeleza wajibu wake(DAMAGE CAUSED BY THE BREACH) mf.madhara huko tabora ni kupotea kwa maisha ya watoto.Ukishindwa kuthibitisha madhara kunakuwa hatuna tort.

Baada ya kuyafanyia kazi mambo hayo hapo juu,basi ndio unaweza kuconclude kwamba fulani anatakiwa kuwajibika katika sheria ya madhara.SASA SWALI LA KUJIULIZA NI JE,NSSF MASWALI HAYO YANAWAINGIA ILI WAYAJIBU?
Tort of negligence inahusisha mambo mengi sana ikiwamo professional negligence

SHERIA nyingine ndogondogo zinzoweza kumwajibisha mtu katika mazingira haya ni pamoja na administrative law ambayo inategemea na specific piece of legislation inayoestablish na kudisestablish madaraka ya mtu husika.lakini effect hapa ni kufukuzwa kazi tu,kujiuzulu ama kushushwa cheo lakini sio kwenda mahakamani.[hii inawahusu zaidi watendaji walioko kwenye utumishi wa umma]

Kanuni nyingine ya responsibility hapa ni political au ministerial responsibility ambayo hii inawahusu mawaziri,ambapo madhara yake ni waziri kujiuzulu tu basi.watoto wamekufa,waziri anajiuzulu,so what?imekwisha au kama sivyo basi mamlaka husika,na hapa kwetu polisi wampeleke mahakamani criminally ambapo ataishia kufungwa,kulipa faini au kuachiwa huru.Lakini hawawezi kumshitaki kwenye tort kwa kuwa hawana mamlaka hayo,wenye mamlaka hayo ni ndugu wa wafiwa.

Ndugu zangu hayo ndiyo maeneo makuu manne yanayotawala vifo hivyo vya TABORA ksheria.
ANGALISHO:
Kwenye tort of negligence hasa occupiers liability,inamtaka mtu awe makini na mazingira yake ili yasilete madhara kwa wengine.Mfano,ukijenga nyumba ukaweka madirisha ukazungushia waya wa umeme ili majambazi wasing'oe nondo,lazima uweke bango kwa tahadharisha kuwa kuna umeme,ili wakija wawe makini,usipoweka wakanaswa wakafa,bado mwenye nyumba upo responsible kwa kusababisha kifo kwa uzembe.Mazingira yako hayakuwa secure enough for visitors.you must always anticipate visitors.
Visitors hapa ni pamja na watoto wadogo,majambazi,kama una watoto wa kike teenagers,wanaume wanaokuja kuwatongoza nao ni visitors ili wanaporuka ukuta wasiumie,na watu wowote unaowaalika kwenye sherehe nyumbani kwako.And that is the reason why ukipita sehemu nyingi utakuta zimeandikwa "MIND YOUR HEAD",MIND YOUR FEETS,SLIPERY FLOOR,MBWA MKALI,ELECTRIC FENCE,DANGER,CCTV IN OPERATION NK.Huu ni wajibu unaotokana na law of torts(sheria ya madhara).kwa faida tu ya wanaopenda kusoma naambatanisha na OCCUPIERS LIABILITY ACT YA TANZANIA

NAOMBA KUWASILISHA.
 

Attachments

  • OCCUPIER'S LIABILITY.pdf
    345 KB · Views: 94
Nimerudi baada ya kupata jibu.

hatuwezi kusema kumwajibisha mkurugenzi wa kampuni yenye jengo kwani kuna vitu ambavyo yeye hausiki hata kidogo.

inawezekana yeye hajui kama kulikuwa na disko kwenye ukumbi wa jengo lake, inawekana pia disko halikuandaliwa na NSSF, hivyo hawawajibiki moja kwa moja na watu walioingia isipokuwa yule aliyekodisha ndo anatakiwa kuangalia idadi ya watu na ukubwa wa ukumbi.

binafsi sioni direct link ya watu kufa kwenye ukumbi na mkurugezi wa NSSF unless kuna taharifa zaidi za kumuunganisha na vifo hivyo.

Watanzania bwana? yaani suala la ukumbi awajibike mkurugenzi mkuu?
Nimeishiwa pumzi miye
 
Mfumwa,
Nafikiri hukusoma makala za nyuma au hata juu yake. Hii imeelezewa sana. Mtu wa kwanza kutoa kibali sehemu kuwa na DISCO ni NSSF. Baadaye walipelekewa MANISPAA kutoa baraka zao. Nafikiri kuna haja hapa waongezwe watu wa FIRE BRIGADE na hawa wawe na wahandisi wao wanaojua sheria za ujenzi wa PUBLIC buildings. Watu waliojenga hilo jengo ni NSSF. Wao wana michoro yote yaani kutoka kwa Architecturer na Structural Engineers. Kutoka kwa Structural Engineer hapa hana shida kwani pamoja na watu kuwa wengi ghorofani na kucheza Disco, jengo halikuanguka. Hongera mhandisi wa hilo jengo. Tatizo ni michoro ya Architecturer. Hii ndiyo inaweza KUWAHUKUMU jamaa wa NSSF. Hii inachorwa kutokana na mahitaji ya jengo. Hawa wana sheria zao kama kuweka milango ya kutokea, madirisha, ventilations, nk. Sasa kama ukumbi ulikuwa wa mkutano na baadaye ukabadilishwa, je walibadilisha hivyo vitu juu? Kama huyu Architecturer aliambiwa abadilishe na yeye akafanya usanii, basi unaweza kukuta badala ya NSSF kukamatwa ni huyu bwana kwani alichezea kazi.
Kwangu mie hapa hata tume haitasaidia. Hili jambo liende MAHAKAMANI. Huko ni SHERIA tu zitaongelewa. Hebu soma mfano huu chini:-
==>> Jengo moja lilipata cracks. Tatizo lilikuwa ni kwamba wakati wa winter owner wa jengo waliamua kuvunja ukuta na kuweka mlango. Kutokana na baridi kuingia kwa haraka, jengo likacrak. Sasa kesi ikaenda mahakamani na kujulikana hayo. Mhandisi akasema kuwa Owner wa jengo ndiyo mwenye kosa kwani alivunja jengo wakati wa winter na kusababisha tofauti ya haraka ya joto. Ila hakimu alimuuliza, je kama jengo zima heating system zingeligoma na kufanya jengo liwe baridi na wakati huo jamaa wanataka kuweka mlango, si ingelikuwa kitu kilekile? Wee Mhandisi ulitakiwa kujua kuwa INAWEZEKANA siku moja kitu kama hiki kikatokea.
Tatizo kubwa hapa ni kuwa watu wengi tunaingilia FANI ya watu. Hapa wanatakiwa waseme WACHORAJI majengo, Wahandisi wa ujenzi waliosomea au wanaodeal na sheria za UJENZI na Wanasheria. Ila Wote inabidi waende Tabora na kujionea wenyewe na kuangalia MKATABA mzima na jengo la DISCO na hapo ndipo MAHAKAMA ianze kazi. Vinginevyo wengi hapa tunaFIKIRI tu bila kuwa na ukweli kamili.

Sikonge, una uhakika kuwa NSSF wanaweza kutoa kibali ya sehemu ya disco. Ina maana siku hizi ukitaka kufungua ukumbi wa disko unaweza kwenda NSSF kuomba kibali. NSSF wamekodisha jengo ili litumike kama ukumbi wa Disco, hilo ndio najua, mfano mimi (Mfumwa) naweza kukukodisha Sikonge nyumba yangu ufanye kuwa ni Hospitali, lakini nakupa ruhusa uendeshe hospitali, ila sikupi kibali cha kuwa na Hospitali. Ina maana hapo waliotoa idhini ya kukubali kuwa ukumbi wa disco, ndio wana matatizo, manake wao ndio wanakagua na kusema sasa unafaa kwa shughuli hiyo kwa vigezo vyao. Kama tume itatulia, lazima wakosaji watapatikana tu, si tume zote zilifanya vizuri, lakini zipo zilishughulika vizuri na tuna mifano.
 
Watanzania bwana? yaani suala la ukumbi awajibike mkurugenzi mkuu?
Nimeishiwa pumzi miye

Kandambili;

Mbona ndio kama jadi yetu... kupenda kujadili watu na vitu vidogo vidogo... kwa kuthibitisha kauli yangu... angalia siasa za uchaguzi Tarime,,,

Siasa za uchaguzi Tarime zimekuwa Siasa za Marehemu Chacha Wangwe... na wale ambao wamezidiwa kwenye Siasa za Marehemu Chacha Wangwe wameenda kwenye familia yake.

Mradi tu... tunaongea upupu... na upuuzi wetu tunaendeleza mila zetu.
 
Ok, Kuna uvumi kuwa kulikuwa na harufu kali kama ya sumu kabla ya watoto hao kuanguka na kuanza kuzirai!!!!!

Si ajabu!!!! Yawezekana jamaa alifanya furmigation na hakuchukua tahadhari ya muda wa siku za kupumzisha eneo hilo. Dawa nyingine zinachukua hadi 14 days kuruhusu matumizi. Sasa na tamaa ya pesa na kutothamini watu basi ndo hivyo tena. Hata mimi nadhani kuna kitu kimefichika hapo. Hata kama ni kukosa hewa si kwa kiasi kile. Lazima kuna kitu cha kuchunguza kwa makini hapo. Pamoja na hayo narudia Child Protection and Safety must be adhered to.
 
Maoni yako ni sahihi lakini kwa upande mwingine naona watawala na watendaji wetu hawawatendei haki watoto wetu. Naamini ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa katika kila miji yanatengwa maeneo kwa ajili ya burudani na shughuli za michezo kwa watoto. Miaka ya nyuma haya maeneo yalikuwepo lakini kwa sasa mengi yameuzwa na kubadilishwa kwa ajili ya matumizi mengine. Wazazi wana jukumu la kulea lakini kuna wakati watoto nao wanataka kufurahi na wenzao. Serikali yetu haiwajali hawa watoto. Angalia kama DSM kipindi cha sikukuu watoto wengi hukimbilia beach ambayo ni sehemu pekee wanayoyoweza kucheza na wenzao lakini kwa mtizamo wa haraka sio sehemu salama sana. Mwanza waliuza uwanja wa Nyamagana pasipo kujali kuwa unawafaa watoto wa eneo hilo na hata wakubwa pia. Kwa hili naona Serikali yetu inahitaji lawama zaidi kuliko wazazi wa watoto waliofariki


taffu69 asante kwa maoni mazuri. Nakubaliana nawe kuwa Serikali haijali watoto. Viwanja vya michezo or open spaces zimeuzwa na uongozi wa manispaa au halmashauri nyingi. Cha kushangaza wananchi wanapiga makelele lakini hakuna hatua inayochukuliwa. Hii inatokana na kwamba, wanunuzi wa maeneo hayo ni walewale wa kifisadi au ndugu wa viongozi hao. Kwa hali hiyo inakuwa vigumu kuchukua hatua yoyote. Wakati mwingine viongozi wa manispaa au halamashauri wanashinikizwa na uongozi wa juu kuwa ni lazima eneo liuzwe kwa jamaa anayehusika tena pengine ajenge baa au godown.

Tungekuwa na uongozi imara ingeagiza majengo hayo yabomolewe but tusitegemee kitu kama hicho kwa Political System na uongozi tuliyo nayo, not committed.
 
Back
Top Bottom