Nunua kwanza hicho kinanda na mashine ya Sampler. Pia nunua Computer yenye Sound Cad nzuri na hiyo program yako uwe unarekodi hizo sampler zako kutoka kwenye kinanda na Sampler mashine na baadaye zote unaziunga kwenye hiyo program yako na kuwa na mziki tayari. Utakavyokuwa ukiendelea, ndiyo utaanza kuona umuhimu wa kuwa na aina nyingine ya mashine. Hapo utakuwa na uhakika, mashine gani hasa unahitaji na siyo kuruka na kusema nataka vyombo vya Studio.
Njia nzuri sana ambayo hata Producer kama Larock walifanya ni kufanya kazi Studio na huko unapata shule moja nzuri sana. Unaweza kuwa unafanya hata BURE. Unamwambia jamaa akuonyeshe na unakuwa ukifanya kazi zake kidogokidogo. Hatakuonyesha vyote ila siku zinavyokwenda, mengine utajisomea mwenyewe maana ngumu siku zote ni kuanza.
Kila la kheri katika safari yako.