Nahitaji Vifaa vya Ujenzi

RMshauri, Nabaki Africa nimepachungulia juu juu tuu juzi. Kuna hadisi nasikia watu wanasema kwa nyumba ya 150SQM inaweza kula Million 20-30 jee hii habari ni kweli kaka? Kama kweli sasa itabidi tupige bati la south lol. Maana hapo sijaongea na madirisha, tiles chini na makolokolo mengine.

Mkuu hiyo 150 sqm una maanisha saizi ya paa au? Kama ni paa si kweli maana paa langu lilikuwa ni sqm 354 na limekula Tshs. 27.3 mil. Hii ni gharama ya material yote yaliyotumika kwenye paa zikiwemo mbao na gharama za ufundi.
 
Wakuu kwa wale wenye uzoefu katika shughuli za ujenzi hebu tusaidiane hapa. Nahitaji kujua wapi naweza kununua nondo imara kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya ghorofa moja na bei yake ikoje kwa tani (eg za mm 8, 12 na 16). Je kweli kokoto nyeupe za mawe hazifai mpaka zile nyeusi tu za Lugoba na Msolwa? Je naweza kupata wapi tofali imara za concreate au vibrated? Bei zake zikoje?
Natanguliza shukrani zangu wakuu.
Mkuu thread ni long tyme. Hem niambie kwa sasa kagorofa kamoja kujenga inaweza ikala shs ngapi kila kitu roughly.
 
Mkuu hiyo 150 sqm una maanisha saizi ya paa au? Kama ni paa si kweli maana paa langu lilikuwa ni sqm 354 na limekula Tshs. 27.3 mil. Hii ni gharama ya material yote yaliyotumika kwenye paa zikiwemo mbao na gharama za ufundi.

Mkuu nilitaka kushangaa, basi nimeshatoa hofu sababu najua kwa M20 naweza maliza kazi yote na chenji ikabaki. Basi tuombe mungu plan inaanza January mungu akijalia.
 
Mkuu thread ni long tyme. Hem niambie kwa sasa kagorofa kamoja kujenga inaweza ikala shs ngapi kila kitu roughly.

Mkuu Ghorofa size matters. Mimi mwenza nilitaka kujenga nyumba ya SQM 300 ndani makolokolo kibao, wataalamu wakaniambia kaka unajenga gofu. Nikashusha mpaka 3 bedroom, ghrofa ya 12 kwa 13 small lakini reasonable. Hapo andaa kama M 100 complete mpaka kuamia. Kama unakwenda kama mzee shauri hapo juu, 357 sqm na kuendelea basi andaa M150 mpaka 200.

Lakini usiogope, kama unaijua engineering kidogo tuu unaweza bishana na fundi mchundo sababu wengi wamemeza. Mfano manondo ya M16 kila mahala that is nonsense, my A-level physics was enough to argue about it. Pili sijui tofali za chipping only kwa msingi sababu nguzo ndio zina bear weight not tofali. Nyumba yenye column 15+ hapo napo nikuumizana kichwa kama ni ghorofa moja. Sijui kokoto za msolwa, zile kokoto ni kwa ghorofa 4+, nunua 1/2 cubic meter not ubuyu, that will do the work.

Nina engineer mzee wa chuo kikuu ambae ndugu yangu alinipa, huyu fundi anakupigia kukwambia mzee sasa mifuko ya cement imebaki 30. Mwisho kupigwa ni lazima, only thing unapunguza %.
 
Naulizia bei ya nondo za mm 16 kwa bei ya rejareja
 
Naulizia bei ya nondo za mm 16 kwa bei ya rejareja

Mara ya mwisho mimi nililipia shilling 26,500 maeneo ya Tegeta. Kuna muda hizi nondo zilikuwa 33,500 sasa kama unataka kujenga anza sasa. Y12 ndio zinauzwa 15,000 kwa sasa.
 
Naomba ushauri na uzoefu wenu wadau kuhusu aina ya mabati, ubora and gharama zake katika suala la ujenzi. Je mabati au vigae vizuri? Je kuna mabati au vigae vinavyotengenezwa nchini vyenye gharama nafuu? Ubora ukoje? Naomba kuwasilisha.
 
Blocks-Email.jpg
glass blocks kwajili madirisha
 
Asante dada Belinda. Hizo nondo ulishawahi kuzitumia na ukajua ubora wake? Maana naambiwa kuna nondo zingine zinazotengenezwa TZ zinavunjika kama kuni. Hivi kuna watu wanao-import nondo kutoka nje zenye ubora zaidi?

Hapo kuna kweli though kwenye kuvunjika kama kuni sina uhakika (ila si imara maana nilishaona mfano ghorofa nyingi za Mwanza nondo zinatoka Dar na inasemekana nje ya nchi wakati MZA kuna kiwanda na ukizilinganisha zipo tofauti), japokuwa tunawalaumu wachina ila na sisi viwanda vya hapa nyumbani vinachakachua maana hizo nondo zenyewe zinatengenezwa kwa kutumia rawa materials kutoka majumbani kama masufuria, mabati, kopo, vyuma mchanganyiko n.k hata ukizigusa tu nondo ya 20ft unaweza kuikunja bila tabu.

Back to the point, jitahidi kufanya utafiti wa nondo nzuri na ngumu ili uweze kujenga kitu kizuri, uzuri wake unajenga ghorofa moja kidogo hata hizi nondo made in Tanzania but in chinese perspectives zinafaa
 
Na mimi kidogo nina kaproject kama kako, hila kama wenzangu walivyo zungumza humu nondo zinauzwa kwa tani bila kujali size yake, na nondo nyigi nzuri zinatoka nje hasa Uturuki, Malyasia, Africa Kusini hakuna nondo zinazo toka Urusi wale warusi pale TABATA nondo wanazo huza zinatoka Uturuki na bei zake kwa tani na kama walivyo quote wenzangu, hila mimi nilkuwa nataka kukupa ushauri kwamba kwa unafuu wa bei kanunue nondo katika kiwanda cha wahindi opposite na Kioo limited, nondo zao zinatengenezwa kutokana na billets kutoka nje kwa hiyo ni za kiwango cha hali ya juu sana na demand yake hapa nchini ni kubwa kwa sasa hivi wamesimamisha kidogo kutokana na kusubili mali ghafi kutoka nje.

Kuhusu kokoto mimi natumia kokote ngumu kama mawe na siyo ubuyu, au za kutoka msolwa au nini. Hizi za msolwa packing density yake ni kubwa sana na sidhani unahitaji kitu kama hicho kwenye ujenzi wako, nyenzo nyingine za ujenzi zinapatikana kirahisi tu.

Wakuu nondo ya MM steel Mwenge-Itv ni Imara pia
 
Hahaha,mihela yote hiyo kha.
Mie nilidhani ni around 300m.

Mkuu ukiwa na 300M unajenga mjengo wa maana sana tu pengine wenye mvuto kuliko hata huo wa mchungaji. Hapa kuna mambo mengi ya kuangalia. Je kiwanja chako ni tambarare na hakiko kwenye udongo wa mfinyanzi? kama jibu ni ndiyo ina maana utatumia pesa kidogo kujenga msingi ambao ndo hula pesa nyingi sana kwa ghorofa. je umetumia kampuni kujenga? Gharama za ujenzi hapa ni kubwa ukilinganisha na aliyetumia mafundi wa kawaida. Pia usimamizi wako wa karibu ni muhimu kuhakikisha kuwa pesa zako zinatumika ipasavyo na si kuishia mifukoni mwa watu.
 
Mkuu ukiwa na 300M unajenga mjengo wa maana sana tu pengine wenye mvuto kuliko hata huo wa mchungaji. Hapa kuna mambo mengi ya kuangalia. Je kiwanja chako ni tambarare na hakiko kwenye udongo wa mfinyanzi? kama jibu ni ndiyo ina maana utatumia pesa kidogo kujenga msingi ambao ndo hula pesa nyingi sana kwa ghorofa. je umetumia kampuni kujenga? Gharama za ujenzi hapa ni kubwa ukilinganisha na aliyetumia mafundi wa kawaida. Pia usimamizi wako wa karibu ni muhimu kuhakikisha kuwa pesa zako zinatumika ipasavyo na si kuishia mifukoni mwa watu.
Mkuu ntakutafuta.
Binafsi nataka kujenga gorofa 1 ya ukweli morogoro.
Nahisi una idea na hivi vitu.
Thanks a lot mkuu.
 
Back
Top Bottom