A_S_K_F
New Member
- Jun 3, 2021
- 3
- 2
Najaribu kufikir hao security wa rais wangechelewa kidg je rais angeweza kujitetea juu ya hicho kisanga.Watu wawili wametiwa mbaroni wakihusishwa na tukio la kumpiga kofi Rais wa Ufaransa, Emmanuel macron alipokuwa katika ziara rasmi Kusini mwa Taifa hilo.
Katika video inayosambaa mitandaoni, mtu huyo anaonekana kumchapa Rais Macron kabla ya kudhibitiwa na maafisa usalama, wakifanikiwa kumwondoa Rais, huku maneno “U-Macron uondoke” yakisikika.
View attachment 1812533
Rais Macron yupo ziarani akitembelea maeneo mbalimbali ya Ufaransa, ziara yake ikitajwa kuwa na umuhimu mkubwa kwa kuwa ni siku moja tu kabla ya taifa hilo kuruhusu kufunguliwa kwa migahawa na baa baada ya kufungwa kwa miezi 7 kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.
Rais Macron ataendelea na ziara yake katika eneo hilo siku ya kesho.
Chanzo: BBC