Video: Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akinaswa kibao na mwananchi

Watu wawili wametiwa mbaroni wakihusishwa na tukio la kumpiga kofi Rais wa Ufaransa, Emmanuel macron alipokuwa katika ziara rasmi Kusini mwa Taifa hilo.

Katika video inayosambaa mitandaoni, mtu huyo anaonekana kumchapa Rais Macron kabla ya kudhibitiwa na maafisa usalama, wakifanikiwa kumwondoa Rais, huku maneno “U-Macron uondoke” yakisikika.

View attachment 1812533

Rais Macron yupo ziarani akitembelea maeneo mbalimbali ya Ufaransa, ziara yake ikitajwa kuwa na umuhimu mkubwa kwa kuwa ni siku moja tu kabla ya taifa hilo kuruhusu kufunguliwa kwa migahawa na baa baada ya kufungwa kwa miezi 7 kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Rais Macron ataendelea na ziara yake katika eneo hilo siku ya kesho.

Chanzo: BBC
Najaribu kufikir hao security wa rais wangechelewa kidg je rais angeweza kujitetea juu ya hicho kisanga.
 
Bora hata hicho kibao, waziri mkuu wa kule kwa Bibi enzi hizo, Bw. John Major alikung'utwa na yai viza!
 
Jamaa kampiga kibao cha dharau
Ndo maana walinzi wetu huku they take no chances rais unampungia tu
Maana suala kama hili lingetokea bongo sipatii picha
 
Dah huyu jamaa bila shaka anavuta mibangi , unampigaje President bana sipati picha kwetu angekula virungu vya ugoko hadi anyooke🤔
 
Mnaogopaga Bure Tu.
Wewe liamshe Tu KUKUUA sio rahisi
Ingekuwa bongo afu amlambe mwendazake ukofi wa namna hiyo....

Hakyamama kabla hajapotea kama Ben Saanane, angekuwa kashachezea kichapo cha risasi laki nane na nusu...
 
Angekua hapa bongo enzi za KAYAFA angekula kisago zaidi ya alichokula Yesu pale msabani....

Kifupi ange sagwa sagwa
Hata sasa hivi akimchapa Mama Samia kibao lazima apotee kwani aliyemchapa Rais Mwinyi tena akiwa ameshastaafu yupo?!!
 
Mzungu akiwa mwehu anakuwa mwehu kwelikweli..no hesitation.

Kibenten cha mtu(macron) kanaswa kibao kimoja matata sasa..yule mkewe mzee atakuwa anamkanda tu saiv.
 
Walinzi walichelewa kufika upande wa kushoto wa rais ... wamefanya makosa ya kijinga kabisa ...wamejitia aibu ya mwaka
Uzembe wa hali ya juu sana! Wana bahati sana mpiga kofi hakuwa na silaha. Isitoshe, hakujipanga vyema kumfanyia rais shambulizi.

Mpaka rais anamsogelea na kumshika mkono mpiga kofi, tayari kulikuwa na upenyo mkubwa sana wa rais kushambuliwa. Walinzi wana bahati sana shambulizi halikuwa kubwa kiasi cha kutishia uhai.
 
Ingekua ni mwenyemeza wa Chadede hapo,

Wanakuchacha wangwe tu.
 
Back
Top Bottom