Jagood
JF-Expert Member
- Aug 15, 2016
- 2,137
- 2,385
Kwani mnapokula huwa mna wala wazima?
Kwani mnapokula huwa mna wala wazima?
Kabisa, na kwa michango ya wengi humu inaonekana hawana uelewa wa hili. Ukitaka kufanya shughuli yeyote fuatilia taratibu zake zikoje.Hakuna kitu kibaya kwenye nchi kama kuingiza mimea na wanyama bila utaratibu.
Nchi za wenzetu, hata apple huingii nalo airport. Kuanzia spices mpaka kwenye wanyama. Hata kipande cha jani au ua kama liliingia kwenye begi bila wewe kujua, mbwa akanusa, utasachiwa begi zima.
Unless kama ulipata kibali na sample ya hao wanyama au mimea ilishachukuliwa na kuonekana hamna tatizo kwa kibali maalum.
Ukitaka kuona hasara ya kuingiza mimea na ndege hovyo, nenda ziwa Victoria uone magugu maji yalivyoleta shida, tembea dar na zenji uone kunguru wanavyosumbua mpaka ukaja mradi wa kuwaangamiza.
Anayetaka kununua vifaranga, anunue hapa hapa nchini. Kutibu magonjwa ya wanyama yanayotoka nchi nyingine ni gharama na hasara kubwa.
Haki za wanyama/ndege zinasemaje kuhusu huo uchomaji wa hao vifaranga? It is inhuman bora wawarudishe walikowatoa.
haki za wanyama zinasemaje??
maana kumuua kwa kumchoma moto mateso ni makali sana.. tena kifaranga.. bora awe kuku mzima
Asante kwa kunielimisha mkuu ingawa inasikitisha.tax compliant ,
Ukivirudisha, utasikia mamalaka za Kenya nazo zitakataa kuwa tayari vimefika Tanzania hata wanaweza wakasema vifaranga wamebadilishwa.
Kwa hiyo, hicho hakiwezekani tena.
Kuhusu haki za wanyama, kwenye ugonjwa hicho kifungu kinatenguliwa kwa kulinda haki ya binadamu ya kuishi kwa mujibu wa Katiba, mujibu wa Wizara inayohusika na Mifungo na hata WHO.
Kwa hiyo vitachomwa tu moto.
Asante kwa kunielimisha mkuu ingawa inasikitisha.
FRESHMAN ,
Ha ha ha ha ha , imebidi nicheke kwanza.
Mkuu, Haki za wanyama na za Binadamu za Binadamu zipo juu hasa panapotokea jambo la kuhatarisha uhai wa Binadamu hizo za wanyama tunaziweka kapuni kwanza.
Hicho kinafahamika kwa mfano, kwenye Katiba , Wizara inayohusika na mifugo , na hata WHO wanaelewa hilo zaidi hadi UN.
Mfano, Simba au mnyama yeyote akihatarisha maisha ya watu mtaani/ kijijini basi, huyo mnyama anauwawa ili kuokoa uhai wa wanadamu.
Hivyo , Uhai wa mtu mmoja tu ni bora mara 1+ Bilion kuliko vifaranga hata 10+Billionii.
point yako haitumiwi kwa faru fausta.. anajaliwa sana kuliko binadamu maelfu... ni bora binadamu wafe ila faru fausta abaki