nkyalomkonza
JF-Expert Member
- Jun 18, 2012
- 1,154
- 443
Jk yuko sahihi
Hivi kuna kitu chochote kutoka kwa JK au CCM ambacho hakipo sahihi kwako?
Wameshawamaliza akili kila kitu kusifia tu kama mazuzu.
Jk yuko sahihi
Kwa mlio msikiliza anasemaje kwa ufupi maana kheri niambiwe kuliko kumsikiliza.
Hivi kuna kitu chochote kutoka kwa JK au CCM ambacho hakipo sahihi kwako?
Wameshawamaliza akili kila kitu kusifia tu kama mazuzu.
Unajua Katibu wenu yuko ujerumani anafanya nini? Safari ya mwezi and so........, unajua nafasi ya ukatibu mkuu? Sasa mtu kama huyu ndo hajawa rais, akiwa rais si atatelekeza taifa?[/sa kuwa na ma]
Katibu wa nani? Unajua mimi ni chama Gani?.
Mimi nazungumzia watu kama nyie mliokuwa kama mazuzu, kila kitu kusifu tu.
Mkumbushe kuwa KIZURI HUJIUZA NA KIBAYA HUJITEMBEZA.With the resources we have haitaji izo safari nyingi kiasi icho.MABEPARI WAKO BIZE KUSAKA RASILIMALI AFRICA HUITAJI KUWAFUATA WANAKUJA WENYEWE.kasema Asipoenda nje ya nchi, hawatakuja kumtembelea. Sisi ni maskini, lazima tutoke ili nao waje kuwekeza.
Mmh......huyo wa China ziara moja tu kapewa Bandari....huyu wetu ziara 300 hata Ngarawa hakuna
kasema Asipoenda nje ya nchi, hawatakuja kumtembelea. Sisi ni maskini, lazima tutoke ili nao waje kuwekeza.
Hatulalamiki kwanini anaenda nje, tunacholalamika safari zimezidi kama vile yeye ni waziri wa mambo ya nje. Na kitu kingine kinashangaza kwenda nje kuwaalika watu waje kutuibia natural resources zetu. Kama sisi hatuna uwezo bora tuziache ardhini mpaka tutakapo pata uwezo. Ndio maana mikataba inakuwa mibovu kwa sababu tunawabembeleza waje kuwekeza. Wawekezaji wa ndani ni wa muhimu kuliko wa nje, serikali ijaribu kuelimisha watu wake kuwekeza, kuliko kupoteza muda kuzunguka nje kutafuta wawekezaji. Elimu bora na uzalendo ndio imewafikisha wenzetu walipo huko mnakoenda kushangaa na si wala safari za kutembelea nchi zilizoendelea. Safari za mara kwa mara si uzalendo kwa nchi yetu hata kidogo.
Kwanini wenyewe hawaji kutuambia tukawekeze kwao
Hakuna safari iliyonikera na kunifedhehesha kama hii "aliyodandia" kwa Ngeleja......Rais wa nchi yangu kuvishwa name tag ilikuwa fedheha sana!....na hakukuwa na Rais mwingine hata wa Burundi hakuwepo!
Hata haiingii akilini rais wa nchi anapokuwa kinara na mratibu wa mauaji ya raia wake!! Huyu bwana sijui ana laana ya namna gani!!!! Kikwete hizi hoja zako zinawafaa nini watanzania ambao hata hawamudu mlo mmoja kwa siku! Hayo maisha bora uliyowadanganya wananchi yako wapi? Shame on you!!!!!!!!
wewe mkuu huu wivu utakuuwa umekaa kumchukia rais na kumnunia wakati mzee anafanya kazi za taifa na kuwatumikia watu wake hizo chuki zenu za asili za kuchukia watu hata hazina nafasi.