Huyu kingunge apimwe akili walizoea kufanya nchi kama yao ndiyo maana aliona ahamie chadema amfuate lowassa kukamilisha genge la kumuwezesha lowassa awe rais ili mambo yao yale ya kufisidi nchi hii yaendelee, inasikitisha sana kwa mzee kama huyu kutanguliza tumbo kuliko maslahi ya wanyonge ni upumbafu kabisaMzee Kingunge ni aina ya wale wazazi waliokuwa wanaongoza shuleni kila somo lakini cha kushangaza hawakupata elimu na kuishia madarasa ya awali kabisa, kila akizungumzia shule utamsikia enzi zangu mimi.
Yeye atakumbukwa kwa lipi kama waziri na mkuu wa zamani, na kiongozi mwandamizi wa chama chao kilichoasisi ufisadi Tanzania?
Mzee Kingunge hajawahi kuwa mshauri mzuri kuanzia kwa serikali aliyoitumikia tangu akiwa kijana na mpaka leo na chama chake cha zamani.
Katika watu wanaotakiwa kuomba radhi kwa Watanzania Mzee Kingunge yupo na CCM wote.
Taratibu za chama zimekiukwa 2015 je 1995 na 2005 hazijakiukwa? Au kwasababu kulikuwa na ujinga wao wa kuachiana ndio ikambidi avute subira?
Nchi hii ina uongozi mbovu ila Kingunge alikuwa mbovu zaidi kama kina Msukuma tu, kama ni ujasiri alikuwa wapi kina Mbowe, Maalim, Mbatia, Lipumba walipokuwa wanaichachafya ccm na kujiweka mstari wa mbele kwenye mapambano?